Kumbe mwakani 2020 ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani

tatum

JF-Expert Member
Jan 16, 2018
5,788
4,490
Nakumbuka ni muda mfupi sana toka tufanye Uchaguzi Mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani na Rais Magufuli kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano yaano 2015 - 2020.

Tumebakiza muda mfupi sana kumaliza miaka mitano ya awamu ya tano na kufanyika tena kwa uchaguzi mkuu...nakumbuka ule mchakato wa uchukuaji wa fomu za uchaguzi kwa ngazi ya urais pale mgombea wa Chadema alipolisimamisha jiji la Dar kwa dakribani saa 3 mpaka 4 magari hayatembei mitaa yote ya mjini kiasi cha Polisi wa usalama barabarani kuacha mambo yajirekebishe yenyewe.

Toka nimeanza kushiriki katika uchaguzi kwakweli sijawahi kuona mtiti wa watu kama ule na sijui kama itaweza kujirudia tena hali kama ile.

Nakumbuka magezeti yalivyoandika kuhusu ule umati na jinsi Dr Kikwete alivyojibu kuhusu ule umati kuwa ni picha za kutengeneza tu kwa tecknolojia ya kisasa wala hakukuwa na umati mkubwa kama ule na hata mikutano mingine ilikuwa ikionekano mtiti wa watu kwenye magazeti.

Watanzania nawasifu sana kwa kuwa mabalozi wazuri wa amani kwakweli na hakukuwa na matukio yoyote ambayo yalitishia kuvunjika kwa amani wala vifaa vya uchaguzi na watumishi wa Tume ya Uchaguzi.

Ni matumaini yangu hata uchaguzi ujao wa 2020 kutakuwa na amani tele na viongozi watapatikana kwa mujibu wa sheria na kanuni za uchaguzi.
 
Uchaguzi wa 2020 utakuwa na amani endapo jiwe atakubari kushinda kwa asilimia chache tu atazozitapa ambazo hazitovuka 60% lkn akijifanya eti kama Mr slim kushinda kwa 99% hapo itakuwa ni ngolane mbondee munene aise

Sent using my iPhone using jamiiforum app
 
Ukiandika hvyo unampa stress Mzee ataongea hovyo manusurua atatembea uchi chezea kupokonywa mamlaka weweee

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe ndiye unajipa stress kwa kufikiri kwa njia ya ramli wakati wewe sio muhusika.

Hijasikua wapinzani wanakuambia mwaka 2020 hakuna uchaguzi kati ya CCM na wapinzani bali kuna Uchaguzi kati ya wapinzani na polisi. Sasa hizo stress azitoe wapi wakati hafanyi uchaguzi.
 
Sahihisho Jiwe hakushinda Sema alitangazwa mshindi na tume ya lubuva .Kazi imeshamshinda aishie hapa hapa tu mnataka mpaka awaambie vitendo hamuoni .
 
Vijana tunamsubiri kwa hamu Tundu Lissu, na rekodi mpya itaandikwa. Cha msingi Jiwe lisogezwe pembeni taratibu bila kubomoa kuta za nyumba
 
Kumekucha

Nasubiri kusoma watu wamejitosa kuwania uongozi.. tabu tutawajua kwa ID kujisema, bila hata kutupa matokeo..
 
Mleta mada anatutoa kwenye issue ya korosho. Sisi tunaunga mkono juhudi za kurudisha korosho kwa wananchi.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom