Anderson Ndambo
Senior Member
- Jun 3, 2017
- 152
- 207
Kuna kila dalili ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuchanganyikiwa baada ya Waziri wa Fedha, Philip Mpango kuwasilisha bajeti yake. Mapokeo ya bajeti hiyo ni makubwa na kwa mara ya kwanza magazeti yote hata yale ya kambi yetu yanaunga mkono.
Hadi sasa, hakuna kiongozi yeyote wa kambi ya upinzani aliyetoa maoni yake kupinga bajeti hiyo na wale waliojaribu kuizungumzia ama wanasema Serikali imesikia kilio chetu ama wanasema japo bajeti ni nzuri, ila haitatekelezwa.
Kwa kweli niseme kwa dhati ya moyo kuwa Mipango ya Waziri Mpango imechanganya Kambi Rasmi ya Upinzani. Hotuba yetu imeandaliwa na Halima Mdee ambapo nilipoipitia kwa kweli imejaa malalamiko badala ya uhalisia.
Kwa vile Waziri Kivuli wa Fedha, Halima Mdee yupo Kifungoni, Naibu wake, David Silinde ndiye atakayewasikisha Hotuba hiyo. Hata hivyo, hayupo tayari kuiwasilisha kwa vile haina hoja za maana.
Kwa hali hiyo, wabunge wa Upinzani wamekubaliana kususia mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali na watatumia hoja ya kufungiwa akina Halima Mdee na Esther Bulaya kama kisingizio cha kutoshiriki mjadala huo. Kuna uwezekano mkubwa Wabunge wa Upinzani wataingia Bungeni Jumatatu na kutoka nje baada ya kipindi cha maswali na majibu.
Hadi sasa, hakuna kiongozi yeyote wa kambi ya upinzani aliyetoa maoni yake kupinga bajeti hiyo na wale waliojaribu kuizungumzia ama wanasema Serikali imesikia kilio chetu ama wanasema japo bajeti ni nzuri, ila haitatekelezwa.
Kwa kweli niseme kwa dhati ya moyo kuwa Mipango ya Waziri Mpango imechanganya Kambi Rasmi ya Upinzani. Hotuba yetu imeandaliwa na Halima Mdee ambapo nilipoipitia kwa kweli imejaa malalamiko badala ya uhalisia.
Kwa vile Waziri Kivuli wa Fedha, Halima Mdee yupo Kifungoni, Naibu wake, David Silinde ndiye atakayewasikisha Hotuba hiyo. Hata hivyo, hayupo tayari kuiwasilisha kwa vile haina hoja za maana.
Kwa hali hiyo, wabunge wa Upinzani wamekubaliana kususia mjadala wa Bajeti Kuu ya Serikali na watatumia hoja ya kufungiwa akina Halima Mdee na Esther Bulaya kama kisingizio cha kutoshiriki mjadala huo. Kuna uwezekano mkubwa Wabunge wa Upinzani wataingia Bungeni Jumatatu na kutoka nje baada ya kipindi cha maswali na majibu.