Kumbe mpenzi wangu ni mke wa mtu?

Kwa mtazamo wangu haiwezekani ukawa na mahusiano na mke wa mtu husigundue mwanzoni tu mwa mahusiano yenu, kwa ajili wewe umesema ni mwanafunzi kama na yeye ni mwanafunzi pia hapa naweza kukuelewa, kwamba yupo chuoni na wewe hupo chuoni na mupo free muda wote.
Kama yeye ni mtumishi wa afya hapo Dodoma na wewe ni mwanafunzi, unatakiwa kujifanyia tathimini wewe mwenyewe ni kwa jinsi gani hupo kwenye mahusiano na mke wa mtu ndani ya miezi saba bila kugundua (utakuwa na matatizo somewhere).
By the way ushauri wangu achana nae huyo mama, mwisho wenu hauta kuwa nzuri, especially kwako wewe pindi mumewe atakapo kubaini unammega mke wake.
 
Kimbia fasta tafuta mchumba mwingine ambaye atakuwa wa kwako peke yako uoe vinginevyo.....
 
Jamani, kwa takribani miezi saba nimekuwa na mahusiano ya kimapenzi na dada mmoja mwenye umri wa miaka 35, mwaka mmoja zaidi yangu! Ukweli mimi ni mwanafunzi na dada huyu ni mtumishi ktk idara ya afya hapa Dodoma, hivyo nikiwa na shida ya kifedha huwa ananisaidia sana!
Swala ni kwamba, hivi majuzi ndo kaniambia ya kuwa yeye ni mke wa mtu, lakini hajisikii kuendelea tena na mumewe ambaye wamezaa nae watoto wawili! Sababu ni kwamba bwana yule hana elimu na cha zaidi, anatumia vibaya pesa za biashara yake ambayo mtaji alipewa na mkewe huyo!
Swali, je unanishauri niendelee na huyu mwanamke ama nimuache?
Je nikiendelea naye mwisho wake ni nini?
Mke wa mtu sumu..na ni umauti ulio karibu!!
 
Yeye ni daktari (Doctor of Medicine- MUCHS), anadai mumewe ni form four tu! Mimi ninafanya masters, hivyo anaona mie ninamfaa zaidi! Ila ukweli ni kwamba, baada ya yeye kuniambia juu ya hili la mumuwe, ndo nikaanza kustuka ya kuwa hanipendi bure, bali elimu na sura! Hii ni kutokana na moangezi yake niongeapa nae! Ndo maana naomba ushauri.

Hicho ni kimeo akikutana na mtu anayefanya phd atakutema abaki n ahuyo wa phd angalia sana
 
Hivi mwanamke aliyeolewa na bahati mbaya mume amepata shida say Kisukari na hawezi kudo. Ataishi vipi huku sex ni muhimu pia kwa afya yake? NAULIZA TU.
 
Ha ha ha ha ha, hii mpya.

Kumbe unakuwa umewaacha dabali(double)?

Basi kuna wanamme humu wameshaachwa na wanamme wenzao ila hawajui lol

Mke wa mtu ukimwacha anaumia mara mbili, anaona kuwa alimuacha mumewe kukufuata wewe, sasa ukimuacha manake umemuacha yeye na mumewe!! Anaumia sana.....:israel:
 
hili ni tatito kubwa kwa wanandoa wanaoheshimu ndoa zao na familia wanapoanzana mmojawapo huwa ni wwanandoa sana sana mwanamke humkubalia kwasababu ni mapenzi ya muda mfupi mara nyingi wanafunzi wa vyuo akijua hatamusumbua akimaliza ataendazake kwihiyo wewe unafikiri umefika bado endelea shughuli zako usijepoteza muda
 
ulikuwa hujui ni mke wa mtu sasa ushajua achana nae.........unashindwa kumwacha sababu ya hivyo vihela anakupatia kumbuka alimpatia mumewe leo anamsimanga
 
mke wa mtu ukimuona muogope, hivi mume wake akikugundua ataku ulimboka ukotwe msitu wa pande, jihadhari kabla ya hatari
 
Kitendo cha kukuambia kuwa ana mme ina maana tayari keshkuchoka huyo anakuambia kuwa ondoka !!!! Maana kama ni sio hivyo angekuwa amkuambia hilo tangu zamanio. kwa nini leo? Kimbia na jamaa likijua umekufa na shule hujamaliza!! atakulimboka tu!!
Jamani, kwa takribani miezi saba nimekuwa na mahusiano ya kimapenzi na dada mmoja mwenye umri wa miaka 35, mwaka mmoja zaidi yangu! Ukweli mimi ni mwanafunzi na dada huyu ni mtumishi ktk idara ya afya hapa Dodoma, hivyo nikiwa na shida ya kifedha huwa ananisaidia sana!
Swala ni kwamba, hivi majuzi ndo kaniambia ya kuwa yeye ni mke wa mtu, lakini hajisikii kuendelea tena na mumewe ambaye wamezaa nae watoto wawili! Sababu ni kwamba bwana yule hana elimu na cha zaidi, anatumia vibaya pesa za biashara yake ambayo mtaji alipewa na mkewe huyo!
Swali, je unanishauri niendelee na huyu mwanamke ama nimuache?
Je nikiendelea naye mwisho wake ni nini?
 
kama anataka kumuacha mumewe awe na wewe, nini kinakufanya uhisi hatakuacha kwa ajili ya mtu mwingine akitokea?
 
kwamba mume wake hana elimu cyo hoja ya kutokuwa interested naye halafu na wewe mkuu unachohitaji kwake ni pesa ni hatari.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom