Kuna baadhi ya kazi hapa duniani, Mbinguni utapasikia tu

Jan 14, 2019
64
61
Siasa
Wanadanganya ili wapate kura wakati wanajua haya mambo hayawezekani kuna watu wapo madarakani wamesahau walichowaambia wananchi+ wanasiasa wa Jamaika lakini sio wa hapa kwetu kabisa sijawahi ona wanasema uongo akiamama

Uanasheria
Mtu anaua/amefanya dhambi kubwa halafu unamtetea ili ulipwe + Wanasheria wa Marekani lakini wa hapa kwetu Kweli kabisa wanatetea vizuri wanyonge

Polisi
Wakikuona kituoni wanaona dili limekuja haijalishi umepeleka mashitaka au umeshitakiwa lakini ni Polisi wa Ulaya wa hapa kwetu wapo vizuri sana wanasimama pamoja wananchi vizuri sana ila Polisi ya Ng`ambo Big no


Kuna kazi duniani ukifanye lazima uenda Mbinguni
i.Udaktari
ii.Uchungaji/Ushekhe
iii.Ualimu


Zipo baadhi ya kazi ni PROBABILITY unaweza kwenda Mbinguni au JEHANAMU
i.Wafanyabiashara
ii.Wakulima
iii.Madreva
iv.Jeshini nk

Mimi kama Mzazi ntamshauli Mwanangu awe Mchungaji tu!
 
Uuguzi/ Ukunga: unasaidia mama kujifungua kitoto kichanga, kinavuta pumzi yake ya kwanza unakiangalia, kinapanua mapafu yake kwa kuvuta hewa hii ya dunia iliyojaa uovu na wema na kisha kinalia ...unaiona furaha ya mama baada ya maumivu makali. Huwa nawaza hivi: kazi yangu imekamilika! haijalishi huyu mtoto atakuwa jambazi, padre, shekhe, nk
Japo Jiwe limegoma kujali maslahi yetu ila basi tu Mungu atatulipa
 
unawazungumziaje wale madaktari wanoshiriki kutoa mimba au wale wanaotamani wateja wao kimapenzi, nao wanaenda mbinguni?

vipi , kuhusu wale walimu ambao hawatimizi wajibu wao vizuri, nao wataenda mbinguni?

mbinguni ataingia askari, daktari, mwalimu, mwanasiasa, mwanasheria ila wataingia wenye moyo safi tu na wenye upendo wa kweli
 
Dhambi zote sawa...nafikiri hakuna mwanadamu mkamilifu..
Hatupaswi kuhukumu maana ata sisi huwenda mbingu tutaisikia tu

Au ata ao wanaseria huwezi kujua labda wanatubu kila baada ya tukio, na Mungu wetu ni wa huruma husamehe kadri tunavyotubu

Sent using Jamii Forums mobile app
Bora Mimi muuza bia nitaenda mbinguni na siibagi change za wateja.
 
unawazungumziaje wale madaktari wanoshiriki kutoa mimba au wale wanaotamani wateja wao kimapenzi, nao wanaenda mbinguni?

vipi , kuhusu wale walimu ambao hawatimizi wajibu wao vizuri, nao wataenda mbinguni?

mbinguni ataingia askari, daktari, mwalimu, mwanasiasa, mwanasheria ila wataingia wenye moyo safi tu na wenye upendo wa kweli
Kipimo cha haki kinalinganishwa na kipimo cha dhambi hatujui wamesaidia uhai wa watu wangapi na kuua watu wangapi??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom