TIGO mtaani kwa sasa ni neno tata kwani linafarakanisha watu kutokana na jina hilo kutumiwa kwa matusi,hili linaishusha hadhi na watu waoheshimiana huogopa kuwa na mtandao huo kuogopa kutaja neno hilo.Je ili kulinda heshima ya kampuni si vema kubadili jina hilo kuachana na matusi?Hivi ni nini chanzo cha neno hilo kutumika kama matusi?Wanajamvi changieni.
mkuu kweli kabisa.....siku hizi JF hamna great thinking.....thread za kipuuzi puuzi kila siku.....alafu kumezuka siku hizi kila kitu udini..kuna watu sijui wametumwa kila kitu wenyewe wanasema ni udini....najua nia yao.....
....msione watu mnaowaulizia wamepotea... ni wapo lakini wanasoma upupu wenu na kusikitika....
....tubadilike thread za upupu hazifai.....kuna thread ambazo mpaka mtu unajiuliza hii ni JF?
Wewe unafikiri ni mzaha lakini watu wanadundana mtaani kwa neno TIGO.Hata wewe ukiwa mtaani mwambie mtu nipe TIGO yako uone muziki wake.This thread shows how much people are not serious and concentrating on issues. It disappoints to see the way our thinking resources are applied.
Do we still need someone to blame?
kuna haja ya kubadilisha fikra zetu!!
mkuu,
ahsante sana kwa angalizo hili muhimu. Nadhani iko haja mods na uongozi wa jf ufanye tathmini mahsusi kabisa itakayoangalia uwezekano wa kupunguza kasi hii ya 'threads upupu'. The way i see, mwendo huu ninaufananisha na uvamizi wa viwavi-jeshi katika shamba, tusipokuwa wangalifu ubora wa jf utaporomoka kwa kasi kama si kwa kishindo.
TigO......Kisamvu walikuwa wanamaanisha nini ati?
hahaaa mkuu you make my day..nimecheka sana...bega kwa bega sio kukaa nyuma yanguuu wanikumbusha mambo la LAMU mieInabidi wabadilishe staili tu kama vile Mzee Kenyatta alivyofanya kule Mombasa.
Mzee Kenyatta akitoa hotuba yake mjini Mombasa, watu wakawa wanamshangilia na kusema mzee sisi tupo nyuma yako.
Kenyatta akawajibu " Nyinyi watu ya Mombasa mnafanya nini nyuma yangu, sema twende bega kwa bega. Hapana kaa nyuma angu".
Kwanini kampuni hii tu ndio inabatizwa majina mabaya? Why not Tritel au Celtel na sasa Zain? Is it something to do with business competition?Nakumbuka kwanza ilikuwa mobitel, watu wakaita wasichana wadogo wadogo vimobiteli. Then Ikaitwa BUZZ, wababa wapenda vimwana wakaitwa mabuzi. Inaitwa tigo, tayari ishapewa tafsiri nyingine. Nawahakikishia hata ikipewa jina jingine bado watapewa tafsiri mpya. Cha msingi si kubadili jina ila kubadili FIKRA!! Namsapoti Mchungaji Mwema, tubadili fikra, si jina!! Mchungaji Mwema, chunga kondoo wako vizuri.