Kuna faida gani kuwatengea wanawake "Viti maalum" 110 vya ubunge?

maramia

JF-Expert Member
Jul 17, 2015
2,030
1,344
Siku zote sikuwahi kujua wala kufikiri kwamba idadi ya viti maalum vya wanawake bungeni inaweza kufikia hii, yaani viti 110, kwa ujinga wangu nilidhani ni chini ya viti 50.

Lakini viti maalum 110, yaani karibu nusu ya wabunge wa kuchaguliwa ambayo namo bado kuna wanawake, kuingia akina mama wengine 110 kinamna ktk chombo nyeti cha kutunga sheria kama bunge naona kuna mushkeli mkubwa tena sana.

Kwa hatua tuliyofikia ya kutoa haki na vigezo vilivyo sawa kwa jinsia zote katika hatua zote za kugombania nafasi za udiwani, ubunge na urais, sioni kama tuna haja tena ya kuwa na viti vingi vya upendeleo kiasi hiki.

Nimejaribu kupekua na kupitia katiba za nchi wenzetu walio katika jumuiya ya madola ambayo na sisi ni mjumbe wa mabunge yake nimegundua kuwa Tanzania ndiyo nchi pekee yenye kuwa na idadi kubwa ya viti vya upendeleo kwa wanawake ndani ya bunge.

Fikiria mlolongo wa shida, matatizo na mdororo wa kiuchumi walionao watanzania lakini bado kuna wabunge 110 wanawake wamewekwa bungeni, wengine wakiwa wameingia tu kishikaji au kimahusiano binafsi kwa malipo ya kodi ya watanzania.

Fikiria pia madeni ya waalimu, ukosefu wa dawa hospitalini, madeni ya wakandarasi, ukosefu wa maji na mengine mengi lakini bado kuna wabunge wanalipwa bila ya kuwa na jimbo wanaloliwakilisha, wanabaki ni wa kudandia dandia tu hoja za wenzao bungeni na kutetea vyama vyao ndani ya bunge.

Nadhani wakati umefika sasa wa kuvipruni viti hivi na kubakiza viti 40 tu au kuvifuta kabisa na wanawake wanaotaka ubunge warudi kugombea kwenye majimbo yao badala ya kuvizia kutafuna kodi yetu huko bungeni bila kazi maalum. Binafsi sioni kama umuhimu wa wabunge hawa unalingana na mabilioni ya kodi yetu wanayotafuna.

Kama Tanzania tumefikia hatua ya mwanamke kugombea urais akashika nafasi ya tatu mbele ya wagombea wanaume watano, na hata kumpata makamo wa Rais mwana mama bado tunadhaniaje wanawake ni wa kupewa upendeleo?
 
Hiyo sheria ya viti vingi hivyo ilipitishwa na wabunge wanaume wakware, watu waliona wanakosa vimada ikabidi waandae miundo mbinu. Sasa hivi huko bungeni labda ushindwe tu kuimbisha. Halafu kumbuka hili kundi la viti maalum hasa wa ccm huwa wameshikiwa akili na serekali, kila kitu cha serekali wao wanaunga mkono bila kujiuliza.
 
Viti vyenyewe eti anapewa watoto wa ditopile , sijui dr Nani ... Aiseee chadema nao eti wakampendekeza mama lowasa.. Dah!! Hii nchi .
 
Ndiyo ifike muda wananchi tuache kufikiri kuwa hawa viongozi kuwa wanaumizwa sana na matatizo tuliyonayo kwa kuyaongea tu.
 
Ndio sehemu moja wapo vyama huungana na kuwageuka wananchi katika kufuja pesa za walipa kodi. . . . !!!

Endeleeni kushabikia vyama
 
Sina chama ila upinzani unaniudhi kwa tabia yake ya kujifanya ina umizwa na matatizo yetu hali ya kuwa kiuhalisia hawako hivyo,hucheza na hisia zetu za matatizo tuliyonayo,mambo mengine hayaitaji hadi uingie ikulu.
 
Hiyo sheria ya viti vingi hivyo ilipitishwa na wabunge wanaume wakware, watu waliona wanakosa vimada ikabidi waandae miundo mbinu. Sasa hivi huko bungeni labda ushindwe tu kuimbisha. Halafu kumbuka hili kundi la viti maalum hasa wa ccm huwa wameshikiwa akili na serekali, kila kitu cha serekali wao wanaunga mkono bila kujiuliza.

Astaghafilullah!!
Tangia nimeanza kuandika humu JF, leo Tindo umenichekesha sijawahi kucheka kiasi hiki, yaani "Ushindwe mwenyewe kuimbisha" na kumwaga sera ya kumpata mbunge wa "kitu maalum"
 
Kuna haja ya kupunguza idadi hii ya viti maalum ukweli wabunge 110 ni mzigo usio wa lazima kwa taifa naomba ifike mahala tuondoe kabisa sheria hii watu wote wachaguliwe na wananchi, kama kuteua ibaki idadi ndogo kwa rais kuteua tena inapolazimu.
NEC tunaomba mtuondolee mzigo huu watanzania ni bora bunge liwe dogo na fanisi.
 
kuna haja ya kurekebisha sheria uwiano uwe 50 kwa 50 wanawake na wao wagombee na kushindana kama ilivyo uchaguzi wa majimbo ili wanawake waende kwa uwezo wao
 
Tulitaka kuunda bunge dogo lenye wabunge wasiozidi 70 ukawa wakasusia tukachakachuliwa na akina change.
 
kazi na dawa. hiyo ni posho ya wakubwa wewe inakuuma kwa sababu hujawa mbunge ukiwa mbunge utaona faida ya kukaa jirani na hao wadada yaani spika anongea wewe mkono upo sehemu sehemu unatafuta network halafu unamuuliza spika hapo umesemaje nilikuwa busy kidogo.
 
kazi na dawa. hiyo ni posho ya wakubwa wewe inakuuma kwa sababu hujawa mbunge ukiwa mbunge utaona faida ya kukaa jirani na hao wadada yaani spika anongea wewe mkono upo sehemu sehemu unatafuta network halafu unamuuliza spika hapo umesemaje nilikuwa busy kidogo.

Mkuu umefanya nicheke sana
 
hii kitu ufutiliwe mbali nchi changa tunajitwika mizigo kufurahisha ulimwengu wakiti kiuhalisia hatuna uwezo huo.
 
Ni kweli ni mizigo, lakini hizi si ndizo Sera za serikali yetu sikivu? Sidhani kama huu ni wakati muafaka kulalamikia haya. Tulipewa muda na tumeutendea haki. So sioni jipya hapa.
 
Kuna haja ya kupunguza idadi hii ya viti maalum ukweli wabunge 110 ni mzigo usio wa lazima kwa taifa naomba ifike mahala tuondoe kabisa sheria hii watu wote wachaguliwe na wananchi, kama kuteua ibaki idadi ndogo kwa rais kuteua tena inapolazimu.
NEC tunaomba mtuondolee mzigo huu watanzania ni bora bunge liwe dogo na fanisi.

Hili la viti maalum limo ndani ya katiba au chini ya NEC?
 
kazi na dawa. hiyo ni posho ya wakubwa wewe inakuuma kwa sababu hujawa mbunge ukiwa mbunge utaona faida ya kukaa jirani na hao wadada yaani spika anongea wewe mkono upo sehemu sehemu unatafuta network halafu unamuuliza spika hapo umesemaje nilikuwa busy kidogo.

Yaani hiyo ya kutafuta "Network" ndiyo faida?
 
Back
Top Bottom