dndagula

JF-Expert Member
Jul 24, 2016
1,455
1,439
Kila awamu huacha kumbukumbu zake muhimu wengine hutumia neno "Legacy". Kwangu mimi ninaamini wananchi na Taifa litamkumbuka Rais Dr JPM kwa mambo yafuatayo baada ya muda wake kuisha:

1. Nidhamu maofisini haijawahi kutokea maadili na nidhamu kurejeshwa hivi hata kama bado kuna changamoto ya rushwa maeneo kadhaa.

2. Kuhamishia serikali makao makuu Dodoma na ujenzi wa Ikulu na mji wa serikali. Na uendelezaji wa jiji hilo kwa kasi i.e miundo mbinu barabara na uwanja ndege Msalato etc.Amevunja mwiko ulioshindikana.

3. Kufufua shirika la ndege la ATCL "the national flag bearer".hili lilishindikana huko nyuma.changamoto nyingine zozote za kiuendeshaji za kampuni ni sehemu ya mapambano kama ilivyo biashara yoyote,rada 4 viwanja vya ndege vikuu nk.

4. Daraja la Busisi Kigongo "generational Miracle" ni alama ya kudumu milele.

5. Reli ya SGR ni alama na kumbukumbu kubwa mno.

6. Daraja la Tanzanite na flyovers.

7. Umeme wa Stiglers Gorge JKNHP.

8. Mifumo ya ukusanyaji mapato ya serikali na mageuzi kwenye madini.Haya ni mambo makubwa sana vizazi vitamkumbuka. Yapo mambo mengi ila haya ni kielelezo na alama ya kudumu. Mungu ambariki

Soma pia Hayati Magufuli ameacha legacy ya kuthubutu kufanya kitu bila ya kuomba ruhusa kwanza kwa mfadhili yeyote
 
1. Nidhamu ya woga iliyojengwa katika msingi wa vitisho na wafanyakazi kulia hawajapandishiwa mishahara kwa miaka si kitu cha kujivunia. Kwa kiasi kikubwa huu ni woga na si nidhamu.

2. Wazo zima la kuhamisha makao makuu ya serikali kwenda Dodoma ni wazo la kisiasa lisilo na tija kubwa kiuchumi.

Ni mazingaombwe ya mtu aliyeshindwa kazi ya kuboresha uchumi wa Mtanzania masikini. Ni habari ya mtu aliyeshindwa kufanya kazi ya umuhimu aliyopewa kufanya, akaamua kujitungia kazi nyingine tofauti ambayo hajapewa.

Nyerere nampenda kwa mengi sana. Hususan zama hizi za uongozi mbovu, nikimkumbuka from all those Ikulu parties - my mom used to work in the Nyerere Ikulu, so, I ate some of Miss Wicken's famous apples. That is to say, Nyerere is a personal figure to me, not just a mythical politician- nikimkumbuka na kumsoma, namuona ni political giant.

Lakini, mimi ni mtu wa ideas. Siangalii mtu. Nilikuwa nabishana na mama yangu kuhusu makisa ya Nyerere - she could see no wrong in the man- mpaka naona inataka kuwa ugomvi mbaya. Namtuliza bi mkubwa kisiasa.

And the man knew how to take care of his immediate staff. Very humane gentleman. Something I cannot say for the current occupant.

So, that is the personal context of how Nyerere was held high in my household.

Lakini.

Kwenye kuhamisha makao makuu ya serikali kwenda Dodoma Nyerere alikosea sana.

Alikuwa anatatua tatizo ambalo halipo, katika nchi ambayo ina matatizo mengi sana ambayo yanahitaji utatuzi.

Hakuna Mtanzania aliyelia anataka makao makuu ya serikali yahamie Dodoma.Hii haikuwa kero ya wananchi.

Nyerere alijitungia tu hii habari. Hii habari haina tija kiuchumi. Kwa kweli ni habari ya anasa inayotugharimu tu.

Kwa hivyo, mimi sioni kama ni kitu cha kujivunia.

It is one of the biggest white elephant projects, economically speaking.

Makao makuu ya serikali tayari yalikuwapo Dar. Kulikuwa na haja gani ya kuhamisha kwenda Dodoma?

Muandiahi mmoja- Nafikiri Jenerali Ulimwengu- alisema akikejeli habari hii, na kusema kwamba makao makuu ya serikali ya Tanzania sasa si Dar wala Dodoma. Ni barabara ya kuiunganisha miji miwili hii.

Viongozi mpaka leo wanatumia muda mwingi sana, mafuta mengi sana, allowances nyingi sana, kwa safari za Dar- Dodoma and back.

Ni anasa ya ajabu sana kwa nchi ambayo ina upungufu wa fedha za kigeni.

3 Habari nzima za "national flag bearer" zimepitwa na wakati. Biashara ya ndege ni ngumu sana, inabadilika kwa haraka sana. Na haiendani na dhana nzima ya serikali kujitoa kwenye biashara na kuweka mazingira ya biashara yawe mazuri. Tulishafika pazuri sana na Fastjet, Precision Airlines etc. Hakukuwa na haja ya serikali kujiingizq katika biashara ya ndege yenye risk kubwa na colossal losses.

Again, we are trying to solve non existent problems, while real and existing problems qre not solved!

Ndege zimeanzia Marekani. Kitty Hawk hapo North Carolina ndipo Wright Brothers waliporusha ndege mara ya kwanza duniani mwaka 1903.

David McCullough, muandiahi wangu mmoja mshindi wa nishqninya Pulitzer ninayempenda sana kaandika kitabu kizuri sana kuhusu historia ya ndege ya kwanza kuruka. Kitabu kinaitwa "The Wright Brothers". Nimekisoma. Kitabu kizuri sana kwa wanaotaka kujua historia ya ndege.

Wamarekani wanajua sana biashara.Ila serikqli yao imekataa habari za "national flag carrier". Kwao ukiongelea flag carriers unaongelea US Air Force. Ndege za kijeshi.

Huku kwenye biashara, serikali imejitoa. Inaweka mazingira ya biashara yawe mazuri tu.

Private companies zinashindana.

Unafikiri Wamarekani ni wajinga kufanya hivyo? Serikali ya Marekani haitaki faida kutika biashara ya ndege?

Wanajua biashara hii iko very tricky. Serikali imeiachia sekta binafsi.

Sisi mpaka leo tunatamba na habari za national flag carrier?

Tunaitaka "national flag carrier" kwa ujiko wa kisiasa au ufanisi wa kibiashara?

If it is the former, how much are we ready to throw down a bottomless pit for this foolish extravagance?

If it is the latter, is this avaricious?

Hivi watu wanajua hata ATCL ina operate at what loss or profit? Woth all this Ikulu interference and audit blocks? All these purchases that are totally outside of the open tender process?

Is this something to be proud of as a legacy?

4. Daraja, hata kama lina tija, halidumu milele.

Hapa tunarudi kwenye mjadala wa maendeleo ya vitu na watu. Granted. Tunahitaji madaraja na vitu. Lakini ukiona kiongozi anasifiwa sana kwa kuleta maendeleo ya vitu lakini hana accomplishment kwenye kuendeleza mawazo ya watu, hapi ujue kuna tatizo.

Nyerere hakuleta maendeleo ya vitu sana. Lakini aliwapa watu maendeleo ya watu. Kuna Bibi alizaliwa kabla ya Nyerere (1920), alikuwa mtu wa dini sana. Lakini alisikitika sana kutojua kusoma.

Nyerere alivyoleta habari za "Elimu ya Watu Wazima", huyu Bibi alipata nafasi ya kusoma. Aliweza kusoma Biblia yake mwenyewe bila ya kusaidiwa na mtu. Alisoma barua zake mwenyewe bila ya kusaidiwa na mtu. Hayo yalikuwa maendeleo makubwa.

Kipindi hicho, Tanzania ilikaribia 100% literacy rate.

Karibu kila mtu wa umri wa kujua kusoma alijua kusoma.

Kwa sasa nafikiri tumeshuka kutoka literamacy rate hizo za enzi za Nyerere.

Watu wengi zaidi, kwa asilimia, hawajui kusoma.

Sasa unaweza vipi kuwa na demokrasia na uhuru wa kuchagua katika nchi ambayo watu wasiojua kusoma wanazidi?

Hiki ni kitu cha kujivunia?

Ukiwa na daraja zuri jipya, halafu watu hawajui kusoma alama za darajani, hilo ni jambo la kujivunia?

6. Unarudia madaraja. Inaonekana huna kitu tofauti. Maneno yangu ya hapi juu jibu namba 5 yanahusika hapa pia.

7. Umeme wa Stiglers Gorge utamsaidia vipi mtu asiyeweza kumudu kuununua na serikali ambayo haiko investor friendly kuweza kuleta investors wengi walete ajira na kuutumia vilivyo? Unajua terms za finacing of the projects? Unajua Return on Investment Projections?

8 Mifumo ya ukusanyaji wq mapato iliwekwa tangu enzi za Makapa alipoanzisha TRA. Sioni kipya alichofanya JPM zaidi ya kuiingilia kisiasa na kusababisha TRA iweke unrealistic goals zinazofanya watendaji wake wabambikie watu kodi za juu kabla hata hawajaanza biashara. Na hili matokeo yake ni watu wengi kuona biashara ni ujinga, kwa sababu wanafanya biashara ili walipe kodi, na faida kwao ni ndogo sana.

Watu wanafunga biashara sasa hivi.

Nina rafiki zangu kadhaa wana biashara zao, wanafunga kwa sababu wamebambikiwa kodi za ajabu.

Watu wanauza nyumba zao Mbezi Beach na Mbweni kwa bei za kutupa, kwa sababu wanadaiwa kodi za ajabu na TRA. Na biashara mbaya, watu hawana hela.

Mimi familia yangu ina nyumba ya biashara prime area Dar (Oysterbay). Rent ilikuwa inapanda tu kila renewal. Kwa sasa rent zimeshuka sana. Hata nyumba zetu za Oysterbqy za kupangisha mabalozi wa nje. Wafanyabiashara wanafunga biashara zao.

Etihad is gone. Exxon Mobil is gone. Dangote is gone. So many more global business brands are gone.

Rafiki zangu wawekezaji wa ndani wanafunga biashara.

Hii ndiyo legacy ya Magufuli.

Rais aliyeua biashara Tanzania.
 
1. Nidhamu ya woga iliyojengwa katika msingi wa vitisho na wafanyakazi kulia hawajapandishiwa mishahara kwa miaka si kitu cha kujivunia. Kwa kiasi kikubwa huu ni woga na si nidhamu.
Ametengeneza Taifa la Wanafiki.

Wengi wameona anapenda sifa basi wamejitoa kabisa Ufahamu, wanamsifia hata Kwa mambo ya Kijinga. Imagine Rais wa nchi anasema hadharani sishauriki, na bado mijitu inampongeza Kwa kauli hiyo.

Ameelekeza nguvu nyingi kupambana na adui ambaye hayupo (Wapinzani wake kimtazamo) ilhali adui halisi anazidi kutamalaki, (ujinga, maradhi, Umasikini). Inashangaza hata Mamlaka zinatishia kuwakamata wanaosema kuna Corona Tanzania.

Legacy kuu ya huyu Bwana Mkubwa ni Umungu mtu - anatamani wote tuwaze anavyowaza yeye, anatamani hata tumsujudie, Kinyume na hapo unabatizwa cheo cha "Siyo Mzalendo".. Chuki na Hofu vimeshika hatamu awamu hii. Sad!
 
“Legacy” ya kiongozi ni kile anachokumbukwa kwacho. Kinaweza kuwa kizuri au kibaya. Kwa mfano, Hitler, Stalin, Pol Pot na Mobutu wanakumbukwa sana, lakini kwa mabaya. Legacy zao ni mbaya. Wengi tunakubali kwamba Mahatma Gandhi, Julius Nyerere, Nelson Mandela na Mother Teresa wana legacy nzuri sana. Tuangalie Legacy ya Rais Magufuli sambamba na legacies za Marais wengine wa nchi yetu.

NYERERE: Anakumbukwa sana kujenga umoja wa kitaifa. Anakumbukwa pia kwa siasa ya Ujamaa na Kujitegemea na kuanzisha Vijiji vya Ujamaa.

MWINYI: Huyu kila mtu anamkumbuka kama Mzee Ruksa. Aliokoa jahazi. Nyerere aliacha nchi haina kitu Hazina. Ilibidi Mwinyi akakope kwa Mugabe fedha za kulipia mafuta. Meli iliyafikisha mafuta bandarini lakini ikakataa kuyashusha mpaka malipo kwanza. Haya nimeyasikia mwenyewe kwenye hotuba ya Mwinyi Harare in the nineties.

MKAPA: Mwinyi alikuwa Mzee Ruksa na Mkapa akawa Mzee Uwazi. Miaka mitano ya kwanza ya Mzee Mkapa ilikuwa mizuri sana. Shilingi ilirudisha heshima yake, na nidhamu ilianza kurudi maofisini. Miaka mitano ya mwisho ya utawala wa Mzee Mkapa iligubikwa na uporaji wa mali za uma. Mikataba mibaya ya madini ilipitishwa wakati huo.

