Kumbe wale wanaofanya siasa za upinzani mitandaoni ni wengine na Wapinzani Wanasiasa halisi ni wengine!

mtoto wa mchungaji

JF-Expert Member
Oct 24, 2020
279
480
Kuna vitu hapo awali nilikuwa sielewi kabisa, kuna wakati wanasiasa halisia walikuwa wanakosea kabisa na hata mtoto ukimuuliza anakwambia kuwa hilo ni kosa lakini wanasiasa wa mtandao walikuwa wanalipongeza sana.

Wakati mwingine uliweza kuona hali ya siasa za upinzani zinapita katika shida na kipindi kigumu mno, lakini hawa wanasiasa wa mitandao wanasema hali ni nzuri na tunachukua nchi mapema asubuhi.

Kuna kipindi nakumbuka hali ilikuwa mbaya sana ktk upinzani watanzania wote walikuwa wanajua uwe CCM au upinzani, unaona kabisa hapa ni kama wamewekewa goti shingoni kama Joji Floidi lakini ukiingia katika wanasisa wa mitandao wanasema chama kinaimarika kwa kasi ya ajabu.

Angalia leo katika uhalisia wa siasa halisi Tanzania upinzani ni kama haupo kwani nchi nzima kati ya wabunge zaidi ya 300 wa kuchaguliwa wapinzani wamepata wabunge ambao hawazidi 3.

Kinachonishangaza mimi huku kwa wanasiasa wa mtandao ukiangalia wanavyoandika ni kama CCM ina wabunge 3 na wapinzani wana wabunge zaidi ya 300.

Jamani hivi hii imekaaje? Mimi naona kama kuna tatizo. Mimi nasema kama kuna components nyingine zilizosababisha kuua upinzani basi hii ya taarifa za kupotosha zitakuwa zimechangia sana kuua upinzani Tanzania kwasababu watu wa siasa za mtandao ni kama vile hali ya mgonjwa ni mbaya anakaribia kufa wenyewe wanasema mgonjwa afya yake inazidi kuimarika kwa kasi ghafla tunasikia mgonjwa kafa.

Je, kulikuwa na mahusiano ya moja kwa moja kati ya wanasiasa wa halisia na hawa wa mitandaoni au ni makundi mawili tofauti kwasababu inashangaza.

Hebu nisaidieni mimi mkusanya sadaka sielewi kitu hapo.

Mtoto wa mchungaji.
 
Kuna vitu hapo awali nilikuwa sielewi kabisa, kuna wakati wanasiasa halisia walikuwa wanakosea kabisa na hata mtoto ukimuuliza anakwambia kuwa hilo ni kosa lakini wanasiasa wa mtandao walikuwa wanalipongeza sana...
Wanasiasa wa mitandaoni ndiyo wanasiasa Halisia ndiyo wakosoaji wazuri wa mapungufu ya CCM uonevu unyanyasaji uovu mateso ufisadi wote wa CCM bila kumung’unya maneno, mfano sasa kipindi hiki demokrasia haipo live hakuna mikutano ya siasa wengi wakitaka kujua madhaifu madhambi ya CCM huingia mitandaoni na hasa JF makao makuu ya utandawazi ukweli na uwazi
 
MWAMBIENI LISU ATUPE MAPATO NA MATUMIZI YA ZILE CHANGIZO KIPINDI CHA KAMPENII. ASITUSAHAULISHE.
Anza na polepole huko CCM kwanza mlipoyapaka Rangi magari ya Serikali magari ya walipa kodi mkayageuza kuwa mali binafsi ya CCM, mapato tokea China michango ya matajiri wa kihindi kiarabu na weusi wenzetu wote zipo wapi chenchi?
 
