Kumbe wale wanaotaka order ya kiti moto kilo 1.5 na ugali huwa wanapanua utumbo tu

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
1638254993404.png

Huyu Mzee mwaka 1550 alijiona anachoka sana, Aliangalia chakula anachokula na kukipunguza kufikia 350g na 414 mls za wine kwa siku.

Kwa hesabu za haraka haraka alikula yai moja asubuhi kama kifungua kinywa.

Kipande cha nyama, kuku au samaki saa kumi jioni kikiwa na kiazi na mboga. Ukubwa wa kopo la Coca Cola aliweka wine. Maji ni muhimu hapa kati kati.

Tunakula vyakula vingi tusivyo vihitaji. Wakati wa WWII, wanajeshi wa Magharibi waliotekwa Japan walilishwa kibakuli cha wali na kipande cha nyama kila baada ya masaa 24. Wengi waliishi mpaka kurudi makwao wakiwa wamekonda sana.

Iliwachukua zaidi ya mwezi kuzoea milo mitatu kwa siku.
 
Hii ni kweli, kula sana sio afya.

Binafsi nilishawahi kaa siku nne nakunywa chai kavu na maji mengi.

Maji ni muhimu sana.
Kuna mama mzungu ali muasili mtoto wa Kitanzania, ilimchukua muda mtoto kuzoea kiasi cha chakula kwenye sahani yake.

Alimfahamisha sababu ya kila walichofanya. Alimwambia nyama ni chanzo cha kuongeza damu mwilini lakini si vizuri kula nyama kila siku.

Nyama ilikua ni Jumapili na J5 lunch na jioni kipande cha mkate, salad na mayai mawili ya kuchemsha.
 
Kulaaa msosi wa kiafrika.

Tena kula vizuri tu vyakula vya asili. Si lazima tufate wazungu. Piga ugali mchicha pilipili mixer maharage na shushia na maji kisha kafanye kazi.

Kama huna kazi ngumu chukua mkeo mshughulikie mpaka atake kukurudishia mahari akulipie yeye.

TUSIENDEKEZE SANA UZUNGU SISI NI WASWAHILI.
 
Back
Top Bottom