Kumbe Viongozi, Wasanii na Wanasiasa ndiyo waliopaswa kwenda Hospitali ya Vichaa Mirembe-Dodoma

Civilian Coin

JF-Expert Member
Dec 2, 2012
2,305
4,334
Sasa nimeamini Vichaa waliopo Hospitali ya Mirembe ni FAKE INSANE na VIONGOZI na WANASIASA na WASANII ndio VICHAA kabisa. Hao ndio walipaswa kwenda Hospitali ya Mirembe.

1. Sheria za Nchi zimekuwa zikipindishwa bila sababu yoyote.

2. Askari wakitisha watu kisa UASKARI wao.

3. Mafisadi wanafungwa Miezi 6, Wala hoi miaka 5 kwa wizi wa kuku.

4. Matokeo ya Chaguzi kupindishwa.

5. Viongozi kutumia Mamlaka kukamatwa watu wenye akili kuliko wao.

6. Majambazi kupewa nafasi za upendeleo za Kiuongozi.

7. Mauaji na majeruhi kipindi Cha Uchaguzi.

8. Watu kuwekwa Vikwazo bila sababu yoyote.

9. Kutaifisha wake za watu na kuua Waume Zao na mipango yao inapokwama wanarudisha Makapi Yao kwa nguvu.

10.Heshima imeshuka yaani Askari anasubiri kutumwa kumkamata Don Nalimison huku anajua DON ni MHESHIMIWA Kama Mawaziri na ana sifa za kuwa Rais.

11. Taarifa za Madaktari kwa wagonjwa nyingi ni Batili na wagonjwa hawapati huduma sitahiki.

12. Dharau nyingi zisizo kuwa na maana kisa madaraja na madaraka.

13. Uongo mwingi usiokuwa na maana Yani maisha ya Watanzania yanageuzwa Vichekesho.

14. Hata VICHAA wanateuliwa vyeo, na wasio VICHAA wanabambikwa Ukichaa.

15. Taifa limekuwa lakulazimisha Mapenzi huku Sheria inasema mapenzi ni hiari.

16. Taifa limekuwa Taifa la Utaifishaji Mali na watoto wa watu wasio kuwa na hatia. Na jamii iko kimya.

Track yangu "INNOCENT" iko njiani inakuja.
Itaendelea baada ya Uchaguzi.

DON NALIMISON.

Screenshot_20200827-191047.png
 
Back
Top Bottom