EINSTEIN112
JF-Expert Member
- Oct 26, 2018
- 21,713
- 35,524
Kikosi cha Wanaanga cha Urusi kilianzisha shambulizi la anga la "usahihi wa hali ya juu" dhidi ya hifadhi za ndege za Ukraine zilizokuwa na silaha na risasi katika eneo la kati la Poltava siku ya Jumatatu, Wizara ya Ulinzi ya Urusi ilisema jana (Jumanne).
Kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya Urusi, shambulizi hilo lililolenga silaha zilizotolewa na Marekani na nchi za Ulaya, lilitekelezwa kwa silaha za usahihi wa hali ya juu za vikosi vya anga vya Urusi na makombora ya Kalibr. Shambulizi hilo liliharibu silaha na zana zilizotengenezwa Magharibi ambazo zingewasilishwa kwa wanajeshi wa Ukraine huko Donbass, iliongeza.
"Ulipuaji wa risasi zilizohifadhiwa ulisababisha moto katika kituo cha ununuzi kisichofanya kazi karibu na vifaa vya mtambo huo," wizara ilisema. Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alisema kwenye Telegram kwamba shambulizi hilo liligonga jumba la maduka liliokuwa na zaidi ya watu 1,000 ndani.
Kwa mujibu wa Wizara ya Ulinzi ya Urusi, shambulizi hilo lililolenga silaha zilizotolewa na Marekani na nchi za Ulaya, lilitekelezwa kwa silaha za usahihi wa hali ya juu za vikosi vya anga vya Urusi na makombora ya Kalibr. Shambulizi hilo liliharibu silaha na zana zilizotengenezwa Magharibi ambazo zingewasilishwa kwa wanajeshi wa Ukraine huko Donbass, iliongeza.
"Ulipuaji wa risasi zilizohifadhiwa ulisababisha moto katika kituo cha ununuzi kisichofanya kazi karibu na vifaa vya mtambo huo," wizara ilisema. Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky alisema kwenye Telegram kwamba shambulizi hilo liligonga jumba la maduka liliokuwa na zaidi ya watu 1,000 ndani.