Kumbe umasikini wa pesa hapa kwetu ni kama nusu maiti

mulwanaka

JF-Expert Member
Feb 19, 2017
5,262
12,835
Ndugu zangu tutafuteni pesa tuacha kuendekeza uchawi udini uliozidi na wanawake, jamii zetu hazituthamini tukiwa masikini wanakuona kama nusu maiti kisa huna kitu

MwanaJF moja kasema eti Wabongo buana ni wanafiki sana yaani mwenye fweza hata akijamba ndani ya kikao watamtengenezea sentensi nzuri kwamba huyu anatatizo la kuumwa tumbo toka jana kwa hiyo tumvumilie wanafamilia watajibu ''haina shida tuendele na mambo mengine hilo tuliache mbona kawaida tu''

Wanaogopa hata kuziba pua japo kishuzi kinanuka mno wanahisi wataonekana wamemdharau jamaa

Sasa jamba wewe maskini utasemwa wewe mpaka utatamani uchukue kitanzi ukajinyonge.hayo ni kawaida hapa kwetu Afrika.

Mimi siko tayari kurudi nyumbani bila pesa bora nifie huku huku nikiwa natafuta kuliko kurudi nyumbani wanidhihaki kama half dead

Ukienda hospitali mateso demu unayepata wa hovyo huwezi kushinda kesi nk.

Kwa hiyo bora nifie huku trying kuliko kuishi nyumbani kama nusu mtu
 
Hata kanisani mwenye hela anakua recognized mapema sana anapewa mic anatema pumba tu...wasali wenyewe!...
Soma biblia yako, Kuna nafasi katika ulimwengu wa kiroho Mungu anakuweka, endapo utakua na uchumi fulani au wadhifa fulani mkubwa katika jamii.

Remember kua kwa Mungu upo utajir wa kutosha tu, ukijua mbinu zitokazo kwake na kuzitumia.
 
Tieni bidii tafuteni hiyo kitu inaitwa
Doo, Njukuri, Mawe, Peni, Dola, Mpunga Dilham, Kyente, Vyente...
heshima zote zinaanziaga hapo.....
kama ww ni mbishi jaribu kuishi bila pesa...
uone mfano wa jehanam
 
Ni kweli kabisa, ila mentality hii imewafanya wengi kuwa na kisasi.
 
Ndugu zangu tutafuteni pesa tuacha kuendekeza uchawi udini uliozidi na wanawake, jamii zetu hazituthamini tukiwa masikini wanakuona kama nusu maiti kisa huna kitu

MwanaJF moja kasema eti Wabongo buana ni wanafiki sana yaani mwenye fweza hata akijamba ndani ya kikao watamtengenezea sentensi nzuri kwamba huyu anatatizo la kuumwa tumbo toka jana kwa hiyo tumvumilie wanafamilia watajibu ''haina shida tuendele na mambo mengine hilo tuliache mbona kawaida tu''

Wanaogopa hata kuziba pua japo kishuzi kinanuka mno wanahisi wataonekana wamemdharau jamaa

Sasa jamba wewe maskini utasemwa wewe mpaka utatamani uchukue kitanzi ukajinyonge.hayo ni kawaida hapa kwetu Afrika.

Mimi siko tayari kurudi nyumbani bila pesa bora nifie huku huku nikiwa natafuta kuliko kurudi nyumbani wanidhihaki kama half dead

Ukienda hospitali mateso demu unayepata wa hovyo huwezi kushinda kesi nk.

Kwa hiyo bora nifie huku trying kuliko kuishi nyumbani kama nusu mtu
let's meet at the top, cheers 🥂
 
Katika dunia ya leo, kukosa pesa ni kosa kubwa sana. Bila pesa wewe ni nani, huenda hata utu wako ukatiliwa mashaka, nafasi yako katika jamii ikashushwa, katika kufanya maamuzi ukaonekana sio kitu, sio lolote.

Tuzitafute tu!
 
Ndugu wakishagundua una vipesa, hata kama ni ki-mshahara tu umeunga unga ukununua kigari, simu za mizinga na lawama kibao zinaanza. Utaambiwa wewe ni tajiri umenunua ndinga na unajenga nyumba huwezi kukosa pesa labda pesa zote unapeleka ukweni, unaishia kushangaa kama kumiliki gari na kujenga nyumba ndo utajiri basi tutakuwa na matajiri wengi sana...
 
Back
Top Bottom