Gudboy
JF-Expert Member
- Aug 14, 2009
- 867
- 77
Jana nilikua nimelala, nakumbuka ilikua usiku wa manane nikaishiwa na usingizi. Mara nyingi huwa nawacha radio ikiimba hadi asubuhi. Niliposhtuka nikasikia kipindi kilikua kinaendelea cha Brother Chiko mtangazaji wa Magic fm (hii ndio radio niipendayo) akiendesha kipindi chake cha malavidavi. Pale studio alikua na mgeni ambaye alikua anaelezea maswala ya mapenzi. Kitu ambacho kilinivutia ni pale yule mgeni aliposema watu wengi huwa wanapenda kupima mapenzi. Akatoa mfano: Unaweza kuwa na mpenzi wako mmekaa miaka hata zaidi ya 3, lakini akapata mpenzi mpya lakini akiendelea na wewe pia, sasa atacompare nani anampenda sana, mathalani kujali, nani analeta zawadi, nani anamusms wakati wa kulala then ndio ataamua amchague yupo.
Wadau wa JF mimi sina experience sana na hili swala, Je kuna ukweli wowote? Naombeni mawazo yenu
Wadau wa JF mimi sina experience sana na hili swala, Je kuna ukweli wowote? Naombeni mawazo yenu