Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,339
- 51,883
KUMBUKA; VIUMBE HATARI HUPENDA KUJIFICHA.
Anaandika, Robert Heriel.
Moja ya sifa kuu ya kiumbe hatari ni kupendelea kujificha, kukaa mafichoni, kukaa chobingo.
Hawapendi kujianika Anika hovyo, kujidhihirisha hovyo.
Kwanza weka akilini kuwa Kiumbe hatari hujijua kuwa yeye ni hatari, tena hujijua yeye ni mbaya asiyehitaji mchezo.
Nyoka, Nge, Tandu, buibui wang'atao ni miongoni mwa wadudu hatari kubwa, hawa hupenda kukaa mafichoni.
Na hata akiingia ndani ya nyumba yako hawezi pita sehemu wazi inayoonekana, lazima atembee na laini ya ukuta chini ili akitembea usimuone.
Viumbe hatari na Wabaya hupendelea giza katika harakati zao. Kwao nuru ni adui mkubwa.
Ukienda Mbugani ni ngumu Sana kuwaona Wanyama hatari, kama vile Chui, Simba, chatu, Koboko, Cobra, n.k.
Saikolojia ya viumbe hatari ni kutokuwa na Imani na yeyote. Muda wote wako machomacho, kujihami, n.k. pia viumbe hatari hupendelea Ambush, naam ndio shambulizi la kushtukiza.
Katika Maisha wapo watu hatari, na watu hatari siku zote wanatabia hizohizo.
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Anaandika, Robert Heriel.
Moja ya sifa kuu ya kiumbe hatari ni kupendelea kujificha, kukaa mafichoni, kukaa chobingo.
Hawapendi kujianika Anika hovyo, kujidhihirisha hovyo.
Kwanza weka akilini kuwa Kiumbe hatari hujijua kuwa yeye ni hatari, tena hujijua yeye ni mbaya asiyehitaji mchezo.
Nyoka, Nge, Tandu, buibui wang'atao ni miongoni mwa wadudu hatari kubwa, hawa hupenda kukaa mafichoni.
Na hata akiingia ndani ya nyumba yako hawezi pita sehemu wazi inayoonekana, lazima atembee na laini ya ukuta chini ili akitembea usimuone.
Viumbe hatari na Wabaya hupendelea giza katika harakati zao. Kwao nuru ni adui mkubwa.
Ukienda Mbugani ni ngumu Sana kuwaona Wanyama hatari, kama vile Chui, Simba, chatu, Koboko, Cobra, n.k.
Saikolojia ya viumbe hatari ni kutokuwa na Imani na yeyote. Muda wote wako machomacho, kujihami, n.k. pia viumbe hatari hupendelea Ambush, naam ndio shambulizi la kushtukiza.
Katika Maisha wapo watu hatari, na watu hatari siku zote wanatabia hizohizo.
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam