Kumbe sheria inamruhusu mke kukopa mahitaji bila ridhaa ya mume na mume aje kulipa...!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,393
Kifungu cha sheria ya ndoa ya Tanzania ya mwaka 1971 kinaruhusu mke kukopa vitu ambavyo mumewe atakuja kuvilipa ilimradi tu vitu hivyo viwe ni muhimu kwa maisha ya familia. Hali inaweza kuwa tofauti kama mke akikopa dhahabu, manukato na nguo za kujipamba au pia kama angekopa vitu vya thamani kubwa kuliko ambavyo mumewe anaweza kuvilipa au vitu vingine ambavyo sio muhimu kwa ajili ya maisha yake na ya familia. Sheria hii inawabana zaidi wale wanaume wanaosafiri kwa muda mrefu huku wakiwa hawajaacha fedha za matumizi zinazokidhi mahitaji ya hapo nyumbani kwa kipindi chote watakachokuwa wako safarini. Au wale wanaotelekeza familia zao kwa muda mrefu bila kujulikana walipo na pale wanaporejea na kukutana na deni baada ya wake zao kukopa, wanakuwa hawana budi kulilipa, kwani sheria inawabana.

Hata hivyo kifungu hicho kimetoa tetezi mbalimbali ambazo mume anaweza kuzitumia ili kumuepusha na wajibu wa kulipa deni hilo. Mume anaweza kuepuka kulipa deni kama tu angekuwa ameshaachana na na mkewe au akiweza kuthibitisha kuwa mkewe anaishi maisha ya waziwazi ya uzinzi. Mfano, kama mume akithibitisha kuwa mkewe anatembea na huyo mwenye duka alipokopa na mtaa mzima unafahamu juu ya hilo, basi hatowajibika kulipa deni hilo. Pia kama akithibitisha kwamba alimpatia mkewe fedha za kutosha kukidhi mahitaji kwa kipindi chote alichokuwa amesafiri au kulikuwa na bidhaa za kutosha kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kwake au kama bidhaa zilizochukuliwa ni nyingi kuzidi uwezo wake wa kulipa, na hapa kiasi cha bidhaa kinaweza kuthibitishwa kwa rekodi aliyokuwa anaiweka mmiliki wa duka kwa bidhaa alizokuwa anamkopesha huyo mke mkopaji.

Sheria hii ni muhimu sana kwa sababu, inalinda familia kutoka kwa mume asiyetaka kutimiza majukumu yake ya kifamilia. Lakini mapungufu katika sheria hii ni kuwa imelalia upande mmoja kwa sababu, haimpi mwanaume uwezo wa kukopa pale mwanamke anapokataa kutimiza majukumu yake ya kifamilia. Labda itaonekana ni jambo la kuchekesha kidogo kwa wasomaji wa JF, lakini sheria hii hii ya ndoa ya Tanzania ya mwaka 1971 katika kifungu cha 63 (b) inampa haki mwanaume kulelewa na mkewe (maintenance) pale anapokuwa hana uwezo wa kuitunza familia kutokana na mapungufu kimwili, kiakili, au inapothibitika kuwa afya yake ni ya mgogoro na inapothibitika kuwa mkewe ana uwezo wa kutunza familia hiyo. Sasa inakuwaje pale mwanamke huyo anapokwepa wajibu wake huo?


Naomba Mods wasiipeleke hii thread kule jukwaa la sheria kwa sababu inawahusu wanandoa na ndio maana nikaiweka hapa MMU kwa faida ya wengi.
 
Aisee Mangi, utaniambia ilikuaje we uibebe familia yangu mwaka mzima wakati mi sipo!, siwezi kulipa aloo, labda kidogo nitafikiria kama mwenye duka ni mwanamke (napo nitaangalia alivyo alivyo, asijekua msagaji). Taratibu za makabila mengi, ikitokea unatakiwa uwataarifu ndugu pande zote waangalie utakavyoishi, ukikimbilia kwa bwashee, nikirudi ni taraka!
 
Aisee Mangi, utaniambia ilikuaje we uibebe familia yangu mwaka mzima wakati mi sipo!, siwezi kulipa aloo, labda kidogo nitafikiria kama mwenye duka ni mwanamke (napo nitaangalia alivyo alivyo, asijekua msagaji). Taratibu za makabila mengi, ikitokea unatakiwa uwataarifu ndugu pande zote waangalie utakavyoishi, ukikimbilia kwa bwashee, nikirudi ni taraka!
Bora hata akope kwa Mangi aiseee, je ikiwa ni kwa Mpemba.......................!
 
uonevu mkubwa sana
hasa kwenye kipindi hiki cha haki sawa
Si umeona jinsi inavyoshangaza eh..................Hizi sheria hazina mashiko wakati mwingine hasa pale inapohusu haki za mwanamke.
 
Ni moja ya sheria zilizo za kijinga sana kupita hata maelezo!

Hata mimi sheria hii imenishangaza kidogo, nikaona niwashirikishe wanaume wenzangu ili tutafakari kwa pamoja. Nashawishika kusema sheria hii inabidi ipitiwe upya. sijui hilo nalo ni kosa la kisheria kutaka sheria ipitiwe upya?
 
Ni moja ya sheria zilizo za kijinga sana kupita hata maelezo!

Sheria nzuri sana hiyo, na wanawake wengi zaidi wanapaswa kuifahamu


* naruhusiwa kukopa hadi asilimia ngapi ya kipato cha mume? :D
 
Ni sheria nzuri inasaidia kina mama

Sasa unasema inamnyima mwanamme fursa ya kukopa, mwanamme naye akope nini? sasabu ndo anategemewa kutunza familia. Akope uhausi?
 
Ni sheria nzuri kwa upande mmoja (mwanamke),lakini pia ni sheria mbaya kwa upande wa mwanaume.Kifupi kwa ujumla wakwe ni sheria yenye mapungufu lakini si mbaya mojamoja.Maudhui yaliomo kama - kuzuia kukopa kupita kipato cha wastani cha mwanaume,kukopa kwa nidhamu na uaminifu mwanaume anapokuwa mbali ni jambo zuri,ila kinachotakiwa ni kudai pia kiongezwe kipengele kama hicho kwa upande wa mwanaume lakini waongeze kwamba mwanaume anaweza kukopa bia kuanzia 1 mpaka 3...kwa sababu inampa akili ya kutafakari mwelekeo wa familia.

Kwa mwanamke liongezwe sharti la kutokopa vocha dukani na kutonunua vyakula vya anasa kama burger,mayonnaise,popcorn na sosage.Kwa mwanaume unayejali hebu gonga like kwa kila mwenye wazo kama hili ili kuboresha sheria kandamizi kama hii.

Asante Mtambuzi kwa kuleta mada nzuri.
 
Ni sheria nzuri kwa upande mmoja (mwanamke),lakini pia ni sheria mbaya kwa upande wa mwanaume.Kifupi kwa ujumla wakwe ni sheria yenye mapungufu lakini si mbaya mojamoja.Maudhui yaliomo kama - kuzuia kukopa kupita kipato cha wastani cha mwanaume,kukopa kwa nidhamu na uaminifu mwanaume anapokuwa mbali ni jambo zuri,ila kinachotakiwa ni kudai pia kiongezwe kipengele kama hicho kwa upande wa mwanaume lakini waongeze kwamba mwanaume anaweza kukopa bia kuanzia 1 mpaka 3...kwa sababu inampa akili ya kutafakari mwelekeo wa familia.

Kwa mwanamke liongezwe sharti la kutokopa vocha dukani....kwa sababu haitasaidia
Una akili sana wewe.....................!
 
Back
Top Bottom