Kumsusa Kikwete, CHADEMA wamevuna mahindi au Mabua?

Cdm kususa wamejifunza kutoka cuf na mtaona baadae kitakachofuata baada ya hawa viongozi kukanyaga ikulu, kwani maalimu.Seif si alianzaje

Maalim yeye alikuwa akifanya siasa kwa maslahi yake binafsi ila cdm wanafanya kwa maslahi ya Taifa kwahiyo wala hilo lisikutatize. Pia cdm wamekuwa ni watu wa kufikiri kabla ya kutenda na ndicho kinachowasaidia ktk siasa mpaka leo
 
Katika Uchaguzi Mkuu mwaka juzi CCM haikuwa na ilani ya Katiba mpya isipokuwa Chadema ulikuwa ni wimbo ulioshehehi Katiba mpya na hata walipomgomea Kikwete kule Dodoma madai yalikuwa ni kushinikiza upatikanajiwa Katiba mpya.

Mwambie huyo mkuu ili aache kulipuka bila kufikiri
 
Kususa ni njia mojawapo ya kujiexpress nadhani ata wewe uliepost kwa namna moja au nyingine unasusa anapokua na dissatsification ili kufikisha ujumbe....CDM hawakulupuki thas y ata jamaa wa magamba kasoma mchezo na kua mpole ili nchi itawalike.....so nampongeza JK na viongozi wa CDM kwani KJ akiacha ushambenga wa uCCM nadhani nchi itaenda sawa..jamani cku hizi kuna facial transp..... huyo jamaa nyuma ya JK ananitisha wakati wa picha wawe wanamtoa yani...........

Anakutisha sura ama nini mkuu?!
 
Slaa,

Nini kinachopotoshwa? nyinyi, wewe hususan ukiwa kiongozi ndiye uliyeongoza maandamano haramu yaliyopelekea watu kufa, wewe kama kiongozi umeshadidia kususa, kuanzia bungeni mpaka mitaani. Hapo ni kipi kinachopotoshwa?

Leo hii, wewe mwenyewe umeona kuwa kususa na maandamano sio tija, ni matatizo tu, ndiyo chama chakao kikaamuwa kumuomba Rais, wako na wetu sote, muonane nae. Kwa uungwana kabisa, Kikwete kakubali kuwaona, jee, mmepoteza nini?

Bado unataka kutuaminisha kuwa kumuona Rais na kujadili mambo muhimu (kama kweli yana umuhim) sio "isolated case"? Hapo ndipo nnapokuona kuwa unaongea kingine na kutenda kingine. Na hiyo inadhihirisha kuwa hata kwenda kwako kumuona kwenye hii unayosema sio "isolated case" si kwa matakwa yako, vipi? ilikuwa ni amri kutoka kwa Mwenyekiti.

Usemi wako wa mwisho hauashirii wema hata kidogo, kuliokoa hili taifa kutoka kwenye nini? Ikiwa Urais, ni demokrasia na kila mtu apendae anapiga kura. Sasa leo utuokoe kwenye nini? wengine tunaona siasa zako za maandamano na vurugu ni kututia kwenye janga na maafa, leo unaongea kutuokoa? Labda unachotaka ni kujiokoa mwenyewe (ambacho pia huwezi) kwa uchu wako wa madaraka lakini usituaminishe kuwa unataka "kuokoa taifa hili". Kikwete ndio "Chaguo la Mungu" na ndio chaguo letu tuliompigia kura, wewe rafiki inabidi ungoje 2015 (kama bado Mungu atakupa uhai, maana ni yeye tu muokoaji wetu sote) ujaribu tena bahati yako.

Kauli za mtu huashiria upeo wake, na hapa kwenye hizi kauli zako chache, na nyingi za uchochezi na siasa majitaka nilizokwisha zisikia, nasikitika sana kukuambia kuwa hufai kuwa kiongozi wa wote, labda baadhi tu ya Watanzania.

Utapoacha siasa za uchochezi na kuingia mitaani na kuanza kuingia Ikulu na kufanya kiukweli kuwa siasa sio "isolated case" kama maana ya neno siasa hapo ntakuona kuwa u mtu makini na unayeitakia mema nchi hii, kwa sasa na kwa kauli hizo tunataka tuone maandamano na kususa kuwa ni "isolated case" nakuona ni bado sana.

Wewe mama umeandika uharo gani hapa?

Hv kwako wewe maandamano ni siasa za chuki??

hv katiba ya nchi unaijua kweli??


Halafu bila aibu unadai maandano ni matatizo na majanga hivi kwa akili yako katiba inaweza kuruhusu kitu kitakacho iletea nchi matatizo na majanga??

Hv una akili zilizo hai japo kidogo?

Nani kakwambia Kikwete ni chaguo la Mungu?!hebu acha kumdhihaki Mungu.

Chaguo la Mungu analindwa kwa nguvu za majini ya Sheikh Yahya?!

Akili zako zilivyo mbovu unadhalilisha wanawake wa Tanzania. Shame on u.
 
I cant wait to see my President Dr. Slaa akitinga magogoni na kuanza mara moja kazi ya kuwakamata wahujumi uchumi, kufilisi mali zao na kuwaseka lupango, pamoja na kufumua mikataba yote ya kipumbavu walioingia Magamba kwenye madini na ardhi ili kulinda hadhi ya Mtanzania

if you can't what you can
 
Wewe mama umeandika uharo gani hapa?

Hv kwako wewe maandamano ni siasa za chuki??

hv katiba ya nchi unaijua kweli??


Halafu bila aibu unadai maandano ni matatizo na majanga hivi kwa akili yako katiba inaweza kuruhusu kitu kitakacho iletea nchi matatizo na majanga??

Hv una akili zilizo hai japo kidogo?

Nani kakwambia Kikwete ni chaguo la Mungu?!hebu acha kumdhihaki Mungu.

Chaguo la Mungu analindwa kwa nguvu za majini ya Sheikh Yahya?!

Akili zako zilivyo mbovu unadhalilisha wanawake wa Tanzania. Shame on u.

Naona kama mwenzako pia umeshindwa kujibu kwa hoja..

matusi ya nini? jibu hoja kwa hoja
 
Loser anaeogelea katika awamu ya pili? ana wabunge zaidi yako, hata nusu yake hujafikia, ana madiwani zaidi yako hata nusu yake hujafikia, alisema "Mie ndio Rais" mtarudi, kauli yake imetimia.

Imetimia kwa mazingira gani? Je hao madiwani na wabunge wao ni wangapi waliiba kura? Kwa ninavyojua tume ya uchaguzi ameiajiri Jk we utategemea nini hapo kama siyo kumpendelea boso wako?
 
Rais Kikwete hakuwaita chadema Ikulu . Ni chadema waliomba kumwona Rais ambae kwa msimamo wa cdm hawakutambua, walimususia wakati wakati wa kuzindua bunge. hoja ya chadema RAIS asiweke saini mswada wa sheria ya. Mchakato wa katiba iligonga mwamba. Mabadiliko wanayohangaikia yasibadili maudhui ya sheria yenyewe. Suala la katiba halijaanzwa na chadema,limekuwepo tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi. Kwa jumla chadema wamevuna pumba poleni sana.
 
kwa mtazamo kwa haraka haraka ningefikiria na kutoa hitimisho kama mleta mada alivyofanya. Ila nikifanya upembuzi zaidi naona hatua zilizofanywa na chadema zimezaa matunda mazuri hadi kufikia leo kukutana ikulu kwa kile kikwete kutekeleza sera na ilani ya chadema.

Ccm haikuwa na ilani ya katiba mpya, kwa vyo vyote hatua za chadema zimemsumbua kichwa kikwete hadi ndani ya siku 100 za mwanzo ambazo chadema walipanga kufanya mchakacho wa katiba mpya rais kikwete amelazimika kutekeleza.

Kwa asiyejua mbinu za kisiasa anaweza kutoa hitimisho la jibu lako, ila kwa wapembuzi watajiuliza iweje ccm itekeleze ilani ya uchaguzi wa chadema badala ya ilani yao ya ccm?

kwenye hii picha inaonekana watu wa ccm(serikali) hawanafuraha. Ukaangalia mzee tyson yuko kama vile amemwagiwa maji ya baridi(yaani amelowa). Nchimbi yeye anamshangaa kikwete anacheka na dr slaa na lusu. Hapa kuna jambo lisilowafurahisha

 
Rais Kikwete hakuwaita chadema Ikulu . Ni chadema waliomba kumwona Rais ambae kwa msimamo wa cdm hawakutambua, walimususia wakati wakati wa kuzindua bunge. hoja ya chadema RAIS asiweke saini mswada wa sheria ya. Mchakato wa katiba iligonga mwamba. Mabadiliko wanayohangaikia yasibadili maudhui ya sheria yenyewe. Suala la katiba halijaanzwa na chadema,limekuwepo tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi. Kwa jumla chadema wamevuna pumba poleni sana.

Ukweli mtupu mkuu
 
By FaizaFoxy
Kususa inkwisha? mlipoteza muda mrefu sana kwa siasa za kususa susa, naona mmejifunza kuwa kususa inatumika kuwa "disadvantage" kwenu.
slaa-lissu-kikwete.jpg


Tukirudi kwenye kesi yetu hapa ambayo imeumiza sana watu kichwa, Chadema kulikuwa na haja ya kumsusia (PROTEST) Kikwete pale Bungeni? Kulikuwa na haja ya Dr. Slaa kutokufika sehemu ya kuapishwa Kikwete pale uwanjani?

Kwangu mie, miaka ya zamani ningelijibu kuwa ilikuwa ni ushamba wa hali ya juu. Utamsusiaje mtu ambaye kesho yake unaenda kwake kumuona? Hiii hali iliendelea kuwepo kichwani kwangu hadi wakati wa vita kati ya Iraq na Iran (Israel vs Palestine) ambapo kila wakati nilikuwa nashangaa jambo moja kuwa kila wakisema wiki lijalo, watakaa mezani kujadili kusimamisha vita, basi vita ilikuwa inazidi kuwa kali sana. Zinapigwa utafikiri wamesema mwisho wa dunia unakaribia.
Nilimuuliza kaka yangu nini kinasababisha hii kitu na yeye akanijibu kwa kiingereza "Bargaining power at the mediation table."

Sina uhakika kwa kiasi gani, Nguvu ya CHADEMA na Dr. Slaa kwa CCM na hata kwa IKULU kwa sasa imekuwa kiasi gani au kupungua kwa kitendo chao cha kumsusia Kikwete na tume yake ya Uchaguzi. Je kama wasingelifanya hivyo, CCM ambayo hata kwenye kampeni zao hawakuwa na ajenda ya katiba mpya, wangelianzisha mchakato huu?

Labda kuna vijimaswali kadhaa inabidi kujiuza na haswa watu kama Lady FF (ingawa nafikiri atakuwa anafahamu hata zaidi yetu wengi humu ndani ya JF) kuwa, msuso wa CHADEMA, umeipa Bargaining Power kiasi gani hapa Tanzania against CCM/Ikulu/Serikali ya TZ?

MAONI YANGU: Kuna dalili kubwa kuwa, kususa kwa CHADEMA kumeleta mchakato wa katiba mpya. Sidhani kama CCM wangelianzisha kitu kama hiki bila ya kusukumwa kutoka nje kama Newton's law of motion inavyosema "a body will remain at rest or will continue to move at a constant velocity, unless an external force is applied. "
Ni mtu ambaye hafikiri sana na hajui au anajua ila anajifanya hajui (FF) ndiye atakuja na maelezo kuwa CCM wenyewe wameamua tu kubadilisha katiba na Rais mwenye kaamua tu kwa HURUMA yake kuonana na Chadema.

AGAIN, remember "a body will remain at rest or will continue to move at a constant velocity, unless an external force is applied. " Ukiona VINAELEA, VIMEUNDWA.

Sikonge thread yako imekaa kipanyapanya. Maana anauma na kupuliza, umejaribu kwa kiasi kikubwa kufikisha ujumbe kwa pre-emptive style. Mimi sijui nakubaliana na wewe ama napingana na wewe na sijui maoni yako yanajibu maoni ya FF au umemqoute FF kwenye picha tu kule juu na hapo chini ni yako. Ila kama ni yako ama ya FF nijibu tu thread kwa ujumla na hasa kwa kuwa kwenye maoni yako umetumia Newton's first law au Law of inertia kuelezea effect ya 'kususa kwa CHADEMA' , mimi nitumie Newton's law pia kuelezea jinsi amavyo huko kususa kwa CDM kulivyoleta impact katika siasa za Tanzania.

Kwa kutumia Newton's third law which states 'For every action, there is an equal and opposite reaction.' Action ya CDM ni dhahiri imeleta reaction ya watawala kujua kuwa Tanzania ya leo si ile ya Nyerere ya kubuluza watu and sooner or Later itakuwa haitawaliki kama wataendelea kulazimisha matakwa yao badala ya yale ya wananchi. Mchakato wa katiba ni moja ya theatre za kuonesha kuwa wanasikiliza. Ila kama watataka kuu-hijack na kuufanya wa CCM v CDM, the only loser will be Country. Kurudia mchakato huu tena baada ya miaka miwili ya kupatanishwa na kupata serikali ya kitaifa baada ya mali kuharibiwa na maisha kupotea kutokana na CCM kulazimisha matakwa yake haitakuwa positive investment kwa CCM na JK, maana wao ndiyo walioshikilia mayai(wahodhi rasilimali za taifa) pindi mawe yakianza kurushwa watapoteza wao hata kama warushaji watakuwa wametolewa uhai.
 
By FaizaFoxy
Kususa inkwisha? mlipoteza muda mrefu sana kwa siasa za kususa susa, naona mmejifunza kuwa kususa inatumika kuwa "disadvantage" kwenu.
slaa-lissu-kikwete.jpg


Nimekuwa najiuliza, hivi ukivamiwa na nchi fulani ya jirani au hata ya mbali, je kuna haja ya kusimama na kuitetea nchi yako? Hili swali ndiyo limenipa msukumo wa kuandika haya machache hapa.

German ikiongozwa na Adolf Hitler, walianza mchakato wa kuzishambulia nchi za jirani na lengo hasa likiwa kujipanua kiuchumi. Walijizatiti kivita na walipokuwa tayari, walianza mchakamchaka wa kuzichukua nchi moja baada ya nyingine. Nchi nyingi kama Waholanzi, Wapolish, Wafaransa, Warusi waliwapinga na hiyo ikapelekea nchi hizo kupigwa vibaya sana na kuharibiwa.
Mji kama Warsaw, waliuvunja zaidi ya asilimia 90. Russia walikuwa wakivunja kila kitu na kwa Moscow, Warusi waliamua na wao wenyewe kuuchoma mji wa Moscow na Wageruman walipokuwa wakifika, hawakuwa na maji, chakula wala sehemu ya kujisetiri.

Vita kali sana ilipiganwa huko Volgograd (zamani ikiitwa Stalingrad - Battle of Stalingrad - Wikipedia, the free encyclopedia ) na vita ilipoisha, kulikuwa na uharibifu mkubwa sana. Katika matukio ya kusikitisha, ni kikosi cha Warusi, askari 10,000 ambao walipelekwa kushambulia Wageruman na wote wakafa. Mengine mtu unaweza kusoma mwenyewe kuhusu vita na hilo si muhimu hapa.

Upande mwingine, kuna nchi ambazo wao walimkaribisha Hitler kwa mikono miwili ingawa kwa shigo upande na kumpa funguo na mji mkuu wao na hiyo ilipelekea nchi hizo zisipigwe hata risasi moja wakati wa vita ya pili ya dunia. Moja ya nchi hizo ni Czech na ukiona mji mkuu wao uitwao PRAGUE, utagundua tofauti yake na nchi nyingi. Pale kuna majengo ambayo mengine hata yana zaidi ya miaka 1,000. Old town ya Prague kwa ujumla ni kipande kizuri cha historia.

Hapa swali langu ndiyo linaanza, je kulikuwa na haja ya nchi kumpinga Hitler? Je walifanikiwa nini zaidi ya kusababisha nchi zao kuharibiwa tu na silaha kali za Hitler? Je hao waliokubali nchi zao kuchukuliwa kirahisi, leo wamefaidika vipi?

Nafikiri hapa jibu litategemea mtu umeamua kukalia kiti katika upande upi. Wengine wanaona kuwa nchi zilizomgomea Hitler, walao baada ya vita ya pili ya dunia, walianza kuipanga miji yao upya hasa ukichukulia kuwa, miaka ya zamani, mitaa ilikuwa myembamba sana na vitu kama mabomba ya maji, umeme, simu, gas nk ilikuwa kwenye mpangilio wa ovyo kutokana na mitaa kuwa myembamba sana na hatari kwa afya ya binadamu.
Kwa wale waliokataa vita, wamebaki na historia yao na huku dunia nzima ikienda kuangalia jinsi zamani nchi za Ulaya zamani zilivyokuwa.

Hata kwa Tanzania, kuna makabila yaliwakubali na kuwapokea Wakoloni bila upingamizi. Wanyamwezi, Wahehe, Wangoni, nk waliamua kula nao sahani moja na kufanya maisha ya jamaa kuwa magumu walau kwa siku za mwanzo. Hapa napo unarudi kwenye lilelile swali, je kulikuwa na haja ya kuwagomea na matokeo yake yakawa kifo cha Isike, Mkwawa, Kinjeketile Ngwale na wananchi wengi sana ambao kulikuwa hakuna haja/kulikuwa na haja?

Tukirudi kwenye kesi yetu hapa ambayo imeumiza sana watu kichwa, Chadema kulikuwa na haja ya kumsusia (PROTEST) Kikwete pale Bungeni? Kulikuwa na haja ya Dr. Slaa kutokufika sehemu ya kuapishwa Kikwete pale uwanjani?

Kwangu mie, miaka ya zamani ningelijibu kuwa ilikuwa ni ushamba wa hali ya juu. Utamsusiaje mtu ambaye kesho yake unaenda kwake kumuona? Hiii hali iliendelea kuwepo kichwani kwangu hadi wakati wa vita kati ya Iraq na Iran (Israel vs Palestine) ambapo kila wakati nilikuwa nashangaa jambo moja kuwa kila wakisema wiki lijalo, watakaa mezani kujadili kusimamisha vita, basi vita ilikuwa inazidi kuwa kali sana. Zinapigwa utafikiri wamesema mwisho wa dunia unakaribia.
Nilimuuliza kaka yangu nini kinasababisha hii kitu na yeye akanijibu kwa kiingereza "Bargaining power at the mediation table."

Sina uhakika kwa kiasi gani, Nguvu ya CHADEMA na Dr. Slaa kwa CCM na hata kwa IKULU kwa sasa imekuwa kiasi gani au kupungua kwa kitendo chao cha kumsusia Kikwete na tume yake ya Uchaguzi. Je kama wasingelifanya hivyo, CCM ambayo hata kwenye kampeni zao hawakuwa na ajenda ya katiba mpya, wangelianzisha mchakato huu?

Labda kuna vijimaswali kadhaa inabidi kujiuza na haswa watu kama Lady FF (ingawa nafikiri atakuwa anafahamu hata zaidi yetu wengi humu ndani ya JF) kuwa, msuso wa CHADEMA, umeipa Bargaining Power kiasi gani hapa Tanzania against CCM/Ikulu/Serikali ya TZ?

MAONI YANGU: Kuna dalili kubwa kuwa, kususa kwa CHADEMA kumeleta mchakato wa katiba mpya. Sidhani kama CCM wangelianzisha kitu kama hiki bila ya kusukumwa kutoka nje kama Newton's law of motion inavyosema "a body will remain at rest or will continue to move at a constant velocity, unless an external force is applied. "
Ni mtu ambaye hafikiri sana na hajui au anajua ila anajifanya hajui (FF) ndiye atakuja na maelezo kuwa CCM wenyewe wameamua tu kubadilisha katiba na Rais mwenye kaamua tu kwa HURUMA yake kuonana na Chadema.

AGAIN, remember "a body will remain at rest or will continue to move at a constant velocity, unless an external force is applied. " Ukiona VINAELEA, VIMEUNDWA.

Ningekubaliana nawe ingekuwa Kikwete alisubiri kutia saini sheria kabla ya kukutana na CHADEMA lakini kwa hali ilivyo ni wazi kuwa CDM waliona hawatopata kitu kuendelea kususa na wao lazima wajitie kwenye Behewa kabla halijaondoka.
Kwa vile mara zote huwa wanasusa na wakirudi ndani sheria zishapitishwa sioni kuwa walisaidia chochote. Kubwa ninaloliona mimi ni kjiuliza nafsini mwangu jee hii ina maana kuwa CHADEMA wanakubali yote yale waliosusa hapo kabla? Pengine na filosofi zako unaweza kunisaidia kuelewa hapo.
 
Siku hizi hata MABUA YANA FAIDA..............Haijalishi wamevuna mahindi au mabua cha msingi wamevuna.............NADHANI WAMETUMIA KANUNI YA

"
IF YOU CA NOT WIN THEM JOIN THEM!"!!!!!!
 
Hofstede,

Tupo pamoja sana ila naona umenisoma haraka haraka na ukapotea mpangilio wa kutokujua mawazo yangu yako.

Nashukuru kwa nyongeza ya Newton's third law of motion ambayo naona watu kama FF wanaiogopa sana. Ukweli ni kuwa Action ya Chadema kwa ujumla, imewafanya hawa waliolala kwa miaka 50 hatimaye waaanze kuamka kutoka usingizini. Wanatoa lugha kali kwa hasira na wenye kujua tunajua tu kuwa External force inayowapiga, inawasumbua sana.

Nakubaliana na maneno yako ya mwisho ya kurusha mawe na hata Nape Nnauye jusi kasema hayo maneno kuwa kuna siku mawe yatarusha na hasa hakuna watu wabaya duniani kama wale wanaosema "We have nothing to loose." Waholanzi mabadiliko makubwa sana yalifanywa na hawa vijana wanaosema hivyo. Ufaransa ndiyo hadi iliwaka moto kwa usemi huo.
Sikonge thread yako imekaa kipanyapanya. Maana anauma na kupuliza, umejaribu kwa kiasi kikubwa kufikisha ujumbe kwa pre-emptive style. Mimi sijui nakubaliana na wewe ama napingana na wewe na sijui maoni yako yanajibu maoni ya FF au umemqoute FF kwenye picha tu kule juu na hapo chini ni yako. Ila kama ni yako ama ya FF nijibu tu thread kwa ujumla na hasa kwa kuwa kwenye maoni yako umetumia Newton's first law au Law of inertia kuelezea effect ya 'kususa kwa CHADEMA' , mimi nitumie Newton's law pia kuelezea jinsi amavyo huko kususa kwa CDM kulivyoleta impact katika siasa za Tanzania.

Kwa kutumia Newton's third law which states 'For every action, there is an equal and opposite reaction.' Action ya CDM ni dhahiri imeleta reaction ya watawala kujua kuwa Tanzania ya leo si ile ya Nyerere ya kubuluza watu and sooner or Later itakuwa haitawaliki kama wataendelea kulazimisha matakwa yao badala ya yale ya wananchi. Mchakato wa katiba ni moja ya theatre za kuonesha kuwa wanasikiliza. Ila kama watataka kuu-hijack na kuufanya wa CCM v CDM, the only loser will be Country. Kurudia mchakato huu tena baada ya miaka miwili ya kupatanishwa na kupata serikali ya kitaifa baada ya mali kuharibiwa na maisha kupotea kutokana na CCM kulazimisha matakwa yake haitakuwa positive investment kwa CCM na JK, maana wao ndiyo walioshikilia mayai(wahodhi rasilimali za taifa) pindi mawe yakianza kurushwa watapoteza wao hata kama warushaji watakuwa wametolewa uhai.
 
Back
Top Bottom