Kumsusa Kikwete, CHADEMA wamevuna mahindi au Mabua?

Faiza sio mchezo, unamtoa kamasi hadi Slaa. Taratibu bibie, usije kumpandisha presha mzee wa watu.
 
Mkuu, uwe unasoma makala kwanza basi kabla hujaanza kukurupuka. Anyway, uchaguzi uliopita wala kura sikupiga kwa sababu ambayo ipo nje ya uwezo wangu na hata kama ningelipiga wengi hapa wanajua ningelimchagua nani.

Mkuu umemsoma vibaya Angel Msofe..swali hili lilikuwa linamwendea Faiza Foxy.....wewe umeleta habari ambayo baada ya kuona mwanzishaji faiza kidogo tuichunieeee kwa hiyo aliyeanzisha suala la mahindi na mabuha ni FF na mimi namjibu kuwa tulipomchagua kikwete tulivuna Mabuha................
 
Hahahaaaa, FF. Ungelikuwa hujaolewa (kama ni Mwanamke) basi ningelifunga pingu za MSIMU na wewe.

Au unataka na wewe tuanze kukutafutia makosa yako ya kiuandishi? Mbona ni mengi tu tunayamezea?

Thread yako ya mwisho, umeianza kwa vijembe kama kawaida yako. Ila nakubaliana na wewe ulipomalizia kuwa MSHINDI AWE NI MTANZANIA. Na hilo ndiyo nilikuandikia kwenye thread kuhusu Vyama vya siasa na majeshi yake ila wewe ukaja na habari za vita za kidini.

Kumbe ukibanwa vizuri kama mjusi mlangoni, huwa unakubali ukweli. Kwa mara ya kwanza naona umetowa HONGERA kwa Chadema ingawa ni kwa shingo upande. Kucheka kwa Slaa kusikupe matumaini sana, ni kicheko huku uso umekunjamana. Unajua hilo na mie najua hilo na wote Kikwete na Slaa wanalijua hilo.

Usisahau, mie tangu mwanzo nimeshasema kuwa "Najua unajua na wewe umeshajua kuwa mie najua kuwa wewe unajua".
Ila kwa makusudi kabisa, tangu mwanzo upo hapa unapotosha umma kama Dr. Slaa alivyosema.
Soma vizuri, sikuanzisha mimi hiyo mada.

mabuha = mabua
 
Ta Muganyizi,

Basi nimuombe kwanza Angel Msofe msamaha na kwa niaba yangu na wale wote waliomuelewa yeye vibaya. Nilimuelewa kwamba hiyo alikuwa kaniandikia mimi. Again, Angel Msofe, samahani na tupo pamoja tuendelee kuelewashana kama TAIFA na si Chama.
Mkuu umemsoma vibaya Angel Msofe..swali hili lilikuwa linamwendea Faiza Foxy.....wewe umeleta habari ambayo baada ya kuona mwanzishaji faiza kidogo tuichunieeee kwa hiyo aliyeanzisha suala la mahindi na mabuha ni FF na mimi namjibu kuwa tulipomchagua kikwete tulivuna Mabuha................
 
By FaizaFoxy
Kususa inkwisha? mlipoteza muda mrefu sana kwa siasa za kususa susa, naona mmejifunza kuwa kususa inatumika kuwa "disadvantage" kwenu.
slaa-lissu-kikwete.jpg


Nimekuwa najiuliza, hivi ukivamiwa na nchi fulani ya jirani au hata ya mbali, je kuna haja ya kusimama na kuitetea nchi yako? Hili swali ndiyo limenipa msukumo wa kuandika haya machache hapa.

German ikiongozwa na Adolf Hitler, walianza mchakato wa kuzishambulia nchi za jirani na lengo hasa likiwa kujipanua kiuchumi. Walijizatiti kivita na walipokuwa tayari, walianza mchakamchaka wa kuzichukua nchi moja baada ya nyingine. Nchi nyingi kama Waholanzi, Wapolish, Wafaransa, Warusi waliwapinga na hiyo ikapelekea nchi hizo kupigwa vibaya sana na kuharibiwa.
Mji kama Warsaw, waliuvunja zaidi ya asilimia 90. Russia walikuwa wakivunja kila kitu na kwa Moscow, Warusi waliamua na wao wenyewe kuuchoma mji wa Moscow na Wageruman walipokuwa wakifika, hawakuwa na maji, chakula wala sehemu ya kujisetiri.

Vita kali sana ilipiganwa huko Volgograd (zamani ikiitwa Stalingrad - Battle of Stalingrad - Wikipedia, the free encyclopedia ) na vita ilipoisha, kulikuwa na uharibifu mkubwa sana. Katika matukio ya kusikitisha, ni kikosi cha Warusi, askari 10,000 ambao walipelekwa kushambulia Wageruman na wote wakafa. Mengine mtu unaweza kusoma mwenyewe kuhusu vita na hilo si muhimu hapa.

Upande mwingine, kuna nchi ambazo wao walimkaribisha Hitler kwa mikono miwili ingawa kwa shigo upande na kumpa funguo na mji mkuu wao na hiyo ilipelekea nchi hizo zisipigwe hata risasi moja wakati wa vita ya pili ya dunia. Moja ya nchi hizo ni Czech na ukiona mji mkuu wao uitwao PRAGUE, utagundua tofauti yake na nchi nyingi. Pale kuna majengo ambayo mengine hata yana zaidi ya miaka 1,000. Old town ya Prague kwa ujumla ni kipande kizuri cha historia.

Hapa swali langu ndiyo linaanza, je kulikuwa na haja ya nchi kumpinga Hitler? Je walifanikiwa nini zaidi ya kusababisha nchi zao kuharibiwa tu na silaha kali za Hitler? Je hao waliokubali nchi zao kuchukuliwa kirahisi, leo wamefaidika vipi?

Nafikiri hapa jibu litategemea mtu umeamua kukalia kiti katika upande upi. Wengine wanaona kuwa nchi zilizomgomea Hitler, walao baada ya vita ya pili ya dunia, walianza kuipanga miji yao upya hasa ukichukulia kuwa, miaka ya zamani, mitaa ilikuwa myembamba sana na vitu kama mabomba ya maji, umeme, simu, gas nk ilikuwa kwenye mpangilio wa ovyo kutokana na mitaa kuwa myembamba sana na hatari kwa afya ya binadamu.
Kwa wale waliokataa vita, wamebaki na historia yao na huku dunia nzima ikienda kuangalia jinsi zamani nchi za Ulaya zamani zilivyokuwa.

Hata kwa Tanzania, kuna makabila yaliwakubali na kuwapokea Wakoloni bila upingamizi. Wanyamwezi, Wahehe, Wangoni, nk waliamua kula nao sahani moja na kufanya maisha ya jamaa kuwa magumu walau kwa siku za mwanzo. Hapa napo unarudi kwenye lilelile swali, je kulikuwa na haja ya kuwagomea na matokeo yake yakawa kifo cha Isike, Mkwawa, Kinjeketile Ngwale na wananchi wengi sana ambao kulikuwa hakuna haja/kulikuwa na haja?

Tukirudi kwenye kesi yetu hapa ambayo imeumiza sana watu kichwa, Chadema kulikuwa na haja ya kumsusia (PROTEST) Kikwete pale Bungeni? Kulikuwa na haja ya Dr. Slaa kutokufika sehemu ya kuapishwa Kikwete pale uwanjani?

Kwangu mie, miaka ya zamani ningelijibu kuwa ilikuwa ni ushamba wa hali ya juu. Utamsusiaje mtu ambaye kesho yake unaenda kwake kumuona? Hiii hali iliendelea kuwepo kichwani kwangu hadi wakati wa vita kati ya Iraq na Iran (Israel vs Palestine) ambapo kila wakati nilikuwa nashangaa jambo moja kuwa kila wakisema wiki lijalo, watakaa mezani kujadili kusimamisha vita, basi vita ilikuwa inazidi kuwa kali sana. Zinapigwa utafikiri wamesema mwisho wa dunia unakaribia.
Nilimuuliza kaka yangu nini kinasababisha hii kitu na yeye akanijibu kwa kiingereza "Bargaining power at the mediation table."

Sina uhakika kwa kiasi gani, Nguvu ya CHADEMA na Dr. Slaa kwa CCM na hata kwa IKULU kwa sasa imekuwa kiasi gani au kupungua kwa kitendo chao cha kumsusia Kikwete na tume yake ya Uchaguzi. Je kama wasingelifanya hivyo, CCM ambayo hata kwenye kampeni zao hawakuwa na ajenda ya katiba mpya, wangelianzisha mchakato huu?

Labda kuna vijimaswali kadhaa inabidi kujiuza na haswa watu kama Lady FF (ingawa nafikiri atakuwa anafahamu hata zaidi yetu wengi humu ndani ya JF) kuwa, msuso wa CHADEMA, umeipa Bargaining Power kiasi gani hapa Tanzania against CCM/Ikulu/Serikali ya TZ?

MAONI YANGU: Kuna dalili kubwa kuwa, kususa kwa CHADEMA kumeleta mchakato wa katiba mpya. Sidhani kama CCM wangelianzisha kitu kama hiki bila ya kusukumwa kutoka nje kama Newton's law of motion inavyosema "a body will remain at rest or will continue to move at a constant velocity, unless an external force is applied. "
Ni mtu ambaye hafikiri sana na hajui au anajua ila anajifanya hajui (FF) ndiye atakuja na maelezo kuwa CCM wenyewe wameamua tu kubadilisha katiba na Rais mwenye kaamua tu kwa HURUMA yake kuonana na Chadema.

AGAIN, remember "a body will remain at rest or will continue to move at a constant velocity, unless an external force is applied. " Ukiona VINAELEA, VIMEUNDWA.

Hapo kwenye red umechapia, Hitler hakuwahifika Moscow, aliyefanyiwa hivyo anaitwa Napoleon
 
Hizo zote pumba, huko ireland unakoongea ni vita vya kidini, nani asiyejuwa? hata sijui unaongea maajabu yepi?

Hayo unayosema ingekuwa Serikali imenyanyuwa bendera nyeupe na kusema haya jamani wacheni kususa na maandamano mje tuongee, hapo ningekuelewa. Lakini bendera nyeupe mmyenyanyuwa nyinyi na mliotaka kuonana na Raisa ambae mlikuwa hamumtambui ni nyinyi na si mwingine. Sasa ujanja uko wapi? Na Kikwete alisemaje siku mliomsusia bungeni? usiniambie hujui.

Tulikuwa tunawaambia hapa, wacheni hizo, maana ya siasa sio hiyo. Hamsikii. Tazama sasa, umewashuka shuu, mnatafuta pakutokea hampapati. Mmerudi kulekule kwa yuleyule aliyewaambia "Mimi ndio Rais..."

Nakwambia seminar za kile chama cha siasa cha Kikristo cha Ujerumani CDU zimewasaidia kwa kiasi fulani, maana inaonesha mlikuwa hamjui maana ya siasa ni nini.

Naomba itazame ile picha ya viwanja vya Ikulu kabla ya kuingia kumuona Rais. Uniambie unakiona nini hapo.

Na mwenyekiti wako juu huko kwenye post kishaanza kusema kuwa katiba sio mwisho wa matatizo. Anajihami kabisaaa, yeye ndio aliilia, halafu yeye ndio akawa hataki mswaada upitishwe haraka, halafu yeye huyo kasusa halafu yeye huko kaomba kuonana na Rais.

Nimefurahi sana kwa hilo, kuwa mmemjuwa Rais ni nani, na makamu wake ni nani na Rais wa Zanzibar ni nani na makamu zake ni nani, na mmerudi.

Kile cheo ndio the most powerful katika Tanzania, kisikie hivihivi. Waone pale mbele yake, wote heshima na adabu, Hakuna kwii wala kwaaa, Unafanya maskhara wewe!

Dada yangu ulichoingiziwa/kupewa na huyu mzee kilikuwa babu kubwa. Huambiwa wala husikiiii........mipasho tu kwenda mbele......hapo ulipo hujui tuyaonayo kijijini kwetu huku. Wewe kula bata tu kwa raha zako lakini sisi tutawapgania wanyonge.
 
Si mlikuwepo mbona hamkujumlisha nyinyi matokeo na kutangazia yaliyo sahihi? ina maana hata hesabu za kujumlisha kura zinawashinda? Unanshangaza!

Usitake kuchakachuwa, ikiwa bungeni tu mnasusa ingekuwa mmeibiwa si ndio mnge zira kabisa.
Bibie,
Ubaya ni system iliyopo. Tuliambiwa tunaweza kutangaza matokeo ya ubunge na udiwani lakini tusiseme chochote kuhusu matokeo ya urais. Hiyo ni domain ya NEC peke yake. Hapo ndipo tulipoliwa. Kama tungeweza kutangaza matokeo yote moja kwa moja kutoka kituoni na waandishi habari kuruhusiwa kutangaza (unofficial results) kama wanavyofanya wengine katika nchi za kidemokrasia, Kikwete asingepata ile 60% aliyokabidhiwa na NEC. The system is sick.
 
Basi mmekatazwa kutangaza hata ushahidi wa kupeleka mahakamani umewashinda kuweka? hizo ni alinacha na habari za kusadikika, kwenye wengine haziingii akilini.
Hata kama tungetangaza mngetuita wachochezi. We know the likes of you.
Waambie NEC basi watangaze matokeo yote. Mbona mpaka sasa wameshindwa hata kuyatundika kwenye website yao? Halafu kwenda mahakamani ili iweje? Hujui kuwa sheria ya uchaguzi Tz inasema NEC wakishatangaza mshindi hakuna cha kwenda mahakamani?
Unadhani sisi majuha?
 
Najua kuwa hawakufika Moscow mjini ila walikaribia sana na kama si Snow kali iliyoanza kunyesha mwaka huo, who knows....

As early as Jul 1941, the Russians knew the Germans were going to breach their defenses and threaten Moscow. On 3 Jul, Lenin's body was moved from Moscow to Tumen to prevent German capture or destruction. Little over two weeks later, on 22 Jul, 127 German bombers raided Moscow, even lightly damaging the Kremlin. As a response, Moscow residents were ordered to build mock houses on Kremlin's grounds and paint the distinct roof of the building in order to blend it in with the rest of the city. Streets were also barricaded in preparation of a German attack. Moscow was proud, however, aided by Joseph Stalin's propaganda machine. One such example was the 7 Nov parade in celebration of the anniversary of the October Revolution, where Russian soldiers marched straight through Red Square toward the battlefields to the west.
After a series of attacks and counterattacks from both sides, the German troops were beginning to show signs of fatigue. Replacements came slowly partly due to the unplanned action in the Balkans and Crete, while the brutal Russian winter loomed dangerously near. The Russians, on the other hand, saw relatively fresh reinforcements from the recently arrived Georgi Zhukov and his troops from the Far East; the inability of the Axis powers to negotiate for a joint-attack on Russian had a significant impact on the German ability to quickly bring down Russia, but Adolf Hitler was too egotistical to see.
After a few days of preparations in Moscow's suburbs, on 2 Oct 1941, Fedor von Bock led German troops to assault directly against Moscow. German advances were slower than they had hoped with a rainy fall season and later a cold early winter. As German vehicles become immobilized, the German army continued to advance, however the cold weather was affecting the morale and fighting ability of the troops to a high degree. On 15 Nov, another push for Moscow was launched, and within two weeks the Germans reached the 27km marker to Moscow, with some soldiers claiming the sighting of the towers of Kremlin.
The weather also significantly harmed the German ability to supply the Moscow contingent by rail, despite Minister Dorpmüller and the German Reich Railways dramatically expanding its operations during the campaign. The water tanks of the locomotives regularly froze under sub-zero conditions, pushing the number of broken-down locomotives at any given time to the hundreds. Additionally, the Russian railways were of a different gauge, forcing the German engineers to re-bed all the railways before the German locomotives could use them. In Dec 1941, with the transport situation so desperate that a special motor transport organization was formed to alleviate some of the pressure. Despite the superhuman results the Germans had achieved in the arena of logistics, it was just not enough. The German frontlines troops, including the air force, required the equivalent of 120 train loads of supplies daily for normal operations (ie. not counting supplies needed to mount major operations); only about 100 train loads worth of supplies were delivered on a regular day. To make matters even worse, Russian partisans regularly sabotaged railway tracks to slow things further.

Battle of Moscow | World War II Database
Hapo kwenye red umechapia, Hitler hakuwahifika Moscow, aliyefanyiwa hivyo anaitwa Napoleon
 
Kijijini kwenu? Si uliandika hapa kuwa unakaa karibu na makao makuu ya CCM Lumumba?

Unafikiri tunasahau unayoandika? Vipi ile Laptop yako ulisema unanunua, bado inafanya kazi? Au ndiyo hii unatumia kusiliba watu hapa JF? Heheeee, kasheshe kwelikweli. Mara kijijini mara mtaa wa Lumumba, lohh.....
Tatizo la kijijini kwenu ni wavivu, sisi kijijini kwetu raha mustarehe, mtandao 24/7, mboga mboga mihogo tunaishusha kila siku sokoni, maziwa fresh, kuku wa kienyeji, umeme wa samadi, mlikuwa wapi nyinyi? nyie huko kijijini kwenu piganeni tu wenzenu kule mjini akina Slaa wameamuwa kumkubali Rais na kumuomba kukutana nae na wemetoka Ikulu wanacheka kwa furaha, ushahidi ni picha. Na Slaa kasemaa hiyo sio "isolated" case. Kalagabaho.


Ndiyo matatizo ya kubisha tu hadi unasahau kuwa unabisha nini. Kuna siku Dr. Slaa akikuita Bibie FF, utabisha kwa sababu tu jina hilo kakuita Dr. Slaa.

Haya sasa, hata hujui katiba ya Tanzania inayosema "NEC ikishamtangaza mshindi, basi imetoka na huwezi kwenda mahakamani."
Basi mmekatazwa kutangaza hata ushahidi wa kupeleka mahakamani umewashinda kuweka? hizo ni alinacha na habari za kusadikika, kwenye wengine haziingii akilini.
 
Hiyo inaitwa "friendly fire" mnajichanganya mpaka mnaripuwana wenyewe kwa wenyewe. Kama hamjajuwa FF basi ndio mimi.

Nafuu kulipuana kwa namna hiii kuliko JK alivyoikana dowans na video tukaona kisha Lowassa akasema kuwa alimpigia simu pishtoba wako akamwambia asiufute mkataba. At least confusion ni kwenye Interpretation na sio denial ya jamaa zako. Kama hatujakujua...tukujue nini...you are merely woman like my wife.....or any woman else....unless otherwise you are not a normal woman as other women i know. So i know you by your ascribed status....sasa kama una achieved status ambazo unazo zianike tuone exeptionality yako.
 
Mwenye "parochial" mind ni mimi au aliyesomea kanuni za kanisa?

Hilo la "isolated case" rudia posts na uone ni nani aliyelisema mwanzo, mimi nimelirudia tu. Usije ukakuta ni Katibu Mkuu wako ndiye aliyelisema hilo, utashushuka.

Ikiwa mtu aliyesusa Rais, aliyepinga kuwa si Rais, aliyeamrisha maandamano, aliyekuwa hajaeda kikao cha mwanzo, na sasa kasalim amri na kaenda na tumemuona, na anapotoka huko anasema "tutawaokoa", "katiba sio mwisho wa matatizo", kuwa hii sio "isolated case", anaeongea hayo unafikiri kaenda kwa kupenda kwake? nnakuhakikishia ni matakwa ya Mwenyekiti wake, aliyekwenda Ikulu mara ya kwanza na wenzake, mara ya pili peke yake (imeripotiwa humu) mara ya tatu kamlazimisha katibu Mkuu aende akitaka asitake. hakuna cha kupotosha hapo ni "common sense" ambayo kwako amma haipo amma ni finyu ndio iliyotumika.

Hilo swali lako la mwisho hiyo ndio reaction za action kama mleta mada alipoielezea theory moja maarufu, au bado hukubali kuwa kila action ina reaction? Unataka kuvamia kituo cha polisi, unaambiwa tawanyika wewe unakaidi, ulitegemea reaction ipi hapo? upigwe na chelewa?

Kama Urais ni taasisi basi Kikwete ndio Rais wa hiyo Taasisi.

Bado unaendelea kudhihirisha ulivyokuwa biased and prejudiced even where things are crystal clear. Go back to what Dr. Slaa has or has to say. Lakini kwa sababu uko mentally intoxicated by religious opium yet you can't think out of the box. May be we should not blame this to you but someone or to them. Lakini JF ni uwanja ambao wengi wanajifunza na mimi narudia go back to moderate school and learn about sematntics and stylistics. Hizi ni taaluma sio elimu ya kukukaririshwa whereby you end up blaming your own archtected problems to the ghosts or to others. Una tatizo la uelewa but you behave like an empty tin na unataka kuwafanya wengine kana mwamba mko kapu moja.

Na usipende kuchanganya mada hapa hata una chuki na mtu. Wewe kila unachoandika lazima useme kanisa. Kama una tatizo nalo basi anzisha thread inayohusu kanisa. Kama ni Dr.Slaa sema yanayomhusu Dr. basi sio kulisema kanisa na kupoteza lengo kile kinachojadiliwa. Ukitaka na wewe ujadiliwe kwa kuchanganya yanakuhusu wewe na imani yako basi sema tu.

Narudia usipotoshe yaliyosemwa na Dr. na wala usijifanye wewe ndiye kila kitu. Wapo wanaojua na wana maadili (ethics) kwenye kujadili, wana lugha ya staha ya kihuni peleka face book au mitaani ndio kuna watu wenye akili ya size za viatu
 
Jk aliuangalia upinzani kwa jicho moja akagundua haoni vizuri sasa anauangalia upinzani kwa macho mawili ndo maana hata leo ukimwambia tunahitaji serikali ya umoja wa kitaifa atakubali chap chap. wizi unahitaji roho ngumu sana na hasa unapokuja gundua uliyemwibia naye anajua ameibiwa na wewe.

Jk kile anachofahamu ambacho na Mungu wake anafahamu ni kuwa ccm iliiba kura ili kuingia ikulu. Lakini presha ya upinzani sasa inamnyima jeykey usingizi.

Wakati watawala wa libya na misri walipoona maandamano yanaanza wapambe wao walijipendekeza kuwaambia hao ni walevi achana nao lakini maandamano yale yamemfanya leo mubaraka asikilize kesi ya mauaji akiwa kwenye machela na gadafi kuiaga dunia hii. Jk kama binadamu hizo alama za nyakati amezishtukia:spy:
 
Kuna hadithi wakati nipo darasa la tatu inaandikwa "SIZITAKI MBICHI HIZI" Sungura aligumia ... nadhani ndio haya ya Slaa.... "Kisebusebu na kiroho papo! kutokana na picha zinavoonesha ni kwamba Slaa alikuwa akitamani sana kumshika angalau mkono Rais , angalau akaribishwe ikulu... na kama Rais alivosema " Mimi ndio Rais wenu ...mtarudi .... kweli wamerudi...hakika nimefurahi... na tuendeshe gurudumu la maendeleo mbele ! panapo wengi hapaharibiki kitu na hasa kukiwa na makundi yenye mtazamo tofauti basi mambo huamuliwa vema na vitu vikanyooshwa ! naamini mustakabali wa Katiba utaenda vema kwa kutmia zaidi ya kichwa kimoja ..Mungu ibariki Tanzania....
 
Hiyo inaitwa "friendly fire" mnajichanganya mpaka mnaripuwana wenyewe kwa wenyewe. Kama hamjajuwa FF basi ndio mimi.
FF, hapo utakuwa una invite wachangiaji wakujadili wewe personally, halafu wasipokujadili unavyotaka, then tatizo litaanzia hapo na mada kugeuka na matusi kuanza, nimejifunza kwenye hilo.

Ni bora ustick kwenye hoja, just ushauri.
 
Kususa ni njia mojawapo ya kujiexpress nadhani ata wewe uliepost kwa namna moja au nyingine unasusa anapokua na dissatsification ili kufikisha ujumbe....CDM hawakulupuki thas y ata jamaa wa magamba kasoma mchezo na kua mpole ili nchi itawalike.....so nampongeza JK na viongozi wa CDM kwani KJ akiacha ushambenga wa uCCM nadhani nchi itaenda sawa..jamani cku hizi kuna facial transp..... huyo jamaa nyuma ya JK ananitisha wakati wa picha wawe wanamtoa yani...........[/QUOTE]

Mkuu hapo kwenye RED, yan jamaa ndo kaharibu mandhar ya hiyo picha kabisa
 
Na hayo mlishinda? nani mwenye wabunge zaidi? nani mwenye madiwani zaidi? ukipata jibu utajuwa Rais wako ni nani kama walivyojuwa viongozi wa chama chako.
Kuwa na Wabunge/ Madiwani wengi siyo indication pekee ya kuwa Mkwer.re alishinda kwa 61%, unamaana kuwa tukichukua 5age ya wabunge/madiwani wa Magamba vesus wa upinzani tutapata idadi yao ni 61%???kama unaamini hivi basi we Mama utakuwa na very narow thinking capacity.
Najua ukweli unaujau kuwa kuwa Mkwer.e alipata 48% na Dr Slaa alipata 42 %, so uchaguzi ulikuwa urudiwe ndipo TISS/NEC wakachakachua...hii iko wazi hata Mkwer.e anajua
 
Yaani wewe FF, ni kama Tupac vile na wimbo wako wa "Me against the world......"

Kwani kuchakachua CCM tutawaweza? Hebu muone huyu MJOMBA wangu wa Igunga ambaye amechoka ila kila siku yupo hapo kuwasaidia nyie mnaojenga MAGOROFA ya biashara Dar na huku mkiishi kijijini kwenye upepo mwanana na Laptop nzito ukitesa ndani ya JF. Nina uhakika hata TV SIKIRINI yako itakuwa ni LG (Life's Good).


Na hayo mlishinda? nani mwenye wabunge zaidi? nani mwenye madiwani zaidi? ukipata jibu utajuwa Rais wako ni nani kama walivyojuwa viongozi wa chama chako.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom