Kuna haja gani ya kuwapongeza mafisadi waliojiuzuru

Shukurani

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
251
11
Jana katika kikao cha bunge, wachangia hoja waliopata nafasi waliwapongeza Lowasa, Karamagi na Msabahaa kwa uamuzi wao wa kujiuzuru. Kwa upande wangu sikuona sababu ya kuwapongeza watu ambao wameshindwa kutimiza wajibu wao na kulitia taifa hasara kubwa. Kiujumula Lowassa alitakiwa ajiuzuru toka miezi sita iliyopita baada ya serikali kuonyesha udhaifu mkubwa sana kwa kuingia mkataba na kampuni hewa,hii ni fedheha kubwa sana. Ndani ya baraza la mawaziri kulikuwa na PhD ngapi? na masters ngapi? zisiweze kujua mambo haya, sitaki kuamini unahitaji elimu kubwa kugundua utapeli wa watu. Ni uzembe uzeembe, sihitaji kumpongeza fisadi yeyote kwa kujiuzuru. nitampongezaje mtu anayeniumiza kwa kunipandishia bei za umeme kila kukicha, ni wendazimu huu. nitalazimika kuwataka wale wote waliowapongeza mafisadi hawa wafute kauli zao ama wajiuzuru,
 
Thats right man..sioni sababu kabisa ya kuwapapongezi hao mafisadi..nasikia JK katoa order kuwa account zao ziwefreezed soon na hawaruhusiwi kusafiri kwa sasa..ni hatua nzuri hii nadhani ss tunapokwenda ndio kwenye UTAMU..huchelewi kusikia muhusika amepatwa na kiharusi ghafla au hypertension!!
 
Thats right man..sioni sababu kabisa ya kuwapapongezi hao mafisadi..nasikia JK katoa order kuwa account zao ziwefreezed soon na hawaruhusiwi kusafiri kwa sasa..ni hatua nzuri hii nadhani ss tunapokwenda ndio kwenye UTAMU..huchelewi kusikia mhusika amepatwa na kiharusi ghafla au hypertension!!
 
Senator hilo naliunga mkono kama ni kweli. Lete source Senator
 
Mimi nitatoa pongezi kwa yule atakayerudisha hizo fedha alizojichotea. kama mtu ana mijihela mingi ya kutosheleza hata vitukuu vyake hakuna chochote kilichopungua katika maisha yake sana sana amepata muda wa kutungua hizo fedha alizojichukulia.

Warudishe hizo fedha and if they suffer from hypertension in the process who cares.
 
Hata mimi nilijaa upepo sana kumsifia mtu aliyepora mali za wananchi kwa ubinafsi wake.Imagine mtu analipwa 152M kwa siku kwa miaka 2 azalishe au asizalishe.Alafu leo apongezwe kwa kuachia ngazi!,Siasa kweli si hasa bali.......
Nachelea sasa kuamini kuwa mzimu wa Rich monduli uliwajumuisha wengi.Siamini kuwa wahusika ni wale waliotajwa tu?
Basi la abiria haliwi na dereva tu,lazima liwe na tingo na fundi makenika,abiria,mizigo tool box n.k. Nadhani umefuatilia ripoti imetaja maeneo mengi ktk wizara husika na watu mbalimbali.
EL,LA na karamagi lazima walikuwa na back up kubwa bungeni ili mzimu huo uendelee kuishi bila ya kufa.Kwa nini haukufa mapema mpaka kamati teule ilipakua yaliyofichika?
Msafara wa mamba na kenge nao wamo.
 
Back
Top Bottom