Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,010
- 9,874
Serikali iangalie hili suala la ulazima wa wajawazito kupima na waliowapa mimba.
Zahanati na kila sehemu inayotoa huduma ya wajawazito imekuwa ni lazima waende na waume zao kupima UKIMWI, hili sio suala baya kwa sababu ya mtoto atakayezaliwa.
Lakini nadhani ni muhimu kutoa ushauri kwa majmzito kuliko kulazimisha mama husika aje na mumewe, what if mwanamke amekataliwa na aliyempa mimba, inakuwaje kama alibakwa? Vipi kuhusu hawa wahudumu nk ambao hupata watoto kwa watu wasiowajua au hata kama wanawajua wanakuwa hawako tayari kuwapokea.
Je, sio kwamba tunawaumiza wanawake kwa kuwalazimisha kuja na wanaume, na wao wana maumivu ya kutelekezwa na waliowapa mimba, au maumivu ya lifestyle yao?
Sikatai kuona umuhimu wa swala la kumlinda mtoto, lakini tuwe na double standards ili tusije kumuumiza mama kisaikolojia. Kama wauguzi watakuwa makini wataona taarifa nyingi za wazazi wa kiume zinazojazwa huwa ni za uwongo, aidha wadanganye kazi za wazazi wenzao au kusema kuwa wamekufa.
Kama mtakuwa makini mtaona sura za wazazi hubadilika wanapojibu kuhusu waume zao, mara nyingi huwa ni maumivu kwao. Tupunguze uwongo! Tujue kabisa family planning kwetu bado ndogo sana hivyo ni ngumu kwa mtu kuwa na mume ambaye amempatia mimba bila mipango ya awali.
Wenyewe mnashuhudia idadi ya singe mothers, hii inaonyesha ukosefu wa ushirikiano baina ya wazazi na wao.
Nawasilisha!
Zahanati na kila sehemu inayotoa huduma ya wajawazito imekuwa ni lazima waende na waume zao kupima UKIMWI, hili sio suala baya kwa sababu ya mtoto atakayezaliwa.
Lakini nadhani ni muhimu kutoa ushauri kwa majmzito kuliko kulazimisha mama husika aje na mumewe, what if mwanamke amekataliwa na aliyempa mimba, inakuwaje kama alibakwa? Vipi kuhusu hawa wahudumu nk ambao hupata watoto kwa watu wasiowajua au hata kama wanawajua wanakuwa hawako tayari kuwapokea.
Je, sio kwamba tunawaumiza wanawake kwa kuwalazimisha kuja na wanaume, na wao wana maumivu ya kutelekezwa na waliowapa mimba, au maumivu ya lifestyle yao?
Sikatai kuona umuhimu wa swala la kumlinda mtoto, lakini tuwe na double standards ili tusije kumuumiza mama kisaikolojia. Kama wauguzi watakuwa makini wataona taarifa nyingi za wazazi wa kiume zinazojazwa huwa ni za uwongo, aidha wadanganye kazi za wazazi wenzao au kusema kuwa wamekufa.
Kama mtakuwa makini mtaona sura za wazazi hubadilika wanapojibu kuhusu waume zao, mara nyingi huwa ni maumivu kwao. Tupunguze uwongo! Tujue kabisa family planning kwetu bado ndogo sana hivyo ni ngumu kwa mtu kuwa na mume ambaye amempatia mimba bila mipango ya awali.
Wenyewe mnashuhudia idadi ya singe mothers, hii inaonyesha ukosefu wa ushirikiano baina ya wazazi na wao.
Nawasilisha!