101 East
JF-Expert Member
- Feb 25, 2015
- 1,040
- 2,118
Nipo Benjamin William Mkapa nasoma kipindi kile (2002-2005) huwa kuna swali najiuliza:
Hivi hizi Chemistry, Biology, Physics, Mathematics, History, Book-Keeping, Civics, English, Kiswahili na Geography huko Ulaya nao wanasoma hizihizi kweli!?
Mbona wenzetu wakimaliza masomo mpaka chuo wanakuwa watu wenye mawazo,maono na fikra zinazoendana na nafasi zao katika jamii zao na serikali. Mbona wenzetu wakimaliza masomo kama ni mwanasiasa anakuwa mwanasiasa na mleta mabadiliko ya kweli na si ubaguzi?
Kama ni injinia anaijenga nchi yake kwa
majengo marefu,barabara nzuri,viwanda vya magari na kila aina ya ubunifu na uvumbuzi wa kisayansi kwa nchi yake
Kama ni daktari anatibu na kutengeneza
kinga dhidi ya magonjwa,uvumbuzi wa dawa mpya za magonjwa mbalimbali na vifaa tiba
Kama ni mfanyabiashara anakuja kuwa mfanyabiashara mkubwa duniani na kutufikia sisi hizo bidhaa zake na kampuni zake kusambaa na kuja hata kuajiriwa na sisi huku Africa
Mbona huku kwetu ni tofauti kabisaa yani mkimaliza chuo wale mainjinia wanaenda kuwa wachungaji,waganga wa kienyeji na matapeli
Wale madaktari wanaenda kuwa madaktari wa kuwapa watu Panadol,kutoa mimba na migomo ya mishahara
Wale wanasiasa wanaenda kuwa waalimu wa vyuo vikuu na wakuu wa wilaya,wanasaikolojia na ma MC's WA sherehe
Wale waliosoma history na arts schools kule chuo na sekondari wanakuja kuwa bodaboda,motivational speakers,mabraza men na matapeli
Sasa katika kundi hili la graduates mmoja Wapo paap anakuwa raisi wa nchi hivi unafikiri ataamini tafiti za kisayansi,atasikiliza ushauri wa wataalam wa afya,atasikiliza majibu ya tafiti
Hivi Viongozi wetu wa Africa kama hawaamini sayansi,madaktari,na tafiti mbalimbali kuhusiana na magonjwa,mafuriko,hali ya hewa,matetemeko ya Ardhi,uchumi basi hakuna haja ya kuwa na taifa la wasomi wala kuwa na Viongozi wasomi wa PhD,degree wala diploma tutambulishane na kupeana madaraka kwa uwezo wetu wa kupiga maombi,kupiga ramli,kusoma ahlal badil,kupaa na ungo,kuweka misukule labda hili litatusaidia maana ndio wengi wetu tunaamini huko kuliko kupambana na janga Kama la CORONA covid19 kwa njia za kisayansi.
Asanteni nawasilisha
Sent using Jamii Forums mobile app
Hivi hizi Chemistry, Biology, Physics, Mathematics, History, Book-Keeping, Civics, English, Kiswahili na Geography huko Ulaya nao wanasoma hizihizi kweli!?
Mbona wenzetu wakimaliza masomo mpaka chuo wanakuwa watu wenye mawazo,maono na fikra zinazoendana na nafasi zao katika jamii zao na serikali. Mbona wenzetu wakimaliza masomo kama ni mwanasiasa anakuwa mwanasiasa na mleta mabadiliko ya kweli na si ubaguzi?
Kama ni injinia anaijenga nchi yake kwa
majengo marefu,barabara nzuri,viwanda vya magari na kila aina ya ubunifu na uvumbuzi wa kisayansi kwa nchi yake
Kama ni daktari anatibu na kutengeneza
kinga dhidi ya magonjwa,uvumbuzi wa dawa mpya za magonjwa mbalimbali na vifaa tiba
Kama ni mfanyabiashara anakuja kuwa mfanyabiashara mkubwa duniani na kutufikia sisi hizo bidhaa zake na kampuni zake kusambaa na kuja hata kuajiriwa na sisi huku Africa
Mbona huku kwetu ni tofauti kabisaa yani mkimaliza chuo wale mainjinia wanaenda kuwa wachungaji,waganga wa kienyeji na matapeli
Wale madaktari wanaenda kuwa madaktari wa kuwapa watu Panadol,kutoa mimba na migomo ya mishahara
Wale wanasiasa wanaenda kuwa waalimu wa vyuo vikuu na wakuu wa wilaya,wanasaikolojia na ma MC's WA sherehe
Wale waliosoma history na arts schools kule chuo na sekondari wanakuja kuwa bodaboda,motivational speakers,mabraza men na matapeli
Sasa katika kundi hili la graduates mmoja Wapo paap anakuwa raisi wa nchi hivi unafikiri ataamini tafiti za kisayansi,atasikiliza ushauri wa wataalam wa afya,atasikiliza majibu ya tafiti
Hivi Viongozi wetu wa Africa kama hawaamini sayansi,madaktari,na tafiti mbalimbali kuhusiana na magonjwa,mafuriko,hali ya hewa,matetemeko ya Ardhi,uchumi basi hakuna haja ya kuwa na taifa la wasomi wala kuwa na Viongozi wasomi wa PhD,degree wala diploma tutambulishane na kupeana madaraka kwa uwezo wetu wa kupiga maombi,kupiga ramli,kusoma ahlal badil,kupaa na ungo,kuweka misukule labda hili litatusaidia maana ndio wengi wetu tunaamini huko kuliko kupambana na janga Kama la CORONA covid19 kwa njia za kisayansi.
Asanteni nawasilisha
Sent using Jamii Forums mobile app