Kumbukumbu ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda

Mu7

JF-Expert Member
Jun 15, 2013
1,559
1,821
Heshima zenu WanaJF wote. Niende kwenye mada:
Tarehe 7 April kila mwaka ni siku ambayo ndugu zetu Wanyarwanda huadhimisha kumbukumbu ya Mauaji ya Kimbari ambamo wapendwa wao karibia milioni 1 waliuawa. Siku hiyo kuna ibada na hotuba za viongozi mbalimbali wakikumbuka tukio hilo lililoacha makovu kama sio madonda ya kudumu mioyoni mwa Wanyarwanda wengi. Siku hiyo tumekuwa tukishuhudia kwenye vyombo vya habari jinsi machungu yanavyoamka upya na kupelekea baadhi yao kuzimia wakikumbuka matukio ya kutisha waliyoyashuhudia wakati wa mauaji yale ya 1994.
MAONI YANGU:
Kwa kuwa machungu ya tukio lile bado ni makali mioyoni mwa Wanyarwanda wengi na nchi hiyo bado inaendeleza juhudi za kuleta maelewano, maridhiano na msamaha miongoni mwa wananchi wake waliotendeana vibaya, nashauri maadhisho hayo yasitishwe kwa kuwa kibinadamu ni vigumu sana kumsamehe mtu uliyemshuhudia akimuua kikatili mzazi wako, dada yako, kaka yako, mtoto wako au mme/ mke wako kumbukumbu ya tukio inapokuwa bado kali. Ni maoni yangu tu.
Karibuni kwa michango yenu.
 
i do conquer... Yaani i was there... Jamaa wana nidhamu tu za woga.. Maana hatua kumi kila kona na kwingine kule city center.. Ni afande kasimama loaded all the time 24 seven... Kiukweli.. Tuendelee tu kuwaombea.. Maana bado hali ni tete mnoo
 
Siasa ni kitu kibaya sana.

Siasa zetu za kiafrika zisizokuwa na ajenda hupenda kukuza sana tofauti baina ya wananchi ili kushika madaraka ya kisiasa. Nchi nyingi hutumia tofauti za kikabila, na ingawa Tanzania tumebahatika sana kushindwa kujenga siasa za kikabila lakini viongozi wetu siku hizi hutumia udini na ukanda.

Tofauti za kisiasa zilziokuwapoa Rwanda na Burundi wakati huo zilitakiwa kutafutiwa jibu la kitaifa badala ya kutumia njia za kijeshi kwa misingi ya kikabila. Mgogoro wa Rwanda ulioleta mauaji hayo ulianza pale ambapo majeshi ya Kagame yalipoitungua ile ndege ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo wakati huo na kumwua; hivyo badala ya kusaidia kuondoa tofauti baina ya makabila yao, wakakuza sana tofauti hizo. Mpaka sasa wanazidi kukuza tofauti hizo kwa kutumia sherehe hiyo ikiwa ni kama time bomb, kwa kuwa sherehe hizo ni kwa ajili ya kabila moja dhidi ya jingine. South Africa hawana siku za kumbukumbu zinawatofautisha kutokana na uongozi mzuri wa Hayati Mandela. Wana siku moja ya reconciliation day, lakini hawana kumbukumbu za mauaji ya Soweto ya mwaka 1976 au ya Sharpeville ya mwaka 1960 au hata ya kufungwa kwa Mandela mwenyewe. Siyo kwamba wamesahahu matukio hayo ila ni kwa vile kumbukumbu hizo zitaongeza hasira na mtengano baina ya weusi na weupe badala ya kuwaleta pamoja kama taifa moja.

Ninavyoona huko mbele ni kuwa tofauti hizo za kikabila huko Rwanda hazaijaisha na zitarudi tu, tusishangae tena iwapo tutasikia mauaji ya kimbari ya namna hiyo hiyo hiyo kutokea sehemu hiyo hiyo siku za mbeleni. Kagame anatakiwa kuwa mwangalifu sana na jinsi anavyoendesha serikali yake kwa vile hata pale anapokuwa yuko right ni vizuri pia awe anatumia busara sana ku-exercise actions zake. Ameshawafunga kwa madai mepesi sana wapinzani wake kisiasa wakubwa wote wanaotokea katika kabila tofauti ya yeye na hiyo ni kuzidi kujenga tofauti baina ya makabila makuu yaliyomo nchini humo.

Akina Mandela na Nyerere ni wachache sana Afrika hii lakini leo katika dunia yanye teknolojia kubwa ya habari ni vizuri sana kuwa na namna nzuri ya kujenga nchi zetu.
 
suluhu ni kitu cha muhimu sana katika maisha, hautasamehewa kama hausamehi wenzio. maridhiano kwa wanyarwanda ni kitu cha kuwapongeza na kuwatia moyo waendeleze maisha yao yote, kwasababu wangeacha vinyongo mioyoni what would be its end result? si unaona maridhiano yameleta mafanikio na maendeleo? pia nawapongeza kuiweka siku hiyo kama siku maalumu ya kitaifa ili hata watoto wadogo wakue wakielewa nini kilitokea ili kisije kutokea tena. pia, nchi nyingine tukiwaangalia wanyarwanda na siku hiyo maalumu tutajifunza, tutajifunza tusifanye yale waliyofanyiwa watu kipindi cha kimbari. vilevile, tunapojadili tujue hili ni donda kubwa na linalouma sana kwa wanyarwanda, hivyo vile utakavyoongea uongee ukijipima kama wewe ungekuwa kwenye nafasi yao ukaongelewa hivyo ungejisikiaje. tuache roho mbaya.

Nimependa hoja yako lakini sijakuelewa hapo mwishoni unaposema:
"...kama wewe ungekuwa kwenye nafasi yao ukaongelewa hivyo ungejisikiaje. tuache roho mbaya."
Ni wapi kwenye maelezo yangu palipokukwaza nilipowasema vibaya ndugu zetu Wanyarwanda?
 
Seems wengi wenu hapo juu are not good student of History,wanachofanya Rwanda kina tofauti gani na walichofanya Germany for Nazis? huwezi kuachia ideologue za genocide au kusahau victims for the name of reconciliation,na victims lazima wakumbukwe no matter what,the way to move on is to shame waliofanya genocide na kuwakumbuka victims na Histoy ime prove hivyo,in US hata kama una miaka100 leo wakijua uliwahi kufanya kazi na NAZI hata kama ni kufagia ofisi unakuwa deported,Rwanda they are doing the right thing ndio maana wameweza kufika walipofika kwa kipindi kifupi sana
 
Seems wengi wenu hapo juu are not good student of History,wanachofanya Rwanda kina tofauti gani na walichofanya Germany for Nazis? huwezi kuachia ideologue za genocide au kusahau victims for the name of reconciliation,na victims lazima wakumbukwe no matter what,the way to move on is to shame waliofanya genocide na kuwakumbuka victims na Histoy ime prove hivyo,in US hata kama una miaka100 leo wakijua uliwahi kufanya kazi na NAZI hata kama ni kufagia ofisi unakuwa deported,Rwanda they are doing the right thing ndio maana wameweza kufika walipofika kwa kipindi kifupi sana

Issue ya ujerumani haifanani kabisa na issue ya rwanda ndugu. Issue ya ujerumani ilikuwa ni chuki kati ya wajerumani na wageni hasa wayahudi, ambao walikuwa wameshikiria sehemu nyeti za kiuchumi. Na ilikuwa ni baribia europe nzima hawa wayahudi walikuwa wametapakaa.
Issue ya Rwanda ni conflict between 2 tribes talking same language and living in same country. Busara kubwa sana inatakiwa kutumika rwanda ili kuleta amani ya kudumu.
 
Problem ni kwamba tunazungumzia maauaji ambayo anaeadhimisha aliua zaidi kuliko mtuhumiwa,je inatakiwa na Wahutu walioko DRC nao waunde tarehe ya maadhimisho yao? Ama kwa kuwa wao hawakuweza kukusanya mafuvu ya ndugu zao waliouwawa kwenye makambi ya wakimbizi ya Tingi-Tingi refugee camp na Loukolela refugee camp kule DRC? Na pia Wahutu waliouwa kwenye makambi ya Internal Displaced People ndani ya Rwanda
http://www.crimesofwar.org/commentary/two-sides-to-every-story-congo-and-the-rwandan-genocide/
http://www.amnesty.org/fr/library/asset/AFR62/033/1997/fr/e4e7a4b8-e904-11dd-be8c-cfccbdfcd668/afr620331997en.html
 
Problem ni kwamba tunazungumzia maauaji ambayo anaeadhimisha aliua zaidi kuliko mtuhumiwa,je inatakiwa na Wahutu walioko DRC nao waunde tarehe ya maadhimisho yao? Ama kwa kuwa wao hawakuweza kukusanya mafuvu ya ndugu zao waliouwawa kwenye makambi ya wakimbizi ya Tingi-Tingi refugee camp na Loukolela refugee camp kule DRC? Na pia Wahutu waliouwa kwenye makambi ya Internal Displaced People ndani ya Rwanda
http://www.crimesofwar.org/commentary/two-sides-to-every-story-congo-and-the-rwandan-genocide/
http://www.amnesty.org/fr/library/asset/AFR62/033/1997/fr/e4e7a4b8-e904-11dd-be8c-cfccbdfcd668/afr620331997en.html

hayo tayari yanatokea, ukienda kama uingereza na kwingineko wahamiaji wa Rwanda wanaadhimisha genocide tofauti, wahutu kivyao na watutsi kivyao.
 
Back
Top Bottom