mpayukaji
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 940
- 349
Kila mwenye uchungu na Tanzania analaani kitendo cha kijinga na kihuni alichofanyiwa dk Steven Ulimboka mwenyekiti wa Jumuia ya Madaktari. Hivi watanzania wataendelea kutumiwa na kila atakaye kulinda kitumbua chake hata kwa kuwatoa roho? Je kumteka na hata kumuua Ulimboka ndilo jibu wanalotaka madaktari? Je hapa haki ya kila mtanzania kufaidi ulinzi iko wapi iwapo watu tena wanaolipwa pesa ya umma wanaweza kuingilia haki za wengine na hata kutishia maisha yao? Tusaidiane na kujifunza toka kwa wenzetu. Je hii ingetokea Misri au Tunisia hali ingekuwaje?