geraldkowero1
JF-Expert Member
- Jul 5, 2014
- 1,838
- 644
Prof hasomi mwelekeo wa upepo???
Atausoma kwa kukosa nini? Kazi aliyotumwa ameimaliza. Mimi nawalaumu sana chadema kwani toka wanaunganisha hizo nguvu kuzaa ukawa nilielewa ni kwa masuala ya kutetea katiba mpya na nzuri basi na sio zaidi ya hapo. Kuungana kumteua raisi mmoja na kuachiana majimbo mlipenda kujiua na kujicheleweshea maendeleo wenyewe.Sasa siku za mbele msijepitisha maamuzi mazito kama yale bila kuwashirikisha wanachama wenu ni hatari sana. Viongozi wangechukua maoni ya wanachama wao ambao wangewapa faida na hasara zake haswa kwa siasa na misimamo ya baadhi ya viongozi wa baadhi ya vyama isiyotabirika msingeleta matatizo makubwa. Hivi kweli wakati mnaungana na cuf mlikuwa mmeshasahau uchaguzi wa 2010 Lipumba alikiri kumpigia kampeni Kikwete eti kwa kuwa alimwona kuzidiwa? Usaliti huu kwa wananchi aliowawakilisha na kwa upinzani aliuombea lini msamaha? Ni kwa nini hamkuyajadili kwanza kwa kuweka misingi(criteria) ya haya anayoyaona sasa kama mapungufu yanayohitaji makubaliano kwanza? Ni kwa nini hata huo ukawa haukuandikishwa kabisa na kuwa na katiba yake ambayo ingetoa suluhu kwa haya yanayooneoana ni matatizo?Sasa muda mliobakia nao mnaamini mnaweza kuyarekebisha yote hayo kabla ya kampeni kuruhusiwa rasmi? Kwa hali hii ilivyo ni bora muungane mnaokubaliana na mtangaze mgombea wenu.