Kumuacha Idd Amin dada afe kifo cha asili tulifanya mfano mbaya sana kwa madikteta

Kwahiyo Uganda hawakutuchokoza kwa kuivamia Kagera?
Ukweli ni kwamba, toka Amini Achukue Nchi, Mwl alifadhili vikundi vya wakina Obote na vinginevyo vikawa vinaingia Uganda vinashambulia vikitokea maporini mpakani upande wa TZ Kagera.
Amini alijaribu kuongea hili na Mwalimu, alivoona mambo yanaendelea akachukua maamuzi japo likawa ndio anguko lake
 
Ukweli ni kwamba, toka Amini Achukue Nchi, Mwl alifadhili vikundi vya wakina Obote na vinginevyo vikawa vinaingia Uganda vinashambulia vikitokea maporini mpakani upande wa TZ Kagera.
Amini alijaribu kuongea hili na Mwalimu, alivoona mambo yanaendelea akachukua maamuzi japo likawa ndio anguko lake
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚kwa hiyo amin alitegwa akategeka๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†
 
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚kwa hiyo amin alitegwa akategeka๐Ÿ˜†๐Ÿ˜†
Kabisa, maana hata wakati tunampiga Amini tuliambatana na makundi kadhaa ya waasi, ambao ndio hao Mwalimu alikua Sponsor!
Huoni Kaguta anavomwelewa mzee.....Anamwita mwenye "HERI"
 
Idd amin aliepuka kifo kwa sekunde kadhaa tu
Najivunia mzee wangu alikwepo front line kumchapa huyo nduli

Magufuli yupo imara hakuna wa kuichokoza nchi yetu
Afadhali Mkuu nawe umeongea.Kimsingi,wazee wetu wengi walioenda vitani ukiwauliza kuhusu Idd Amin wanasema he was such an evil man.Pale Uganda walishuhudia mabaki ya uovu wa Amin, mengine waliambiwa na Waganda wenyewe.Na ndo maana JWTZ haikukutana na upinzani kutoka kwa raia, sana sana walipokewa kwa shangwe zote.

Lakini cha ajabu:kuna kizazi ndani ya Tanzania yetu (ambacho hakikwenda vitani na wala hakijui vita ni nini) kinaamini Idd anazushiwa.Na ukichunguza wengi wao wanatoa utetezi wakichagizwa na udini.Na sijui kwanini hawawaulizi wapiganaji kama Yusuph Himid kuhusiana na Amin?

Siku zote huwa nawasihi ndugu zangu wale, dini isiwafanye wasione maovu ya muumini mwenzao hata kama yapo.Mimi ni Mkristo, lakini Ukristo wangu siwezi kuutumia kukanusha ukweli kwamba Wakristo wenzangu,tena Wakatoliki wenzangu Jean-Bedel Bokassa, Benito Mussolini,Adolf Hitler walikuwa madikteta.Kwanini dikteta Mwislamu akijadiliwa Waislamu waje juu?
 
Duh..Aliyemfukuza ni Nyerere ila jamaa alikuwa na marafiki wenye nguvu tu na walikuwa wakiona yupo sawa Gadafi anayetajwa sana ni mzuri alimtumia shehena ya silaha Saudia walimpa hifadhi

Nyerere naye alikuwa akiingilia mataifa ya watu na kupindua serikali zao huku akizituhumu zimemchokoza kama Marekani inavyofanya,
Alipindua Serikali ya Uganda ikiwa huru, Serikali ya Zanzibar ikiwa huru, na akaunga mkono waasi huko Nigeria waliotaka kujitenga
Wafuasi wake watasema alikuwa anafanya kwa nia njema ila kwenye siasa kila mtu akifanya kitu anadai anafanya kwa nia njema
Nigeria-TZ diplomatic saga Ndio mwanzo wa viwanja vya biafra sio?
 
Habari wakuu,

Kitendo cha kumuacha idd amin dada akimbie na kumuacha mpaka afe kwa amani kilikuwa ni mfano mbaya sana kwa madikteta, sasa madikteta wanajua wanaweza kuichezea nchi yetu na wakakimbia bila kuchapwa, huu ulikuwa ni mfano mbaya sana, kosa kama hili tusilirudie tena
Asanteni
Point yako hasa nini mkuu funguka!
 
20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom