Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,426
- 7,736
Wakinamama takribani watatu wamethibitika kupewa talaka baada ya hekaheka za uchaguzi. Wete katika jimbo la Gando mume ametoa talaka kwa bi. Zawadi Ally Haji
"Niliachwa kipindi hicho cha siasa, mume aliniambia nikienda kupiga kura ndio talaka yangu na mimi nikaenda, nilivyorudi jioni ndio nikawa nishaachika. Nilipokwenda nikamchagua Rais ninaemtaka mie, Hussein na Salim Mussa, kwa sababu ndio yeye hakuwataka sikumfuata upande wake atakao, kwa sababu nimefata upande wangu ninaoutaka" Alisema Bi. Zawadi, mke alieachika.
Mzazi wa Bi. Zawadi, Zadi Hamad Iddy amesema kwa masikitiko binti yake huyo amerejea nyumbani akiwa na mtoto wake mdogo.
"Sijapokea uzuri kwa sababu alipoanza kumposa huyu ni mwali na mama yake alikuwa ni mwana CCM na alipokuja tulimwambia unakuja tuolea mwenetu lakini yuko upande wa CCM na huyu mwanaume alikuwa ni CCM, baada ya kukaa na kugombana na wazazi wake akatoka CCM akajifanya CUF kwanza, baadae ndio akaja ATC lakini wakati wote huo hawana ugomvi lakini ikifika wakati wa siasa tu!
Safari hii anamtilia tena usiende kupiga kura kwa sababu ajua ni against na yeye, huyu ni CCM, yeye ni ATC. Kwao hatuwaingilii lakini hii kuacha sasa, kamuacha kweli na sasa hivi yuko nyumbani kama unavyomuona wala hajaja kusema anamrejea, kajizuia na sisi tumejizuia. Si jambo zuri, huu ni mchezo tu ingawa twawania dola sio kama mchezo wa mpira"
Nae Jaffari Suleiman amesema binti yake ameachwa kwa habari ya siasa, alienda akakaa PO Shezamwe, aliporudi mume akamtaliki hivyo amerudi nyumbani na watoto wawili bila ya kumshughulikia mke aliemuacha na watoto wake. Jaffari anasema hatua aliyochukua ni kulifikisha suala hilo kwenye chama na Serikali.
"Niliachwa kipindi hicho cha siasa, mume aliniambia nikienda kupiga kura ndio talaka yangu na mimi nikaenda, nilivyorudi jioni ndio nikawa nishaachika. Nilipokwenda nikamchagua Rais ninaemtaka mie, Hussein na Salim Mussa, kwa sababu ndio yeye hakuwataka sikumfuata upande wake atakao, kwa sababu nimefata upande wangu ninaoutaka" Alisema Bi. Zawadi, mke alieachika.
Mzazi wa Bi. Zawadi, Zadi Hamad Iddy amesema kwa masikitiko binti yake huyo amerejea nyumbani akiwa na mtoto wake mdogo.
"Sijapokea uzuri kwa sababu alipoanza kumposa huyu ni mwali na mama yake alikuwa ni mwana CCM na alipokuja tulimwambia unakuja tuolea mwenetu lakini yuko upande wa CCM na huyu mwanaume alikuwa ni CCM, baada ya kukaa na kugombana na wazazi wake akatoka CCM akajifanya CUF kwanza, baadae ndio akaja ATC lakini wakati wote huo hawana ugomvi lakini ikifika wakati wa siasa tu!
Safari hii anamtilia tena usiende kupiga kura kwa sababu ajua ni against na yeye, huyu ni CCM, yeye ni ATC. Kwao hatuwaingilii lakini hii kuacha sasa, kamuacha kweli na sasa hivi yuko nyumbani kama unavyomuona wala hajaja kusema anamrejea, kajizuia na sisi tumejizuia. Si jambo zuri, huu ni mchezo tu ingawa twawania dola sio kama mchezo wa mpira"
Nae Jaffari Suleiman amesema binti yake ameachwa kwa habari ya siasa, alienda akakaa PO Shezamwe, aliporudi mume akamtaliki hivyo amerudi nyumbani na watoto wawili bila ya kumshughulikia mke aliemuacha na watoto wake. Jaffari anasema hatua aliyochukua ni kulifikisha suala hilo kwenye chama na Serikali.