Ukweli Thread Ni NzuriJitaidi kuwa mshauri mzuri tu. Wewe ni wa kwanza kufanya haya ulipokuwa mtoto ila ulivumiliwa, kwann ushindwe wewe kumvumilia mtu ambaye kapewa zawadi ya maisha marefu na Mungu?
hahaha hata mimi asee kuna kipindi nilimuudhi bi mkubwa yani alikua ananigombeza namjibisha aloo akaanza kuongea huku analia yani nilijisikia vibaya sana yani mpaka leo sijawahi kukaa kubishana nae tena sitaki kuona yale machozi tena.Nani anaweza mpiga mzazi wake. Mimi bi mkubwa wangu nikiongea nae huwa sauti yangu kama naongea na MUNGU. Naongea nae kama naongea na raisi.
"Na Mola wako Mlezi ameamrisha kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu, na wazazi wawili muwatendee wema. Mmoja wao akifikia uzee, naye yuko kwako, au wote wawili, basi usimwambie hata: Ah! Wala usiwakemee. Na sema nao kwa msemo wa hishima. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma. Na useme: Mola wangu Mlezi! Warehemu kama walivyo nilea utotoni." Qur'an 17: 23-24 |