Kuna Chuo Chochote Kinatoa Mafunzo Namna Ya Kuongea Mbele Ya Kadamnasi?

Katavi

Platinum Member
Aug 31, 2009
41,983
12,700
Heshima wakuu...
Nauliza kama kuna chuo chochote hapa nchini kinachotoa mafunzo ya namna ya kuongea mbele ya kadamnasi. Hii inatokana na namna watu mbalimbali tulivyo waoga kuongea mbele ya watu hasa katika sherehe au msibani.
Kuna kisa kilinitokea msibani baada ya kumaliza kutoa heshima kwa mwili wa marehemu na kuwa tayari kusafirishwa, niliombwa nitoe neno la shukrani. Lakini niliweza kukwepa na kumtupia jamaa mmoja aliyekuwa jirani yangu, lakini kumbe yeye ndiye alikuwa mbovu kuliko mimi. Alianza kwa kusema "MSIBA OYEEE"......shukrani kwa mzee mmoja aliyeokoa jahazi.
Naombeni elimu ya namna ya kujiamini nisije kupatwa na aibu kama hiyo........
 
My goodnesss.........is this Katavi or am lost somewhere

Mkuu for the first time naona umeweza kuandika post ina zaidi ya mistari miwili......

Nice beginning na nadhani utakuwa umeanza kozi ya kuongea na kuandika mbele ya kadamnasi
 
My goodnesss.........is this Katavi or am lost somewhere

Mkuu for the first time naona umeweza kuandika post ina zaidi ya mistari miwili......

Nice beginning na nadhani utakuwa umeanza kozi ya kuongea na kuandika mbele ya kadamnasi
Ahahahahaaaah!!! Mkuu imenichukua zaidi ya masaa mawili kuandika.....
Naomba msaada wapi kuna chuo au namna gani nitapata uzoefu....
 
Ahahahahaaaah!!! Mkuu imenichukua zaidi ya masaa mawili kuandika.....
Naomba msaada wapi kuna chuo au namna gani nitapata uzoefu....

Hahaaaaaaa, kaka yaani hivi vimistari kadhaa 2 hours!!!!!!!!!!?????........

dah, labda kusomea zile kozi za public relation nahisi kwa nature ya kazi yenyewe huenda wanafundishwa hii kitu......au sijui ndo ile ya journalism?
 
Viongozi wa dini wanaweza kusaidia?? Vipi kuhusu mambo ya sherehe??

ni wazoefu wa kuzungumza mbele za watu!! nina hakika watakushirikisha uzoefu na technics zao ambazo zitakusaidia kwa kiwango kikubwa.
 
Heshima wakuu...
Nauliza kama kuna chuo chochote hapa nchini kinachotoa mafunzo ya namna ya kuongea mbele ya kadamnasi. Hii inatokana na namna watu mbalimbali tulivyo waoga kuongea mbele ya watu hasa katika sherehe au msibani.
Kuna kisa kilinitokea msibani baada ya kumaliza kutoa heshima kwa mwili wa marehemu na kuwa tayari kusafirishwa, niliombwa nitoe neno la shukrani. Lakini niliweza kukwepa na kumtupia jamaa mmoja aliyekuwa jirani yangu, lakini kumbe yeye ndiye alikuwa mbovu kuliko mimi. Alianza kwa kusema "MSIBA OYEEE"......shukrani kwa mzee mmoja aliyeokoa jahazi.
Naombeni elimu ya namna ya kujiamini nisije kupatwa na aibu kama hiyo........

Wee Katavi umenifanya watu wanishangaee baada ya kuangusha kicheko-"MSIBA OYEEE"
 
Heshima wakuu...
Nauliza kama kuna chuo chochote hapa nchini kinachotoa mafunzo ya namna ya kuongea mbele ya kadamnasi. Hii inatokana na namna watu mbalimbali tulivyo waoga kuongea mbele ya watu hasa katika sherehe au msibani.
Kuna kisa kilinitokea msibani baada ya kumaliza kutoa heshima kwa mwili wa marehemu na kuwa tayari kusafirishwa, niliombwa nitoe neno la shukrani. Lakini niliweza kukwepa na kumtupia jamaa mmoja aliyekuwa jirani yangu, lakini kumbe yeye ndiye alikuwa mbovu kuliko mimi. Alianza kwa kusema "MSIBA OYEEE"......shukrani kwa mzee mmoja aliyeokoa jahazi.
Naombeni elimu ya namna ya kujiamini nisije kupatwa na aibu kama hiyo........

Hahahaha hii kali Msiba Oyee
Kama una aibu unakamata kilaji kiduchu usizidishe
Na ukinywa mbege utakuwa unaongea kilugha, ukimata bia utakuwa unaongea kiswahili ukikamata wine unawachanganya wahudhuriaji maana utakuwa unafanya code mixing mara kijerumani mara kiingereza mara kicongo
 
Hahahaha hii kali Msiba Oyee
Kama una aibu unakamata kilaji kiduchu usizidishe
Na ukinywa mbege utakuwa unaongea kilugha, ukimata bia utakuwa unaongea kiswahili ukikamata wine unawachanganya wahudhuriaji maana utakuwa unafanya code mixing mara kijerumani mara kiingereza mara kicongo

Na kama sio mlevi, si ndio nitaharibu zaidi??
 
Kasomehe ualimu au fanya kazi ya ukonda na kupiga debe stendi utapata experience mkuu.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom