Kuna ardhi zimevimbiwa maovu

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,530
Nimekaa na tafakuri ya kina nilipoona mabaki ya bar maarufu sana kinondoni iliyobomolewa jana au juzi, bar ya Mango garden
Nikajikuta nakumbuka na viwanja vingine vilivyokuwa na utata wa kutosha kabisa... Magomeni kwa Macheni, Chezi ntemba kinondoni small garden, Ulayaulaya,zote za magomeni,...... List ni ndefu sana ila hizi chache ziko kwenye spotlight na leo hii haziko tena...
Ni bar juu ya ardhi zilizoacha makovu mengi ya magonjwa kama ukimwi, mimba zilizomea na kuzalisha watoto wa mitaani, vyuo vya uchangu kwa mabinti waliopotea step, ushoga kamari wizi utapeli nknk
Miaka ile ya mwishoni mwa 90-2000 vingi nilivyotaja hapa vilikuwa viwanja vyangu.... Mango garden pana mchango mkubwa kwa kushamiri ushoga kinondoni... Vijana walishikishwa kutwa za chooni pale mango na wengine waliandika mpaka namba zao za simu... Haikuwa ajabu kuingia chooni na kusikia mtu anashughulikiwa ama haikuwa ajabu kufuatwa chooni na shoga akikuomba live umkune
Kwa macheni ile bar acha tu ife... Inasemekana huyo macheni mwenyewe alikuwa mteja, yani alikuwa ngangaripoa.. Ulawiti ulikuwa unafanyika wazi chooni na kwenye kona yoyote tulivu.... Kwa macheni watu walikuwa wanashughulikiana huku wamekaa wanakunywa na hakuna mtu alikuwa anashangaa... Kwa macheni ni bar ambayo haikufaa kwenda na mpenzi wako, asipoibwa yeye... Utaibwa wewe.... Mmekaa meza moja mnaangaliana kumbe nyuma yake unakonyezwa na yeye nyuma yako anatongozwa... Na mmoja wetu akiwa banditu ataenda kula ama kuliwa bila mwingine kujua... Vya fasta ndio ilikuwa biashara kwenye gesti zilizozunguka kwa macheni
Gesti hizo haikuwa ajabu kukuta watu wamepanga foleni ya kuingia chumbani na watu wao.. Kule chumba cha kulala kilipatikana kuanzia saa tisa usiku...
Haya ndio yalikuwa maisha ya usiku kwenye hizi bar ambazo zilibebesha ardhi ya mola maovu mengi
Sasa zimebaki story tu za kusimuliwa na kusimulia
 
Back
Top Bottom