Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,606
- 20,347
Baada ya tabiri zake mbili za hivi karibuni kuhusu uchaguzi kuonekana ni za uongo, yule mnajimu ameanza kutapatapa. Kwanza alitabiri kutokuwepo kwa uchaguzi mwaka huu 2010, pili akatabiri kifo cha mgombea maarufu wa urais kabla ya uchaguzi. Yote hayakutokea.
Humu JF tuliwahi kuandika kwa mzaha tu kuwa lazima jamaa atahusisha kifo cha kocha Syllesaid Mziray na mgombea urais Kuga Peter Mziray. Post hiyo iko HAPA.
Na kweli imetokea hivyo, nimesoma katika gazeti moja la udaku eti mnajimu anasema kocha Mziray aliingilia nyota ya mgombea urais Mziray. Nadhani huyu jamaa aliisoma ile post, ila naona wahusika wa hayo majina wamchukulie hatua ili aache kabisa kutabiri.
Humu JF tuliwahi kuandika kwa mzaha tu kuwa lazima jamaa atahusisha kifo cha kocha Syllesaid Mziray na mgombea urais Kuga Peter Mziray. Post hiyo iko HAPA.
Na kweli imetokea hivyo, nimesoma katika gazeti moja la udaku eti mnajimu anasema kocha Mziray aliingilia nyota ya mgombea urais Mziray. Nadhani huyu jamaa aliisoma ile post, ila naona wahusika wa hayo majina wamchukulie hatua ili aache kabisa kutabiri.