mechard Rwizile
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 1,571
- 873
Nilijua kuwa taasisi ya urais ni baraza la mawaziri, kumbe wale wote ni vibarua, taasisi nzima ni rais na makamu wake. Kwa tafsiri hii ya Rais aliyoitoa jana, kuna kila sababu kuanzisha mchakato wa katiba mpya ili kuondokana na maisha ya taifa kuwa mikononi mwa watu wawili.
Kuanzia jana, ile dhana ya "washauri wa rais wanampotosha" haina mashiko tena. Kosa likitendwa kwenye Halmashauri ya wilaya fulani, taarifa itolewe kwa rais naye alitolee mwelekeo.
Nyerere bwana, ndio maana baadhi wanatamani awe mtakatifu, ni kwa sababu kama hizi, hakutaka nchi iongozwe na mtu, alitaka iongozwe na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hakika majuto ni mjukuu
Kuanzia jana, ile dhana ya "washauri wa rais wanampotosha" haina mashiko tena. Kosa likitendwa kwenye Halmashauri ya wilaya fulani, taarifa itolewe kwa rais naye alitolee mwelekeo.
Nyerere bwana, ndio maana baadhi wanatamani awe mtakatifu, ni kwa sababu kama hizi, hakutaka nchi iongozwe na mtu, alitaka iongozwe na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hakika majuto ni mjukuu