Tajiri la Bitcoin
JF-Expert Member
- Apr 9, 2017
- 1,082
- 641
Anaitwa mama, rais wa JMT, amir jeshi mkuu, kipenzi cha watu, Tanzanite lady, mkombozi wa watanzaniaUkweli ni kwamba, lipo kundi ndani ya Taifa hili tukufu la Tanzania linaloinyooshea vidole Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwamba imekumbwa na Rushwa na Ufisadi ghafla.
Kundi hili linamwona Rais Samia Suluhu Hassan kama ni Mtu aliyeshindwa kupambana na Rushwa na Ufisadi ila Hayati Dkt John Pombe Joseph Magufuli ambaye hata hivyo kutetea mfu ni kumkufuru Mungu.
Rais Samia Suluhu Hassan wakati akiwa Bandari ya Dar es Salaam alilishambulia vikali kundi hili linalodai kulinda na kutetea Legacy ya Hayati Dkt John Pombe Magufuli kwa kuinyooshea vidole Serikali yake kwa Rushwa na Ufisadi yenye vimiezi vichache tu madarakani.
HOJA YANGU KWENU NI HII
Kati ya nafasi zaidi ya 1,000 za Uteuzi alizopewa Rais na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Samia Suluhu Hassan Viongozi wapya aliowateua hawajafika watu 100 hadi naandika makala hii. Hawa Viongozi zaidi ya 900 ni Viongozi walewale wa awamu zilizopita hasa hasa awamu ya tano.
SWALI LANGU
1. Hawa watu wanaonyooshewa Vidole wameleta tabia mpya ya Rushwa na Ufisadi awamu ya Sita wametoka Wapi kwa kipindi hiki kifupi au ni hawa wapya 100?
2. Je, nihawahawa waliotoka awamu zilizopita leo wote wamegeuka ghafla mashetani weusi au ndicho walichokifanya huko nyuma ila Utawala uliwaatamia tu na leo wamekwama kuiba wanaanza kubeza?
3. Au wanaposema wanalinda legacy maana yake ni kutekeleza Rushwa na Ufisadi kisha kuisingizia Awamu ya Sita ambayo hata mwaka haina au ndio Legacy kwa Vitendo hii?
4. Au mambo haya yanafanyika kwa maksudi mazima ili kumdhoofisha Rais Samia Suluhu Hassan na Serikali yake? Je nikweli Rushwa imekithiri au nihadaa tu wanafanya kwa Wananchi?
5. Mnaotetea Legacy ya Hayati Dkt John Joseph Pombe Magufuli kwa kutafuna mali za umma kwani yeye alipenda Rushwa na Ufisadi?Msitafute laana,
NB: uwekeni Uzalendo wa Taifa letu mbele kuliko masilahi yetu binafsi kwani nchi hii ni kubwa kuliko yeyote kila mmoja aupinge Ufisadi toka ndani ya moyo wake,