Ungekuwa na akili timamu kabla ya utopolo mwingine ulipaswa kujiuliza ilikuwaje ccm ikapata idadi hiyo ya wabunge , maana dunia nzima inajua
Hakuna uchaguzi Tanzania kilichofanyika ni CCM kuulawiti kuubaka kuunajisi uchaguzi mkuu kwa njia haramu za kishetani tu
 
Nchi ina zaidi ya miaka 59 hakuna maendeleo licha ya kuwa na rasilimali nyingi kuliko mataifa mengi Duniani, CCM hawataki maendeleo walitumia nguvu kubwa kuwashawishi wananchi kuweka pesa Benk kuziamini Benk lakini sasa utawala wa CCM umeivuruga imani kwa Benk huenda zikafirisika kwa kukosa wateja hususani wafanyabiashara wakubwa baada ya TRA kuanza Tabia mbovu na mbaya mno.

kwenda kufunga Account zao kufunga biashara zao kuwabambikia kodi kubwa kwa njia haramu za kishetani kutengeneza mazingira ya Rushwa na pia kuwakomoa hasa wale ambao hawakuichangia CCM kipindi cha kampeni, ni wanasiasa wa mitandaoni huibua haya maovu tu lakini wanasiasa wa mitaani wanufaika wa uonevu wa CCM kamwe hutawasikia wakikemea haya maovu.
 
Pesa nyingi za walipa kodi hutumika kudidimiza demokrasia kuwabambikia kesi uonevu unyanyasaji mateso kwa wapinzani badala ya maendeleo ni vigumu Nchi kupiga hatua katika mfumo huu kandamizi
 
Ungekuwa na akili timamu kabla ya utopolo mwingine ulipaswa kujiuliza ilikuwaje ccm ikapata idadi hiyo ya wabunge , maana dunia nzima inajua
Ndo Kama wewe mwanasiasa wa mtandaoni anaosema mna tofauti na wanasiasa halisi mnasema tundu atachukua nchi asubuhi na mapema.
 
Upinzani halisi upo kwenye mioyo ya watu, hicho unachokiona kuwa CCM Wana wabunge wengi Ni nguvu za Dola. Hakuna mahali watu Wana shida kukusanya watu Kama ilivyo kwa viongozi wa CCM.
 
Anza na polepole huko CCM kwanza mlipoyapaka Rangi magari ya Serikali magari ya walipa kodi mkayageuza kuwa mali binafsi ya CCM, mapato tokea China michango ya matajiri wa kihindi kiarabu na weusi wenzetu wote zipo wapi chenchi?
Tunaomba mtuelezee na kutuonesha mapato na matumizi ya zile sadaka mlizokusanya kwenye zile ndooo nyeupee, usihamishe magolii.
 
Akili yako ingekuwa inafanya kazi vizuri ungejiuliza kwanini upinzani bungeni haupo lakini kwenye mitandao umejaa tele?

Kuamini upinzani umekufa wakati wewe mwenyewe unakiri umejaa mitandaoni, tena zaidi unakubali wapinzani wa mitandaoni wengi wao sio viongozi, kwangu mimi huo ndio utajiri wa upinzani.

Wakati wa kampeni hukuona Lissu alivyowapeleka mbio CCM? mtoto wa mchungaji mambo ya siasa huyajui, endelea tu kuwaibia waumini sadaka.

Kama sio kwa hisani ya NEC na jeshi la polisi, hali halisi ingetakiwa iwe wapinzani wana wabunge 300 na CCM ina wabunge wawili.
 
Kuna vitu hapo awali nilikuwa sielewi kabisa, kuna wakati wanasiasa halisia walikuwa wanakosea kabisa na hata mtoto ukimuuliza anakwambia kuwa hilo ni kosa lakini wanasiasa wa mtandao walikuwa wanalipongeza sana...
Toka mmepora haki ya watanzania ya kuchagua ni miezi miwili karibu na nusu. Hakuna la maana mnalofanya zaidi ya kusimamishana/kutumbuana wenyewe kwa wenyewe na kuweweseka na upinzani ambao mlikuwa mnasemaunawachelewesha kuleta maendeleo.
 
Jamani mimi nashauli tuchange mada zangu kwa upendo na c kutukana matusi biblia inafundisha kuonyana kwa zaburi maana mtu akinitusi nitamwachia laana.
Kujadili mambo ya nchi yetu ni ya wote lakini swala la ukusanyaji wa sadaka hili si la wote.
Nashukuru kwa tunaoshambuliana kwa hoja inaleta kujifunza zaidi
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom