KUMBE SILAHA ZA MAREKANI HAZINA UJANJA KWA ZILE ZA URUSI.

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,651
18,021
Kitendo cha Uturuki kuamua kuanza kupokea makombora ya s-400 ya Urusi, kimemfanya Marekani akiri hadharani hofu yake kuwa silaha za Urusi zikiwa karibu na zile ndege zake za F-35 ambazo Uturuki pia alishazilipia, kutasababisha udhaifu wa zile ndege kugundulika!!!! Sasa najiuliza kwa nini asingesema tutagundua udhaifu wa zile S-400 Russian anti-missile defence system. Hii inaonyesha Marekani hajiamini kabisa kwa silaha zake, na ameamua kutokuziachia ziende Uturuki kwa hofu siri ya udhaifu wake itagundulika. Hii imedhihirisha kuwa Marekani anafahamu kuwa ndege zake zina udhaifu mkubwa na anawauzia "marafiki" zake kwa bei kubwa sana hiku akijua ni kama toy fulani vile!!! Marekani ni vitisho tu lakini mbele ya silaha za mbabe wa ukweli analia lia mpaka anatia huruma. Msikilize anaposema hapa BBC: The officials said they did not want the F-35 jets to be near S-400 systems because they feared Russian technicians would be able to access the F-35's vulnerabilities.
Mimi ningedhani Marekani angefurahia mshirika wa NATO kuwa na silaha za Urusi ili iwe rahisi kwake kuchunguza udhaifu wake>.
 
Urusi yuko vizuri kwenye Techinolojia ya Siraha.
Kuanzia Ndege za kivita, Nyambizi, Makombola, Meli za kivita, vifaru, Mitambo ya Ulinzi na kadhalika.

Ukitaja Top 5 ya either Vifaru, Helicopta, ndege, Meli, nyambizi, makombola na mitambo ya Ulinzi basi humukosi Murusi kwenye top 5 tena saa zingine akiwa na na mitambo miwili kwenye top 5
 
Kitendo cha Uturuki kuamua kuanza kupokea makombora ya s-400 ya Urusi, kimemfanya Marekani akiri hadharani hofu yake kuwa silaha za Urusi zikiwa karibu na zile ndege zake za F-35 ambazo Uturuki pia alishazilipia, kutasababisha udhaifu wa zile ndege kugundulika!!!! Sasa najiuliza kwa nini asingesema tutagundua udhaifu wa zile S-400 Russian anti-missile defence system. Hii inaonyesha Marekani hajiamini kabisa kwa silaha zake, na ameamua kutokuziachia ziende Uturuki kwa hofu siri ya udhaifu wake itagundulika. Hii imedhihirisha kuwa Marekani anafahamu kuwa ndege zake zina udhaifu mkubwa na anawauzia "marafiki" zake kwa bei kubwa sana hiku akijua ni kama toy fulani vile!!! Marekani ni vitisho tu lakini mbele ya silaha za mbabe wa ukweli analia lia mpaka anatia huruma. Msikilize anaposema hapa BBC: The officials said they did not want the F-35 jets to be near S-400 systems because they feared Russian technicians would be able to access the F-35's vulnerabilities.
Mimi ningedhani Marekani angefurahia mshirika wa NATO kuwa na silaha za Urusi ili iwe rahisi kwake kuchunguza udhaifu wake>.
Vipi kipindi kile China na Russia walipokuwa wanapiga kelele kupinga THAAD kuwekwa South Korea unalizungumziaje hilo? Bila kusahau Russia anavyopiga kelele kuhusu kuwekwa Defence Shield ya Marekani pale Poland.
 
VITA NI TECHNOLOGY, TECHNOLOGY N UCHUMI. BAJETI YA MAREKANI BILA HATA VITA NI MARA 4 YA BAJETI YA URUSI. KWA LUGHA NYINGINE MAREKANI INAMUDU GARAMA ZA VITA MARA 4 YA URUSI. KUPIGA KOMBORA MOJA TU NI MILLIONS OF DOLLARS, PIA KUZUIA KOMBORA MOJA NI MILLIONS OF DOLLARS. PIA MAREKANI INA USHAWISHI MKUBWA DUNIANI KULIKO URUSI. PIA MAREKANI HAJAFUNGUA HAZINA YA SILAHA, HIZO S500 ANA KAMA HIZO MUDA, KAWEKA STOO.
 
Hiv zile ambazo zipo Syria ni s400 au Nini !?!maana israel anafanya kila apendalo huko syria na hiyo michumachuma ikiwepo au ni tofauti na hiz!?
 
Marekani kutaka kujua madhaifu ya S-400?

In Fact tayari kwa asilimia kubwa madhaifu ya S-400 yapo wazi na kuna njia mbalimbali tu za kukabiliana nazo ukiachana na Stealthy Technology ambayo imekuwa ikiipa Urusi wakati mgumu sana kukabiliana nayo.

Kwa upande wa Urusi, kama ni swala la kugundua udhaifu wa hizo ndege kumbuka S-400 zipo kule Syria chini ya Urusi ukiacha zile 'S-300'.

Tayari ndege za F-35 zimeshafanya Operations mbalimbali Syria zikifanywa na Majeshi mbalimbali ya anga kama vile RAF ya Uingereza na Israeli Air Force zikitumika Variants tofauti tofauti za F-35 na Urusi imekuwa ikizifuatilia kwa muda mrefu tu.

Hizo ndege ni ngumu sana kuzichunguza (Detect) na si kwamba hazionekani kabisa kwenye Radar. La hasha.

Kwa kutumia Low-Frequency Radars ambazo Urusi imekuwa ikiwekeza kwazo na kuzifanyia uboreshaji kwa muda sasa, inawezekana kuziona hizo F-35.

Tatizo ni kwamba kuiona tu F-35 ama F-22 kwenye Radar bado haitoshi.

Kuna zoezi la Interception ambapo ili zoezi lifanikiwe kuna michakato mbalimbali ambapo kwa hizo Low-Frequency Systems bado ni mtihani mkubwa sana kwa Modern SAM System yeyote ile kwa sasa.

Hilo ni kutokana na madhaifu yake ikiwemo 'Accuracy' ndogo hivyo ni ngumu kuyaongoza makombora kwa ufanisi kuelekea kwenye Targets husika.

Hapo zitahitajika High-Frequency Radars ili kuweza kuzifuatilia hizo ndege wakati wa kuzishambulia ambapo kwa hizo Radar kuziona tu hizo ndege mtihani unarudi palepale.

Hiyo ni kutokana na uwezo wa hizo ndege na jinsi zilivyoundwa kuziwezesha kuwa na vitu kitaalamu vikijulikana kama Low Radar Cross Sections katika hizo Frequency kubwa.

Isitoshe katika Operations kubwa hizi ndege huambatana pia na mifumo mingine ya kukabiliana na kuharibu mifumo ya ulinzi wa anga. Na hapo ugumu wa kuzishambulia hizo ndege unazidi kuongezeka.

Kuhusu Uturuki kinachohofiwa zaidi ni jinsi gani hiyo mifumo ya S-400 itajumuishwa ili ifanye kazi pamoja kitu ambacho hakitokwenda sambamba na mifumo ya ulinzi wa anga ya NATO iliyopo ambapo Uturuki ni mwanachama wake.

Je Uturuki watawezaje kuiendesha mifumo hiyo Separately bila kuleta matatizo ya kiusalama?

Kumbuka hata Urusi pia imekuwa ikisita kuzikabidhi zile S-300 moja kwa moja kwa mshirika wake, Syria aziendeshe sababu moja ni kuhusiana na maswala kama hayo ya kiusalama ikumbukwe kuwa Syria ilishawahi kuitungua ndege ya Urusi kimakosa na mifumo kama hiyo.
 
VITA NI TECHNOLOGY, TECHNOLOGY N UCHUMI. BAJETI YA MAREKANI BILA HATA VITA NI MARA 4 YA BAJETI YA URUSI. KWA LUGHA NYINGINE MAREKANI INAMUDU GARAMA ZA VITA MARA 4 YA URUSI. KUPIGA KOMBORA MOJA TU NI MILLIONS OF DOLLARS, PIA KUZUIA KOMBORA MOJA NI MILLIONS OF DOLLARS. PIA MAREKANI INA USHAWISHI MKUBWA DUNIANI KULIKO URUSI. PIA MAREKANI HAJAFUNGUA HAZINA YA SILAHA, HIZO S500 ANA KAMA HIZO MUDA, KAWEKA STOO.
Hiyo bajeti mara 4 usifananishe na pale ufipa wana bajeti kubwa ya kukodi jengo la nyumba nzima hali ya kuwa wanaweza kodi hata vyumba 2 mwaka huu na mwakani wakajenga lao,pale marekani bajeti kubwa wizi mtupu ila kwa mrusi hiyohiyo bajeti ndogo wenye uelewa kama waturuki wananunua vifaa,russia sio wa dunia hii kiteknolojia.
 
Urusi yuko vizuri kwenye Techinolojia ya Siraha.
Kuanzia Ndege za kivita, Nyambizi, Makombola, Meli za kivita, vifaru, Mitambo ya Ulinzi na kadhalika.

Ukitaja Top 5 ya either Vifaru, Helicopta, ndege, Meli, nyambizi, makombola na mitambo ya Ulinzi basi humukosi Murusi kwenye top 5 tena saa zingine akiwa na na mitambo miwili kwenye top 5
Kajifundishe kiswahili kwanza acha kushabikia Urusi mkongoman wewe.🤣


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Vipi kipindi kile China na Russia walipokuwa wanapiga kelele kupinga THAAD kuwekwa South Korea unalizungumziaje hilo? Bila kusahau Russia anavyopiga kelele kuhusu kuwekwa Defence Shield ya Marekani pale Poland.
Hivi unadhani Urusi akipeleka S-400 Cuba au Venezuela Marekani atakaa kimya? Mimi nimeweka wazi tu kile Marekani wenyewe wamesema kuwa udhaifu wa F-35 utakuwa wazi mbele ya Urusi kama zikikaa karibu na silaha za Urusi.
 
Marekani kutaka kujua madhaifu ya S-400?

In Fact tayari kwa asilimia kubwa madhaifu ya S-400 yapo wazi na kuna njia mbalimbali tu za kukabiliana nazo ukiachana na Stealthy Technology ambayo imekuwa ikiipa Urusi wakati mgumu sana kukabiliana nayo.

Kwa upande wa Urusi, kama ni swala la kugundua udhaifu wa hizo ndege kumbuka S-400 zipo kule Syria chini ya Urusi ukiacha zile 'S-300'.

Tayari ndege za F-35 zimeshafanya Operations mbalimbali Syria zikifanywa na Majeshi mbalimbali ya anga kama vile RAF ya Uingereza na Israeli Air Force zikitumika Variants tofauti tofauti za F-35 na Urusi imekuwa ikizifuatilia kwa muda mrefu tu.

Hizo ndege ni ngumu sana kuzichunguza (Detect) na si kwamba hazionekani kabisa kwenye Radar. La hasha.

Kwa kutumia Low-Frequency Radars ambazo Urusi imekuwa ikiwekeza kwazo na kuzifanyia uboreshaji kwa muda sasa, inawezekana kuziona hizo F-35.

Tatizo ni kwamba kuiona tu F-35 ama F-22 kwenye Radar bado haitoshi.

Kuna zoezi la Interception ambapo ili zoezi lifanikiwe kuna michakato mbalimbali ambapo kwa hizo Low-Frequency Systems bado ni mtihani mkubwa sana kwa Modern SAM System yeyote ile kwa sasa.

Hilo ni kutokana na madhaifu yake ikiwemo 'Accuracy' ndogo hivyo ni ngumu kuyaongoza makombora kwa ufanisi kuelekea kwenye Targets husika.

Hapo zitahitajika High-Frequency Radars ili kuweza kuzifuatilia hizo ndege wakati wa kuzishambulia ambapo kwa hizo Radar kuziona tu hizo ndege mtihani unarudi palepale.

Hiyo ni kutokana na uwezo wa hizo ndege na jinsi zilivyoundwa kuziwezesha kuwa na vitu kitaalamu vikijulikana kama Low Radar Cross Sections katika hizo Frequency kubwa.

Isitoshe katika Operations kubwa hizi ndege huambatana pia na mifumo mingine ya kukabiliana na kuharibu mifumo ya ulinzi wa anga. Na hapo ugumu wa kuzishambulia hizo ndege unazidi kuongezeka.

Kuhusu Uturuki kinachohofiwa zaidi ni jinsi gani hiyo mifumo ya S-400 itajumuishwa ili ifanye kazi pamoja kitu ambacho hakitokwenda sambamba na mifumo ya ulinzi wa anga ya NATO iliyopo ambapo Uturuki ni mwanachama wake.

Je Uturuki watawezaje kuiendesha mifumo hiyo Separately bila kuleta matatizo ya kiusalama?

Kumbuka hata Urusi pia imekuwa ikisita kuzikabidhi zile S-300 moja kwa moja kwa mshirika wake, Syria aziendeshe sababu moja ni kuhusiana na maswala kama hayo ya kiusalama ikumbukwe kuwa Syria ilishawahi kuitungua ndege ya Urusi kimakosa na mifumo kama hiyo.
Hiyo Drone ya Marekani iliyotunguliwa na Iran hutumia technologia ya stealth na ni ya gharama sana. Marekani hawakuamini kama Iran ingeweza kuiona na kuitungua, lakini ilidondoshwa na kombora la bei rahisi tu lakini la teknologia kali.
 
Hiv zile ambazo zipo Syria ni s400 au Nini !?!maana israel anafanya kila apendalo huko syria na hiyo michumachuma ikiwepo au ni tofauti na hiz!?
Jeshi la Syria halina S=400, bali lina S-200. Ila S-400 zilizopo Syria zinalinda kambi ya Jeshi la anga la Urusi lililopo Syria. Na hapo si Israel au Marekani anaweza kujichanganya. Hata hiyo S-200 huwa inatungua sehemu kubwa sana ya makombora ambayo Marekani na Israel huwa wanarusha ndiyo maana adui hurusha mamia ya makombora lakini yanayofanikiwa huwa machache vinginevyo hiyo nchi ingeshasambaratika zamani.
 
Marekani hana S-500 wala teknologia hiyo hana!!!! Mfumo wa kujilinda wa marekani ni kutumia Patriot ambao ni wa kizamani ndiyo maana Syria ikaamua kuchukua mfumo wa Kirusi badala ya huo wa Marekani. Urusi ndiyo ana hiyo S-500 na hiyo ni yake tu na hajaiweka sokoni bali kwa ulinzi wake tu!!!!
Hivi haushangai Taifa moja la Urusi linatambia mataifa zaidi ya 30 ya ulaya magharibi na mashariki akiwemo Marekani!!!!! Marekani alipeleka majeshi Syria ili kusaidia waasi kumwondoa Rais Asaad wa Syria madarakani. Urusi naye akatia Syria kuhakikisha Asaa anabaki madarakani na kuwasambaratisha waasi. Nadhani unajua ni nani aliyeibuka mshindi huko.
Na juzi juzi Marekani alitaka kumwondoa rais Maduro wa Venezuela ili kuweka kibaraka wake. Mrusi akatia timu na panya akajikuta kakaa kimyaa!!!!!
 
Ile drone yao waliipamba kama hivi unavyo zipamba ndege zao. ..Lakini walipigwa Bomba 1 tu chali. .hahaa Mpaka sasa hivi wapo kwenye maabara zao wana jikuna vichwa hawaamini walichokiona. ..wanadhani kuwa kilicho tokea ni njozi tu 'labda ipo siku itatokea wakaamka kwenye huo usingizi mzito
Marekani kutaka kujua madhaifu ya S-400?

In Fact tayari kwa asilimia kubwa madhaifu ya S-400 yapo wazi na kuna njia mbalimbali tu za kukabiliana nazo ukiachana na Stealthy Technology ambayo imekuwa ikiipa Urusi wakati mgumu sana kukabiliana nayo.

Kwa upande wa Urusi, kama ni swala la kugundua udhaifu wa hizo ndege kumbuka S-400 zipo kule Syria chini ya Urusi ukiacha zile 'S-300'.

Tayari ndege za F-35 zimeshafanya Operations mbalimbali Syria zikifanywa na Majeshi mbalimbali ya anga kama vile RAF ya Uingereza na Israeli Air Force zikitumika Variants tofauti tofauti za F-35 na Urusi imekuwa ikizifuatilia kwa muda mrefu tu.

Hizo ndege ni ngumu sana kuzichunguza (Detect) na si kwamba hazionekani kabisa kwenye Radar. La hasha.

Kwa kutumia Low-Frequency Radars ambazo Urusi imekuwa ikiwekeza kwazo na kuzifanyia uboreshaji kwa muda sasa, inawezekana kuziona hizo F-35.

Tatizo ni kwamba kuiona tu F-35 ama F-22 kwenye Radar bado haitoshi.

Kuna zoezi la Interception ambapo ili zoezi lifanikiwe kuna michakato mbalimbali ambapo kwa hizo Low-Frequency Systems bado ni mtihani mkubwa sana kwa Modern SAM System yeyote ile kwa sasa.

Hilo ni kutokana na madhaifu yake ikiwemo 'Accuracy' ndogo hivyo ni ngumu kuyaongoza makombora kwa ufanisi kuelekea kwenye Targets husika.

Hapo zitahitajika High-Frequency Radars ili kuweza kuzifuatilia hizo ndege wakati wa kuzishambulia ambapo kwa hizo Radar kuziona tu hizo ndege mtihani unarudi palepale.

Hiyo ni kutokana na uwezo wa hizo ndege na jinsi zilivyoundwa kuziwezesha kuwa na vitu kitaalamu vikijulikana kama Low Radar Cross Sections katika hizo Frequency kubwa.

Isitoshe katika Operations kubwa hizi ndege huambatana pia na mifumo mingine ya kukabiliana na kuharibu mifumo ya ulinzi wa anga. Na hapo ugumu wa kuzishambulia hizo ndege unazidi kuongezeka.

Kuhusu Uturuki kinachohofiwa zaidi ni jinsi gani hiyo mifumo ya S-400 itajumuishwa ili ifanye kazi pamoja kitu ambacho hakitokwenda sambamba na mifumo ya ulinzi wa anga ya NATO iliyopo ambapo Uturuki ni mwanachama wake.

Je Uturuki watawezaje kuiendesha mifumo hiyo Separately bila kuleta matatizo ya kiusalama?

Kumbuka hata Urusi pia imekuwa ikisita kuzikabidhi zile S-300 moja kwa moja kwa mshirika wake, Syria aziendeshe sababu moja ni kuhusiana na maswala kama hayo ya kiusalama ikumbukwe kuwa Syria ilishawahi kuitungua ndege ya Urusi kimakosa na mifumo kama hiyo.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom