green rajab
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 11,304
- 35,850
Nikiwa sebleni kwa shemeji yangu na king'amuzi ameshakilipia huku na subiri dada apike ugali na nyama nile..halafu Askari vinalipwa pesa mbuzi tarehe kama hizi wanapumulia gesiHao mapolisi wanaotesa watanzania wenzetu hatutawapumzisha kamwe unyama mlioufanya kwa watu wasio na hatia mtajibu.
Komando Lingwenya alisema aliteswa mateso makali akiwa uchi wa mnyama huku wakimrekodi video kwa simu.
Mdude alisema hivyo hivyo eti ata wanawake wanavuliwa nguo na hao mapolisi wanateswa na kurekodiwa juu,, Mdude anasema Kuna mdada mmoja alikuwa chumba Cha pili kutoka alichokuwa mdude,, unaambiwa alivyokuwa analia kwa kuteswa hajui walikuwa wanamtesa na nini.
Halafu unavuliwa nguo Kama ni mwanaume anakuja askari wa kike anaupiga uume wako halafu anakuambia simamisha, what a humiliation .
Wanawake wanaoteswa vituoni wanavuliwa nguo na kuteswa uchi( sio maneno yangu ni ushuuda wa Mdude, Lingwenya na Adomo)
Mlaaniwe nyie Askari mnaodhalilisha watanzania wenzetu,, lakini pia mbalikiwe Askari mnaotenda haki.