Kuna amri 10 za Mungu, lakini kuna amri 5 za Mbuyu "Junior" Twite.

demigod

JF-Expert Member
Jan 2, 2015
8,246
15,084
Salaam.

Leo nimeona iwe vyema kuwaletea maajabu ya huyu Kijana, anaitwa Mbuyu "Junior" Twite. Kuna facts za Ajabu sana kuhusu huyu kijana tangu aliposaidiwa na Agent wake "Aden Rage" kutua pale mitaa ya Jangwani.

Nina kila sababu kusema kuwa huyu Kijana hajutii hata mara moja kutua kwa wanajangwani. Maana kuna Maajabu kadhaa aliyo sababisha tangu atue pale Jangwani.

Maajabu 5:
Tangu Mbuyu "Junior" Twite atue Jangwani mnamo 31/08/2012.

1. Simba haijawahi beba Ubingwa wa LigiKuu Tanzania. Kwa lugha nyingine Mbuyu Twite hajawahi kuiona Klabu hiyo yenye makazi yake pale Msimbazi (Matopeni) wakibebwa Ubingwa.

Ila siwezi kubisha kuwa njia pekee ambayo huenda alitumia ni kuingia Google na kupakua (download) picha za simba akibeba ubingwa misimu ya nyuma kabla ya 2012 kwa lengo la kuzitazama tu.

2. Tangu atue Jangwani amebeba Ubingwa wa VPL mara nyingi zaidi kuliko mchezaji yeyote yule wa simba ndani ya Miaka 16 iliyopita.

VPL:- 2012/13 - 2014/15 - 2015/16.
Azam Sports Federation Cup - 2015.

3. Tangu Mbuyu Twite asaini Jangwani Klabu ya Simba haijawahi kushiriki michuano yeyote mikubwa nje ya Tanzania.... Namzungumzia (CAF)

4. Tangu asaini Jangwani Klabu ya Simba imebadilisha walimu (Makocha) wasio pungua 5.

5. Tangu ajiunge Jangwani amecheza Dar Derby 9. Ambapo amepoteza mechi moja (1) tu dhidi ya Simba....kwa bao moja bila.

Shukrani sana Mbuyu Twite.

Leo tunakuaga rasmi pale uwanja wa Uhuru kwa mechi ya kirafiki dhidi ya JKU Zanzibar.

Ama kweli Uwepo wako Jangwani ulikuwa mwiba mkali mno ndani ya maisha ya Mashabiki wa Msimbazi. Tutakukumbuka sana. Haswa kwa haya Maumivu uliyosababisha kwa Warani zetu.

....
 
Utaruka ruka sana lakini nasikia jamaa kagoma kulipa pesa za Kessy itabidi muanze kupitisha kapu kuchanga. Huu ni mwanzo tu mmeukalia hauchomoki kirahisi pamoja na jitihada za kujaribu kupeleka attention kwingine.
 
Utaruka ruka sana lakini nasikia jamaa kagoma kulipa pesa za Kessy itabidi muanze kupitisha kapu kuchanga. Huu ni mwanzo tu mmeukalia hauchomoki kirahisi pamoja na jitihada za kujaribu kupeleka attention kwingine.

Pale Jangwani kuna kitu kinaitwa 'Mfuko wa Klabu"..... yaani ni mfuko wa fedha ambazo zinatokana na mapato madogo madogo ya Klabu..

Hazikosekani vi_MIL50.

.
.
.
 
Utaruka ruka sana lakini nasikia jamaa kagoma kulipa pesa za Kessy itabidi muanze kupitisha kapu kuchanga. Huu ni mwanzo tu mmeukalia hauchomoki kirahisi pamoja na jitihada za kujaribu kupeleka attention kwingine.


Pia pale TFF pana pesa zetu za Azam.... bado hatuja chukua...

Usiwe na wasiwasi kuhusu pesa. Jangwani ndio matajiri wa Jiji..... Manji anatoa za Kusajili tu. Ila za masuala madogo madogo kama haya..... Haitofikia hatua ya wanachama kuchanga pesa.....

Usiogope mtapata pesa zenu..
 


Pia pale TFF pana pesa zetu za Azam.... bado hatuja chukua...

Usiwe na wasiwasi kuhusu pesa. Jangwani ndio matajiri wa Jiji..... Manji anatoa za Kusajili tu. Ila za masuala madogo madogo kama haya..... Haitofikia hatua ya wanachama kuchanga pesa.....

Usiogope mtapata pesa zenu..
Wewe deiwaka unajua chochote kuhusu yanga?
 
Utaruka ruka sana lakini nasikia jamaa kagoma kulipa pesa za Kessy itabidi muanze kupitisha kapu kuchanga. Huu ni mwanzo tu mmeukalia hauchomoki kirahisi pamoja na jitihada za kujaribu kupeleka attention kwingine.
Mdosi kasusa?..
 
Mngekuwa na so called mfuko wa klabu msingedaiwa bilioni 11 na Manji. Alitishia kujiuzulu mijitu mizima ikampigia magoti. Kuna siri kubwa sana kushuhudia watu wazima wanampigia magoti mtu asisepe. Hao waliopiga magoti wanajua akisepa tu mnarudia enzi za Rashid Matunda kuchanga maharage na mchele ili wachezaji wale. Una pana pua ohh tuna pesa zetu Azam mmekumbuka matapishi na bado.
 


Pia pale TFF pana pesa zetu za Azam.... bado hatuja chukua...

Usiwe na wasiwasi kuhusu pesa. Jangwani ndio matajiri wa Jiji..... Manji anatoa za Kusajili tu. Ila za masuala madogo madogo kama haya..... Haitofikia hatua ya wanachama kuchanga pesa.....

Usiogope mtapata pesa zenu..
Asee mbona mlipitisha mabakuli
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom