Kumradhi Mtukufu Mheshimiwa Rais wetu Magufuli

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Kwa unyenyekevu na heshma kubwa, naomba kuandika kwako ewe mheshimiwa amiri jeshi mkuu, mkuu wa Nchi na Serikali kiongozi wetu mpendwa Magufuli.

Ninachokiandika kwako Mheshimiwa Rais; haimaanishi kuwa najua kukuzidi muheshimiwa, au pengine mimi nina elimu sana, la hasha! Bali najaribu kuchangia kauelewa kangu kiduchu nilikonako kama mchango wangu kwa nchi yetu hii mheshmiwa Rais wangu.

Mheshimiwa Rais; Ili taasisi yeyote (ya umma au binafsi) iweze kufanikiwa, kuna kanuni za kitaalamu na pengine za kimaumbile zinazokubalika ulimwengu mzima ambazo ni lazima zifuatwe vinginevyo lazima taasisi itashindwa kufikia malengo yake, na najua nawe hili unalielewa vyema ila ni katika kukumbushana tu mheshimiwa rais wangu. Kanuni hizo zilikuwepo, zipo na zitakuwepo tu iwe tunapenda ama hatupendi, yaani ni sawa na ambavyo ni lazima binadamu ale ili aishi vinginevyo atakufa.

Mheshmiwa rais; Ili taasisi yeyote iweze kufanikiwa, ni lazima iwe na 1.maono (vision) 2. Mpango mkakati (strategic plan) na iufuate kikamilifu, 3. Rasilimali vitu/fedha na 4. Rasilimali watu. Mkuu sio kuwa nakufundisha maana najua tayari yote haya unayajua ila nakukumbusha tu maana najua una majukumu mengi na unaweza kusahau baadhi ya vitu.

Mheshimiwa Rais; naomba nikukumbushe kidogo kuhusu hili la "Rasilimali watu" kwa leo ambapo kwa mazingira haya nazungumzia "watumishi wa umma katika upana wake". Nimeona nilizungumzie hili kwa kuwa pengine ndilo eneo kubwa zaidi ambalo linaweza kuamua hatima ya taasisi yeyote ile, kwa muktadha huu; "Serikali yako tukufu".

Mheshimiwa Rais wetu mpendwa; Ili taasisi yeyote iweze kufanikiwa (Serikali yako adhimu kwa muktadha huu) ni lazima 1. iwe na Rasilimali watu/ Watumishi wenye uwezo mzuri na 2. Itumie mbinu za kitaalam na zinazokubalika kitaalam au kimaumbile (universally acceptable) za kuwafanya watumishi hao wafanye kazi kwa ari, juhudi na maarifa ili kuleta matokeo yanayolengwa na taasisi (kwa muktadha huu, malengo ya serikali yako mh.Rais).

Mheshimiwa Rais: ukiangalia tasisi zote duniani za umma au binafsi zilizofanikiwa sana, utagundua kwamba waliajiri watumishi wenye uwezo mzuri na kisha wakawekeza katika kutumia mbinu za kitaalam zinazowajenga watumishi ili watekeleze malengo na kuleta matunda yaliyokusudiwa na kinyume chake taasisi zilizoshindwa nasikuwekeza kwenye maeneo hayo. Najua mh.Rais wewe ni mtafiti na hilo unalijua vizuri sana.

Mheshmiwa Rais wetu; Kote ulimwenguni, wataalamu wa masuala ya kazi, ajira na mambo ya rasilimali watu kwa ujumla, wanakuballiana (kinadharia na kiutafiti) kuwa ili taasisi ifanikiwe, ni lazima wafanyakazi washughulikiwe katika namna ambayo inawatia hamasa na ili kuwatia hamasa ni lazima yafuatayo yawepo;-

Kuwe na hali ya Kukubalika (appreciation). Wafanyakazi huhamasika sana pale wanapofanya jambo jema bosi wao akaonesha “appreciation”. Kinyume chake hujikatia tama na kuamua bora liende.

Heshima “ be valued” wafanyakazi huhamasika wanapohisi kuwa wanadhaminiwa na kuna hali ya kuheshimiana na viongozi wao. Kinyume chake hukata tama na kujiona ni viumbe wasio na maana kwenye taasisi.

Kuaminika “be trusted” mfanyakazi akigundua kuwa bosi wake anamuamini, huhamasika kujitahidi zaidi ili kulinda uaminifu wake kwa bosi wake kinyume chake akiona haaminiki hata pale anapotunza uaminifu hukata tamaa.

Kushirikishwa kwenye maamuzi na kupewa majukumu; wafanyakazi hupenda kushirikishwa kwenye maamuzi kwa namna nzuri na kisha kupewa majukumu (kwa namna ya kuelekezwa zaidi kuliko kuagizwa), hali hiyo huwafanya kujihisi kwamba wao ni sehemu kamili ya maamuzi na majukumu wanayotekeleza hivyo kujituma haswa.

Mkuu mheshimiwa Rais wetu mpendwa; yako mengi, ila sipendi nikuchoshe zaidi hasa ukizingatia una majukumu mengine mengi na muhimu. Hata hivyo, nakushauri kuwa, kama ikikupendeza, inaweza kuwa na faida kama utayazingatia hayo hapo juu katika serikali yako tukufu kwani kwa kufanya hivyo, watumishi wa umma watakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kufanikisha malengo ya serikali yako tukufu katika upana wake na hivyo kuiletea nchi yetu matunda stahiki.

Mwisho nikuombe radhi mh. Rais wangu kwa kukuchukulia muda wako kusoma mambo yote haya.Yapo mengi lakini siwezi kuyazungumza yote kwa wakati mmoja. Kadhalika kama nitakuwa nimekuudhi au kukukosea kwa namna yeyote ile unisamehe kwani mimi ni mtu mnyonge sana nisiye na hili wala lile na nisiye na wakunitetea kama ukiamua kunifanya lolote.Nikutakie kila la heri katika majukumu yako.
 
Kwa unyenyekevu na heshma kubwa, naomba kuandika kwako ewe mtukufu amiri jeshi mkuu, mkuu wa nchi na serikali kiongozi wetu mpendwa Magufuli.

Nnachokiandika kwako Mtukufu Rais, haimaanishi kuwa najua kukuzidi muheshimiwa, au pengine mimi nina elimu sana, la hasha! Bali najaribu kuchangia kauelewa kangu kiduchu nilikonako kama mchango wangu kwa nchi yetu hii mheshmiwa rais.

Mtukufu Mheshimiwa Rais: Ili taasisi yeyote (ya umma au binafsi) iweze kufanikiwa kuna kanuni za kitaalamu nap engine za kimaumbile zinazokubalika ulimwengu mzima ambazo ni lazima zifuatwe vinginevyo lazima taasisi itashindwa kufikia malengo yake, na najua nawe hili unalielewa vyema ila ni katika kukumbushana tu mheshimiwa. Kanuni hizo silikuwepo, zipo na zitakuwepo tu iwe tunapenda ama hatupendi yaani ni sawa na ambavyo ni lazima binadamu ale ili aishi vinginevyo atakufa tu.

Mtukufu rais; Ili taasisi yeyote iweze kufanikiwa, ni lazima iwe na 1.maono (vision) 2. Mpango mkakati (strategic plan) na iufuate kikamilifu, 3. Rasilimali vitu/fedha na 4. Rasilimali watu.Mkuu sio kuwa nakufundisha maana najua tayari yote haya unayajua ila nakukumbusha tu maana najua una majukumu mengi na unaweza kusahau baadhi ya vitu.

Mtukufu rais; naomba nikukumbushe kidogo kuhusu hili la rasilimali watu kwa leo ambapo kwa mazingira haya nazungumzia watumishi wa umma. Nimeona nilizungumzie hili kwa kuwa pengine ndilo eneo kubwa zaidi ambalo linaweza kuamua hatima ya taasisi yeyote ile, kwa muktadha huu; serikali yako tukufu.

Mheshimiwa Rais wetu mpendwa; Ili taasisi yeyote iweze kufanikiwa (serikali yako adhimu kwa muktadha huu) ni lazima 1. iwe na rasilimali watu/ watumishi wenye uwezo mzuri na 2. Itumie mbinu za kitaalam na zinazokubalika kitaalam au kimaumbile (universally acceptable) za kuwafanya watumishi hao wafanye kazi kwa ari, juhudi na maarifa ili kuleta matokeo yanayolengwa na taasisi (kwa muktadha huu, malengo ya serikali yako mh.rais).

Mtukufu rais: ukiangalia tasisi zote duniani za umma au binafsi zilizofanikiwa sana, utagundua kwamba waliajiri watumishi wenye uwezo mzuri na kisha wakawekeza katika kutumia mbinu za kitaalam zinazowajenga watumishi ili walete malengo yaliyokusudiwa na kinyume chake. Najua mh.wewe ni mtafiti na hilo unalijua vizuri.

Mtukufu rais; Kote ulimwenguni, wataalamu wa masuala ya kazi, ajira na mambo ya rasilimali watu kwa ujumla, wanakuballiana (kinadharia na kiutafiti)kuwa ni ili taasisi ifanikiwe nilazima wafanyakazi washughulikiwe katika namna ambayo inawatia hamasa na ili kuwatia hamasa ni lazima yafuatayo yawepo;-

Kukubalika (appreciation). Wafanyakazi huhamasika sana pale wanapofanya jambo jema bosi wao kuonesha “appreciation”. Kinyume chake hujikatia tama na kuamua bora liende.

Heshima “ be valued” wafanyakazi huhamasika wanapohisi kuwa wanadhaminiwa na kuna hali ya kuheshimiana na viongozi wao.Kinyume chake hukata tama na kujiona ni viumbe wasio na maana kwenye taasisi.

Kuaminika “be trusted” mfanyakazi akigundua kuwa bosi wake anamuamini, huhamasika kujitahidi zaidi ili kulinda uaminifu wake kwa bosi wake kinyume chake akiona haaminiki hata pale anapotunza uaminifu hukata tamaa.

Kushirikishwa kwenye maamuzi na kupewa majukumu; wafanyakazi hupenda kushirikishwa kwenye maamuzi na kisha kupewa majukumu, hali hiyo huwafanya kujihisi kwamba wao ni sehemu kamili ya maamuzi na majukumu wanayotekeleza na kujituma haswa.

Mkuu yako mengi, ila sipendi nikuchoshe hasa ukizingatia una majukumu mengine mengi na mhimu. Hata hivyo, nakushauri kuwa, kama ikikupendeza, inaweza kuwa na faida kama utayazingatia hayo hapo juu katika serikali yako tukufu kwani kwa kufanya hivyo, watumishi wa umma watakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kufanikisha malengo ya serikali yako tukufu katika upana wake.

Mwisho niombe radhi kwa kukuchukulia muda wako kusoma mambo yote haya. Kadhalika kama nitakuwa nimekuudhi au kukukosea kwa namna yeyote ile unisamehe kwani mimi ni mtu mnyonge sana nisiye na hili wala lile na nisiye na wakunitetea kama ukiamua kunifanya lolote.
Kama mambo magumu andika barua acha kazi,Ubembelezwe wewe nani ?Taifa la watu milioni 45 unaongelea watumishi wa uma na binafsi mpo wangapi?Kuna kundi kubwa huku tunamkubali Raisi wetu,Tulilalamika sana kuhusu ufisadi na watumishi wa uma kuwa na dharau,Acheni kazi hatuwezi bembeleza wezi wa kodi
 
Kama mambo magumu andika barua acha kazi,Ubembelezwe wewe nani ?Taifa la watu milioni 45 unaongelea watumishi wa uma na binafsi mpo wangapi?Kuna kundi kubwa huku tunamkubali Raisi wetu,Tulilalamika sana kuhusu ufisadi na watumishi wa uma kuwa na dharau,Acheni kazi hatuwezi bembeleza wezi wa kodi
mkuu, jana kwenye uzi huu
Unapobaki kimya wakati mwenzako akidhulumiwa, hakuna atayekusaidia zamu yako ikifika
niliandika hivi:

"Watanzania tumekuwa na utaratibu wa ajabu sana. Utaratibu wa mtu au kundi linapoona mtu au kundi lingine linadhulumiwa, tena dhulma za wazi kabisa, basi mtu au kundi ambalo haliguswi moja kwa moja na dhulma hiyo kwa wakati huo, si tu kwamba halimtetei anayedhulumiwa kwa namna yeyote bali hata halifanyi jitihada zozote za kukemea dhulma husika na pengine linaweza kushabikia.

Kwa mfano; kumekuwa na kautaratibu kwa watu wanaona kwa mfano mtu anaibiwa wanaangalia tu, watu wanawekwa ndani kwa dhulma za wazi wengine kimya, watu wanadhulumiwa haki zao mbalimbali wengine kimya. na mifano mingine isiyo na idadi ambayo sipendi kuitaja humu.

Wale wasiochukua hatua yeyote au wanaoshangilia wakati wengine wanadhulumiwa ukiwauliza jibu lao rahisi sana " Kwani Mimi/sisi inatuhusu nini?"

Wewe kaa kimya wakati mwenzako anadhulumiwa, tena dhuluma za wazi kabisa ila tu ujue nawe ikifika siku yako ya kudhulumiwa, na wengine nao watabaki kimya vile vile. Utapiga kelele kuomba msaada lakini hakuna atakayekusaidia.Sana sana wataibuka wanaokukejeli, kushabikia au kuunga mkono jinsi unavyodhulumiwa kama ambavyo nawe ulikuwa unafanya.

Watanzania tujengeni tabia ya kuwa wakweli na kutetea haki hata kama anayedhulumiwa ni mtu wa tatu. "Usiseme tu wanaodhulumiwa au kubaguliwa si wale, mimi si miongoni mwao" hiyo ni dhambi ambayo "Karma" yake ni mbaya sana na itamfika kila mtu kwa wakati wake na katika namna na mazingira ambayo hukuwahi kuyafikiria."
 
Kama mambo magumu andika barua acha kazi,Ubembelezwe wewe nani ?Taifa la watu milioni 45 unaongelea watumishi wa uma na binafsi mpo wangapi?Kuna kundi kubwa huku tunamkubali Raisi wetu,Tulilalamika sana kuhusu ufisadi na watumishi wa uma kuwa na dharau,Acheni kazi hatuwezi bembeleza wezi wa kodi
Mkuu, mtu anapozungumzia mfano ugonjwa wa malaria, haina maana kwamba hakuna magonjwa mengine lakini uwepo wa magonjwa mengine hakuwezi kuwa ni sababu ya kutozungumzia malaria. Hata hivyo mtu hawezi kuzungumzia vitu vyote wakati mmoja na sehemu moja. Kwa hiyo ukiona mwenzako kazungumzia kitu kimoja kaacha kingine, wewe zungumzia hicho kilichoachwa na mwingine atazungumzia kingine na kingine.

Pia usiwe na tabia ya kuzungumzia kitu pale kinapokuathiri wewe tu, jenga tabia ya kuzungumzia kitu chochote tenye maslahi kwa ustawi wa jamii ya mwanadamu hata kama atakayenufaika ni mtu usiyemjua. Huo ndio ubinadamu na uungwana. Unatakiwa ujue hata hapo ulipo sasa upo hivyo ulivyo maana kuna watu walikuhakaingia na pengine wewe hujawasaidia chochote na hutawasaidia.kwanza wala hawakujui pengine. Jenga tabia ya kufikiri nje ya boksi.
 
kumwita binadamu mwenzako mtukufu hapa duniani ni kumkashifu Mwenyezi Mungu, Mungu peke ndio ana weza kuitwa mtukufu. Ujipange kujieleza kwake Mungu kwanini ulitumia jina lake kumwita binadamu mwenzio.
 
Hakuna MTUKUFU anaeishi hapa duniani.
Nimejaribu kuelewa ulchokua unamaanisha
Inawezekana usielewe kwa sababu kubwa mbili, amma umeona uvivu wa kusoma hivyo hukusoma kabisa na kisha ukawahi kucoment, au umeamua kuwa usielewe. hata hivyo hakuna kitu ambacho kishawahi kueleweka kwa watu wote au kuungwa mkono au kupingwa na watu wote. Hii inatokana na tabia ya kimaumbile ambayo inatufanya tuangalie vitu vile tulivyo badala ya kuangalia vitu vile vilivyo.
 
Nawashangaa sana wale wanaosema eti nidhamu ya watumishi umma imerudi wakati mtumishi huyu katelekezwa na wala hathaminiwa katika awamu hii.r

Mtumishi ambaya hasaminiwa atapata wapi morali ya kazi?
Ili mfanyakazi kwenye taasisi yeyote aweze kufanya vizuri sana "outstanding performance" anatakiwa awe na nidhamu ya hali ya juu, morali ya kazi, kujituma, ubunifu, elimu na ujuzi sahihi na kikubwa kupita vyote pengine ni dhamira njema. Kwa hiyo pamoja na juhudi za kujenga nidhamu ambazo kimsingi ni muhimu, ipo haja pia ya kuangalia ni kwa namna gani unaweza kujenga nidhamu na wakati huo huo hayo mengine nayo yakajengeka na kuimarika ili kuwa na matokeo bora.
 
Wafanyakazi walivifunga Vitabu vyote vya STANDING ORDERS AND REGULATION kwenye Serikali na Taasisi zetu wakaanza kutumia Kanuni zao za kujineemesha wao Binafsi na kugeuza Ofisi zao kuwa Maduka na Kampuni zao yote waliweka pembeni.Na haya tunayoyashuhudia ndiyo Matokeo.Kisha watu wanakuja hapa JF Kulalama hiki na kile.Mh.Raisi kaza Buti turudi ktk mstari NIDHAMU MAADILI MIIKO NA UAMINIFU Tusonge mbele
 
Ili mfanyakazi kwenye taasisi yeyote aweze kufanya vizuri sana "outstanding performance" anatakiwa awe na nidhamu ya hali ya juu, morali ya kazi, kujituma, ubunifu, elimu na ujuzi sahihi na kikubwa kupita vyote pengine ni dhamira njema. Kwa hiyo pamoja na juhudi za kujenga nidhamu ambazo kimsingi ni muhimu, ipo haja pia ya kuangalia ni kwa namna gani unaweza kujenga nidhamu na wakati huo huo hayo mengine nayo yakajengeka na kuimarika ili kuwa na matokeo bora.
Najikuta napata hasira kila nikisoma unachoandika ww mtu,unadhan mwanao ukimtia hofu kisa alikuwa anafeli ndiyo atafaulu mtihani?
Ww bure kabisa rudi tena kasome management and administration uone mbinu za uongozi,eti mwasema mnawasaidia wanyonge,kwan mwalimu cyo mnyonge,mbona viongozi wa siasa ktk utawala mishahara yao mizuri na hamuwabani km hawa watumishi wa umma? Na ndiyo maana hao mawazir na wakuu wamikoa/wilaya wana fanyakazi vizuri kwakuwa maslahi yao yanalindwa,acheni upumbavu ,km huna kazi isiwe chuki kwa mwenye kibarua chake..
Naamini rais ataona kilio cha watumishi cyo nyie wenye chuki.
 
Back
Top Bottom