Kuna haja gani kusoma kama huwezi kukumbuka ulichosoma?

FikraPevu

JF-Expert Member
Jan 2, 2010
303
236
Kwa mujibu wa Jhumpa Lahiri katika kitabu chake cha The Namesake anasema, “ Kusoma kitabu ni kitendo cha kusafiri bila kusogea kutoka pale ulipo”. Naye David Bowie msanii ajulikanaye kama msomaji mkubwa wa vitabu; alipokuwa akijibu maswali mbalimbali aliyoulizwa kwenye dodoso, alipoulizwa kuhusu maana halisi ya “furaha ya kweli ni ipi?”, Bowie alijibu ni kusoma.

Hata hivyo, kuna haja gani kusoma kama huwezi kukumbuka ulichokisoma? Hakuna kitu kinakatisha tamaa kama kuwekeza muda wako kusoma kitabu fulani halafu baadaye ukasahau vyote ulivyosoma. Kuendelea kusoma kitabu fulani ambacho taarifa zake za mwanzo umezisahau ni kama kusoma kitabu kipya kwa kuanzia katikati ya matukio.

Bill Gates husoma vitabu takribani 50 kila mwaka na alitumia njia hizi kuweza kukumbuka yote aliyoyasoma kwenye vitabu hivyo 50;

- Tambua kile kinachokuvutia

- Nakili au andika kile ulichojifunza

- Wasimulie wengine ulichosoma

- Tafakari na husianisha kile ulichosoma na matukio yanayokuzunguka

Zaidi, soma hapa => Fahamu njia 7 za kukusaidia kukumbuka kila kitu ulichosoma
 
Kwa mujibu wa Jhumpa Lahiri katika kitabu chake cha The Namesake anasema, “ Kusoma kitabu ni kitendo cha kusafiri bila kusogea kutoka pale ulipo”. Naye David Bowie msanii ajulikanaye kama msomaji mkubwa wa vitabu; alipokuwa akijibu maswali mbalimbali aliyoulizwa kwenye dodoso, alipoulizwa kuhusu maana halisi ya “furaha ya kweli ni ipi?”, Bowie alijibu ni kusoma.

Hata hivyo, kuna haja gani kusoma kama huwezi kukumbuka ulichokisoma? Hakuna kitu kinakatisha tamaa kama kuwekeza muda wako kusoma kitabu fulani halafu baadaye ukasahau vyote ulivyosoma. Kuendelea kusoma kitabu fulani ambacho taarifa zake za mwanzo umezisahau ni kama kusoma kitabu kipya kwa kuanzia katikati ya matukio.

Bill Gates husoma vitabu takribani 50 kila mwaka na alitumia njia hizi kuweza kukumbuka yote aliyoyasoma kwenye vitabu hivyo 50;

- Tambua kile kinachokuvutia

- Nakili au andika kile ulichojifunza

- Wasimulie wengine ulichosoma

- Tafakari na husianisha kile ulichosoma na matukio yanayokuzunguka

Zaidi, soma hapa => Fahamu njia 7 za kukusaidia kukumbuka kila kitu ulichosoma
Asante Mkuu
 
alberteinstein1-2x.jpg


mkuu asante kwa motisha na elimu.
nadhani hata kama mtu anaPHD au Masters lakini amekaa muda mrefu kiasi cha kukumbuka mambo ya shule ya msingi au sekondari zaidi ya hayo aliyobobea au hawezi kiyaaply kwenye jamii kwa maoni ya mkuu Einstain elimu ya mtu huyo ni ya sekondary katika uhalisia.
 
Back
Top Bottom