Kumekucha CCM! ...na Bado!!

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,720
21,779
CCM wamtimua Shibuda


*Atupiwa virago kwenye Kamati ya Siasa
*Adai ni kundi la wanaojifanya watu wa JK


Na Suleiman Abeid, Shinyanga

MBUNGE wa Maswa mkoani hapa, Bw. John Shibuda, amejikuta katika wakati mgumu baada ya kutimuliwa kwenye kikao cha Kamati ya Siasa ya CCM ya wilaya ya Maswa, akidaiwa kutokuwa mjumbe halali.

Hali hiyo ilijitokeza jana muda mfupi kabla kikao hicho hakijaanza katika ofisi za CCM wilayani hapa, ambapo Bw. Shibuda alionekana akitoka nje ya ofisi hizo, huku akihangaika kufanya mawasiliano na viongozi wa ngazi za juu wa chama hicho.

Akizungumza na Majira baada ya kutimuliwa katika kikao hicho, Bw. Shibuda alisema kitendo hicho kilichofanywa na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo, Bw. Peter Bunyongoli na Katibu Mwenezi na Itikadi, Bw. Jeremiah Makondeko, ni cha kumdhalilisha na kumvunjia heshima ndani ya Chama.

Bw. Shibuda alisema anavyofahamu yeye ni mjumbe halali wa Kamati hiyo ya Siasa kwa mujibu wa Katiba ya CCM Ibara ya 81(1)(f) ambayo inaonesha wazi kuwa wajumbe wa kamati hiyo ni pamoja na wabunge wa majimbo, wenyeviti wa halmashauri za majiji, manispaa, miji na wilaya.

Ibara hiyo inasomeka: “Mbunge, au wabunge wanaotokana na CCM wanaowakilisha wilaya hiyo au wabunge wa aina nyingine wanaoishi katika wilaya hiyo,” ni wajumbe halali wa kamati ya siasa ya CCM wilaya.

Bw. Shibuda alielezea kushangazwa kwake na hatua hiyo ndani ya kikao hicho, ambapo siku zote amekuwa akialikwa kuhudhuria vikao vya kamati hiyo akiwa mjumbe na kuonesha ushahidi wa baadhi ya barua za mialiko kwa vikao hivyo alizokuwa akipelekewa.

Baadhi ya barua hizo za mialiko zilikuwa ni zenye kumbukumbu namba CCM/KS/28/46 ikiwa ni ya mwaliko wa kikao cha dharura cha Julai 16 mwaka huu; Kumbukumbu namba
CCM/MSW/KS.15/VOL.III/47 ya Juni 28 mwaka huu na kumbukumbu namba CCM/MSW/K.50/13/3/50 ya Julai 12, mwaka huu, ikiwa ni mwaliko wa kikao ambacho alitimuliwa kwa kuelezwa kuwa si mjumbe.

Alisema pamoja na juhudi za kumweleza Mwenyekiti wake asome Katiba vizuri, alikataa kwa kueleza kuwa toleo la Katiba chapisho la hivi karibuni halioneshi kuwa wabunge ni wajumbe wa kamati za siasa za wilaya.

Bw. Shibuda alisema Mwenyekiti huyo alisisitiza kuwa yeye ni Mwenyekiti wa Wilaya hiyo na kwamba uamuzi wake ni wa mwisho na kuendelea kumtaka atoke nje ya kikao mara moja ili wao waweze kuendelea na kikao.

“Kwa kweli nimesikitishwa sana na kitendo hiki cha kufukuzwa ndani ya kikao kama mbwa, tena mbele ya kadamnasi, sijui Mwenyekiti huyu anajivunia kitu gani, nahisi ni kile ambacho amekuwa akitamba nacho kila siku kuwa yeye ana uhusiano binafsi na Rais Jakaya Kikwete, wakati Rais alishasema hana makundi,” alidai Bw. Shibuda.

Hata hivyo, alisema hali hiyo imeanza kumpa wasiwasi iwapo atatendewa haki atakapoamua kugombea nafasi yoyote ya uongozi ambayo inahitaji kuthibitishwa na vikao vya chama, na kusema kuwa ni wazi hawezi kutendewa haki.

Akizungumza na Majira kwa njia ya simu, Katibu wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, Bw. Gustav Muba, alisema wabunge wote wa majimbo ya uchaguzi ni wajumbe halali wa kamati za siasa za wilaya.

Bw. Muba alisema iwapo kweli viongozi wa CCM wa wilaya ya Maswa watakuwa wamemfukuza ndani ya kikao Bw. Shibuda, watakuwa wamefanya makosa, na pia aliahidi kufuatilia hali hiyo mara baada ya kupokea taarifa rasmi.

“Wabunge wote wa majimbo kwa tiketi ya CCM ni wajumbe halali wa vikao vya kamati ya siasa ya wilaya, inawezekana viongozi wa Maswa watakuwa wameitafsiri vibaya Katiba, au kuna kosa fulani limefanyika katika uchapishaji, nitafuatilia hali hiyo, baada ya kupewa taarifa rasmi,” alieleza Bw. Muba.

Kwa kipindi kirefu sasa, uongozi wa CCM wilayani Maswa, umekuwa na mgogoro mkubwa unaotokana na kambi wakati wa uchaguzi wa kura za maoni za uteuzi wa wagombea ubunge ndani ya chama hicho, hali ambayo inaonekana kukithiri kadri siku zinavyokwenda.

Juzi Makamu wa Rais, Dkt. Ali Mohemmed Shein, aliwataka viongozi wa wilaya hiyo kuwa na mshikamamo wa pamoja, ili kutekeleza kikamilifu Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005, ili kulinda imani ya wananchi kwa chama hicho, lakini hata kabla hajamaliza ziara yake mkoani hapa, malumbano yameanza kujitokeza.
 
CCM wamtimua Shibuda


*Atupiwa virago kwenye Kamati ya Siasa
*Adai ni kundi la wanaojifanya watu wa JK


Na Suleiman Abeid, Shinyanga

MBUNGE wa Maswa mkoani hapa, Bw. John Shibuda, amejikuta katika wakati mgumu baada ya kutimuliwa kwenye kikao cha Kamati ya Siasa ya CCM ya wilaya ya Maswa, akidaiwa kutokuwa mjumbe halali.

.

...waandishi wengine bwana, kichwa cha habari na habari yenyewe wala haviwiani, au ndio kuuza magazeti?

hovyoo!
 
...waandishi wengine bwana, kichwa cha habari na habari yenyewe wala haviwiani, au ndio kuuza magazeti?

hovyoo!

Mchongoma angalia joke nyingine ya Saed Kubenea, the most talked about newsman in the country today:

Rais Kikwete atapeliwa

Ni katika mradi wa mabilioni
Edward Lowassa ahusishwa

Na Saed Kubenea
Mwanahalisi~Maslahi ya Taifa Mbele
July 16, 2008

BARAZA la Wadhamini la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UV-CCM), limemtapeli Rais Jakaya Kikwete katika mradi wa mabilioni ya shilingi, MwanaHALISI limeelezwa.

Baraza la Wadhamini, chini ya mwenyekiti wake Edward Lowassa, limeingia ubia na mfanyabiashara Shubhash Patel kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa mabilioni ya shilingi kinyume cha taratibu, na rais hakupewa taarifa sahihi.

 
Huyu si alikuwa mgombea urais? mbona anaonekana kama asiyekuwa na nguvu ndani ya chama hata ngazi ya wilaya?

Ama huyu alikuwa mtandao wa Sumaye na hivyo sasa mtandao wa JK wanamshughulikia?
 
Rais apata ajali

Nikanunua gazeti ili kujua kulikoni.

Rais wa chama cha ngumi Tanzania Emmanuel Mlundwa (aliwahi kuwa bingwa huyu wa EA kama sikosei) amepata ajali ya gari lakini hakuumia sana.

Nilikasirika sana. Mzee Rukhsa ndiye aliyekuwa katinga Ikulu miaka hiyo.
 
Rais apata ajali

Nikanunua gazeti ili kujua kulikoni.

Rais wa chama cha ngumi Tanzania Emmanuel Mlundwa... amepata ajali ya gari lakini hakuumia sana.

Nilikasirika sana.

Ha ha aaaaaaa ha haaaaa

This is hilarious! LOL

E bwana unaikumbuka toka wakati wa Mwinyi?

Pole mwanangu. Yani wanajifanya wajanja ile mbaya ma Editor.

Ha haaaa! Hiyo kali mwanangu!
 
Huko ni kuanguka kwa CCM ila wakishaona mbunge amepoteza mvuto kwa wananchi na kuna hatari ya kupigwa budi utakapowadia uchaguzi basi humfanyia njama za kumdhalilisha na halafu wanaibuka na mwengine ambae atafanyiwa mapinduzi na kuekwa kwenye Ubunge.CCM ndivyo walivyo wakishakutumia wanakupiga buti huku wanakwambia utajiju >
 
Miaka ya 1997 niligongana na Kichwa cha Gazeti moja la kila wiki kikisema
"Mchungaji abaka Kondoo" nililikimbilia hilo gazeti nikalinunua haraka. Hofu yangu ilikuwa huyu mtumishi wa Bwana amekuwaje hadi akafanya uharamia mkubwa namna hiyo?

Nikanunua gazeti langu nikatafuta kibaraza, pahala patulivu nijisomee bila kusumbuliwa hadi nielewe kulikoni.
TOBA!!! Kuingia ndani kwenye habari: Kumbe mchungaji anayezungumziwa kwanye habari ni wa mifugo.
Nilisikitika sana.

Waandishi angalieni kwa umakini vichwa vya Habari Mnavyouza navyo magazeti.
 
Rais apata ajali

Nikanunua gazeti ili kujua kulikoni.

Rais wa chama cha ngumi Tanzania Emmanuel Mlundwa (aliwahi kuwa bingwa huyu wa EA kama sikosei) amepata ajali ya gari lakini hakuumia sana.

Nilikasirika sana. Mzee Rukhsa ndiye aliyekuwa katinga Ikulu miaka hiyo.
Huu ni ufisadi mwingine maana wanafanya makusudi ili waweze kuuza magazeti yao lakini at the same time wametumia attractive headings ili wakushawishi kununua gazeti.
Sijui hawajatambua kuwa huu ni ufisadi pia?
 
Back
Top Bottom