20PROFF
JF-Expert Member
- Nov 5, 2013
- 7,970
- 6,756
Hahaha umetumia njia ngumu sana kueleza. Ila ngoja nijaribu kuweka hivi.Dhahabu na mawe mengine ya madini yanauzwa pesa nyingi sana na wanaoyapata hutajirika, sivyo?
Basi matapeli hutafuta yaliyo ya bandia ya kufanana, yaani madini feki na huwauzia wasiojua na kuwatapeli pesa nyingi sana sivyo?
Je, watu watupe dhahabu na madini yao ya kweli kwa kuwa kuna yaliyo feki?
Je, ni kosa la madini ama ni kosa lako wewe usiyeyaelewa vizuri mpaka ukauziwa kanyaboya?
Jifunze kuyatofautisha ili usiibiwe lakini kamwe matapeli wa madini hawayafanya yaliyo ya kweli yaache kutafutwa au kuuzwa pesa nyingi!
Na watu hawatasema kwa kuwa almasi feki zimekuwa nyingi basi TUVAE VIDANI VILIVYOTENGENEZWA KWA VIJIWE VIJIWE TU VISIVYO NA THAMANI!
ni tafakuri ndogo tu mkuu,Kile kinachoigwa sana ndio kina thamani ujue, vijiwe utamuibia nani mamilioni!
Hakuna atae kaa na kuumiza kichwa kuandaa kokoto feki, maana haina thamani.
Lakini utaona watu wanakaaa kuandaa Dhahabu feki.
Shetani atapotosha na kutaka kupigan na cha kweli, ili akamate watu zaidi