KIKWETE: Huyu Rais anakumbukwa kwa safari nyingi. Anakumbukwa pia kwa kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari. Magazeti, redio na TV zilikuwa huru sana wakati wa Rais Kikwete. Yapo mabaya pia yanakumbukwa kutokea kipindi hiki. Yaliyowasibu Ulimboka, Dr. Mvungi na Alphonce Mawazo ni sehemu ya Legacy ya Mzee Kikwete. Sio lazima awe ametenda yeye lakini it happened during his watch.

MAGUFULI: Ujenzi wa reli ya kisasa, bwawa kubwa la kuzalisha umeme, kuadimika kwa fedha mitaani na ubabe wa kupitiliza ni sehemu ya legacy ya Rais Magufuli. Kuna mazuri na mabaya kwenye huu ubabe. Kuna miradi kama ujenzi wa hospitali na zahanati na kutatua matatizo sugu ya maji sehemu nyingi ambayo ilikuwa inakwenda kwa utani wa Kiswahili, lakini sio kwa huyu Mzee. “Hapa kazi tu” ni sehemu ya legacy yake. Kupotea kwa baadhi ya watu, na Polisi kubambikizia watu makosa makubwa ya kutisha ni sehemu pia ya legacy ya Rais wa sasa. Kwa kifupi legacy ya Magufuli hadi sasa ni “hapa kazi tu”, “sijaribiwi” na demokrasia sitaki.
 
Tundu Lissu, Lema na Chadema kwa ujumla mkitaka kuuwa legacy ya hayati rais Magufuli kwa watanzania itabidi ufanye yafuatayo.

Unapokula kichwa mradi wa umeme kutoka bwawa la Nyerere ambao umefikia 50% itabidi watuambie umeme tutatoa wapi?

Unapokula kichwa serikali kuhamia Dodoma na kusema ni hasara itabidi wajieleze.

Unapokula kichwa reli ya kisasa ambayo inakaribia Makutupora itabidi wajieleze kwa watanzania hiyo Tanzania ya viwanda itawexekana vipi.

Unapokula kichwa ujenzi wa meli mpya kwenye maziwa makuu itabidi watueleze watatusafirisha na nini?

Wanapokula kichwa ndege zetu itabidi tuwawekee video za kina Heche, Lema, Lissu wakitukana serikali iliyoshindwa kununua ndege.

Watakaposema wachimbaji wadogo, bodaboda na mama ntilie wafukuzwe itabidi watueleze wanafanya haya kwa faida ya nani?

Watakapoamua zahanati na hospitali zote zilizojengwa na Magufuli zifungwe, itabidi watueleze tutaenda kutibiwa wapi?

Watakaposema wamefuta elimu bure itabidi watueleze kodi zetu zinafanya kazi gani?

Watakaposema lazima Watanzania millioni 60 wachanjwe, itabidi watueleze wao mpaka sasa

Hawajachanjwa
Nyungu hawajapiga
Hawajajifungia ndani wanaenda kazini kila siku
Mbona hawajafa na corona sasa?

Watakaohoji haya maelezo siyo Magufuli wala watoto wa Magufuli ni Watanzania.

Anayedhani itakuwa rahisi kuuwa legacy ya Magufuli atakutana na nguvu ya uma.

Muda utaongea.
 
Hivi mbona legacy ya Nyerer hakuna anayeahangaika hivi kuitetea iendelee kuwepo? WHY huyu?
Si ndio nyie mnaojidanganya kwamba akifa mtu na legacy yake anakufa nayo? Watu wa aina yako mlijitahidi kumfuta Nyerere wee na nia yake ya kujenga nchi huru inayojitegemea, lakini wapi. Ndio maana tunasema msifurahi kupita kiasi, kufa kwa JPM si kufa kwa spirit au legacy yake.
 
Hivi unajua hakuna aliyeijenga nchi hii kama mjerumani.legacy yake iko wapi

Hivi unajua kaburu alivyoijenga South Afrika au hujui

Hayo madude yamejengwa kwa damu na machozi ya Watanzania

Baya moja hufuta mazuri 100
Nakwambia haitakuwa rahisi.
 
Si ndio nyie mnaojidanganya kwamba akifa mtu na legacy yake anakufa nayo? Watu wa aina yako mlijitahidi kumfuta Nyerere wee na nia yake ya kujenga nchi huru inayojitegemea, lakini wapi. Ndio maana tunasema msifurahi kupita kiasi, kufa kwa JPM si kufa kwa spirit au legacy yake.
Tundu Lissu alijaribu kutukana legacy ya Nyerere akakutana na nguvu ya uma.

Hatokaa arudie tena.
 
Back
Top Bottom