Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Kwa mujibu wa ibara ya 63(2) ya katiba ya jamhuri wa muungano wa Tanzania bunge ndicho chombo kikuu chenye madaraka ya kuisimamia serikali kwa niaba ya wananchi.
Kwa mantiki hiyo, chombo hicho kama taasisi na mojawapo wa muhimili wa dola kinapashwa kiwe na mwenendo ambao haautiliwi mashaka na wananchi kinao wawakilisha. Katika siku za hivi karibuni zimetolewa shutuma nzito dhidi ya bunge hilo, tena kutoka kwa wabunge wenyewe, zinazobainisha kwamba wabunge wa bunge hilo wanalipwa mara mbili (na wakati mwingine zaidi) kwa kazi ile ile. Kwa mtizamo wa haraka haraka, inaonekana bunge letu limekula njama na serikali ili kuwaibia wananchi
Kwa kufanya hivyo bunge hilo limefungua mlango kwa wizi mkubwa zaidi. Kwani naambiwa ya kwamba hata watendaji wanapofanya vikao vyao vya ndani ambavyo ni sehemu ya kazi yao wana lipana posho. Siyo hiyo tu, hata mawaziri wanaofikia kwenye nyumba za serikali wanapokuwa huko Dodoma kwaajili ya bunge hulipwa posho ya kujikimu.
Kuna wengine wamekwenda mbali zaidi na kudai kwamba hata viongozi wa kitaifa hulipwa posho ya kujikimu wanapokuwa ziarani huko mikoani, wakati wanafikia ikulu ndogo ambapo kila kitu hulipiwa. Kwa kuzingatia uzito wa suala hili haikutegemewa hata kidogo, kwa spika wa bunge linalotuhumiwa kushindwa kutekeleza wajibu wake kutokana na mgongano wa maslahi kutoa majibu mepesi kwa tatizo hilo zito.
Hii imenifanya niamini ya kuwa spika huyo hataweza kuimudu vizuri nafasi aliyonayo kwakuwa upeo wake wakutafakari mambo ni mdogo sana.
Kwa mantiki hiyo, chombo hicho kama taasisi na mojawapo wa muhimili wa dola kinapashwa kiwe na mwenendo ambao haautiliwi mashaka na wananchi kinao wawakilisha. Katika siku za hivi karibuni zimetolewa shutuma nzito dhidi ya bunge hilo, tena kutoka kwa wabunge wenyewe, zinazobainisha kwamba wabunge wa bunge hilo wanalipwa mara mbili (na wakati mwingine zaidi) kwa kazi ile ile. Kwa mtizamo wa haraka haraka, inaonekana bunge letu limekula njama na serikali ili kuwaibia wananchi
Kwa kufanya hivyo bunge hilo limefungua mlango kwa wizi mkubwa zaidi. Kwani naambiwa ya kwamba hata watendaji wanapofanya vikao vyao vya ndani ambavyo ni sehemu ya kazi yao wana lipana posho. Siyo hiyo tu, hata mawaziri wanaofikia kwenye nyumba za serikali wanapokuwa huko Dodoma kwaajili ya bunge hulipwa posho ya kujikimu.
Kuna wengine wamekwenda mbali zaidi na kudai kwamba hata viongozi wa kitaifa hulipwa posho ya kujikimu wanapokuwa ziarani huko mikoani, wakati wanafikia ikulu ndogo ambapo kila kitu hulipiwa. Kwa kuzingatia uzito wa suala hili haikutegemewa hata kidogo, kwa spika wa bunge linalotuhumiwa kushindwa kutekeleza wajibu wake kutokana na mgongano wa maslahi kutoa majibu mepesi kwa tatizo hilo zito.
Hii imenifanya niamini ya kuwa spika huyo hataweza kuimudu vizuri nafasi aliyonayo kwakuwa upeo wake wakutafakari mambo ni mdogo sana.