Kumbe Lusinde wa Chadema na Malecela walikubaliana kuachiana Jimbo

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
302
KATIBU wa CCM wa Wilaya ya Tarime, Livingstone Lusinde, amelalamikia viongozi wa chama hicho wilaya ya Chamwino, Dodoma kumruhusu mbunge wa Mtera, John Malecela 'kukampeni' kabla ya wakati.

Akizungumza jana na waandishi wa habari ofisini kwake, kuwa viongozi wa wilaya walionesha dhahiri kumpendelea Malecela kwa kumruhusu kufanya mkutano Dodoma Mjini.

Lusinde alifikia hatua hiyo baada ya kudai kushambuliwa na viongozi wa wilaya ya Chamwino, baada ya kutangaza nia yake ya kugombea Mtera Machi 7 mwaka huu, katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Alidai kuwa yeye na Malecela walikubaliana mwaka 2005 wakati Lusinde akiwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (chadema) na kuamua kipindi hicho alipohamia CCM.

"Mimi na Malecela tulikubaliana kuachiana nigombee ubunge wa Mtera ... nashangaa mara ya kutangaza nia yangu hiyo, nashambuliwa na viongozi wa wilaya, ninamtaka Mzee Malecela apinge kama hatukukubaliana mwaka 2005," alisema Lusinde.

Lusinde alikoti katiba ya chama cha mapinduzi ukurasa wa 21 kifungu kidogo cha katiba cha 7 ambacho kinasema ni marufuku jumuiya yoyote inayoongozwa na chama cha mapinduzi kumjenga ama kumbomoa mgombea yeyete mgombea mwingine.

Alidai ni haki ya kikatiba kutangaza nia ya kugombea na kusema yupo tayari kuacha au kufukuzwa na hata kusimamishwa kazi ya ukatibu wa CCM Tarime kama ni makosa yeye kugombea jimbo hilo.

Gazeti hili lilipowasiliana na Mwenyekiti wa Wilaya ya Chamwino Dodoma kuhusu kumruhusu Malecela kukampeni kabla ya muda na viongozi kumshambulia Katibu huyo mara baada ya kutangaza nia yake kugombea Mtera, Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Chamwino, Charles Uranga alikiri kufanyika mkutano Dodoma lakini haukuwa wa kumpigia kampeni Malecela.

Uranga alisema mkutano huo, ulikuwa wa kutoa tamko la kuzuia kampeni na kuhusu habari zilizotolewa na gazeti moja la kila siku alidai kuwa lilikosea.

Alidai kuwa gazeti hilo lilimkariri Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chamwino, Patrick Nyambuya, akidaiwa kushawishi Umoja wa Vijana wa CCM wa Wilaya hiyo, kumpigia debe Malecela atetee kiti cha ubunge Mtera jambo ambalo si kweli na kulitaka gazeti hilo likanushe habari hiyo.

Uranga alisema Katiba ya CCM inakataza kumuunga mkono mgombea mmoja na kwamba wagombea wote wanapewa demokrasia sawa wakati ukifika.
 
KATIBU wa CCM wa Wilaya ya Tarime, Livingstone Lusinde, amelalamikia viongozi wa chama hicho wilaya ya Chamwino, Dodoma kumruhusu mbunge wa Mtera, John Malecela 'kukampeni' kabla ya wakati.

Akizungumza jana na waandishi wa habari ofisini kwake, kuwa viongozi wa wilaya walionesha dhahiri kumpendelea Malecela kwa kumruhusu kufanya mkutano Dodoma Mjini.

Lusinde alifikia hatua hiyo baada ya kudai kushambuliwa na viongozi wa wilaya ya Chamwino, baada ya kutangaza nia yake ya kugombea Mtera Machi 7 mwaka huu, katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Alidai kuwa yeye na Malecela walikubaliana mwaka 2005 wakati Lusinde akiwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (chadema) na kuamua kipindi hicho alipohamia CCM.

"Mimi na Malecela tulikubaliana kuachiana nigombee ubunge wa Mtera ... nashangaa mara ya kutangaza nia yangu hiyo, nashambuliwa na viongozi wa wilaya, ninamtaka Mzee Malecela apinge kama hatukukubaliana mwaka 2005," alisema Lusinde.

Lusinde alikoti katiba ya chama cha mapinduzi ukurasa wa 21 kifungu kidogo cha katiba cha 7 ambacho kinasema ni marufuku jumuiya yoyote inayoongozwa na chama cha mapinduzi kumjenga ama kumbomoa mgombea yeyete mgombea mwingine.

Alidai ni haki ya kikatiba kutangaza nia ya kugombea na kusema yupo tayari kuacha au kufukuzwa na hata kusimamishwa kazi ya ukatibu wa CCM Tarime kama ni makosa yeye kugombea jimbo hilo.

Gazeti hili lilipowasiliana na Mwenyekiti wa Wilaya ya Chamwino Dodoma kuhusu kumruhusu Malecela kukampeni kabla ya muda na viongozi kumshambulia Katibu huyo mara baada ya kutangaza nia yake kugombea Mtera, Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Chamwino, Charles Uranga alikiri kufanyika mkutano Dodoma lakini haukuwa wa kumpigia kampeni Malecela.

Uranga alisema mkutano huo, ulikuwa wa kutoa tamko la kuzuia kampeni na kuhusu habari zilizotolewa na gazeti moja la kila siku alidai kuwa lilikosea.

Alidai kuwa gazeti hilo lilimkariri Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chamwino, Patrick Nyambuya, akidaiwa kushawishi Umoja wa Vijana wa CCM wa Wilaya hiyo, kumpigia debe Malecela atetee kiti cha ubunge Mtera jambo ambalo si kweli na kulitaka gazeti hilo likanushe habari hiyo.

Uranga alisema Katiba ya CCM inakataza kumuunga mkono mgombea mmoja na kwamba wagombea wote wanapewa demokrasia sawa wakati ukifika.

Lusinde wa chadema ndio yupi huyo mkuu..?
 
Mkuu Luteni pitia thread za nyuma, hii ilishawekwa hapa zamani.Asante
"Mimi na Malecela tulikubaliana kuachiana nigombee ubunge wa Mtera ... nashangaa mara ya kutangaza nia yangu hiyo, nashambuliwa na viongozi wa wilaya, ninamtaka Mzee Malecela apinge kama hatukukubaliana mwaka 2005," alisema Lusinde.

Nilifikiri maneno hayo juu ya Lusinde aliyoyasema jana ni mapya kumbe yameshajadiliwa ni thread gani mkuu naona ilinipita lakini ni maneno ya tarehe 24/3/2010
 
Huu upuuzi mtupu, kila mtu ana haki ya kugombea kwa wakati wake, hii ya tulikubakiana kuachiana haina mashiko. ndiyo yale yale yaliyomkuta yule kijana wa Rorya(jina limenitoka alikuwa kiongozi wa ngazi za juu daruso) na prof sarungi 2005.
 
mkuu luteni pitia thread za nyuma, hii ilishawekwa hapa zamani.asante


si mbaya akatukumbusha kaka
kuna ma thread ya ufisadi mia zaidi humu kila siku yanatoka hayo hayo na yanashambuliwa kwli......
 
si mbaya akatukumbusha kaka
kuna ma thread ya ufisadi mia zaidi humu kila siku yanatoka hayo hayo na yanashambuliwa kwli......
Ni kweli mbona ya Lowassa na Richmond pamoja na kufungwa bungeni bado inaongelewa hata hivyo yale maneno yametamkwa jana na Lusinde baada ya Malecela kupigiwa kampeni Dodoma Mjini.
 
Isije ikawa kuwa lusinde yuko upinzani na hiali ni ndugu yake kumbukeni hilo kwani Lusinde ni Koo za akina malecela
 
Isije ikawa kuwa lusinde yuko upinzani na hiali ni ndugu yake kumbukeni hilo kwani Lusinde ni Koo za akina malecela

Mkuu pata tano kwanza, Nami najua hao ni ndugu wa karibu sana, inanikumbusha mzee Malecela na Mzee Lusinde walivyohangaika pamoja na kuvunja taratibu za sheria kwa kumtetea Dr Madinda (marehemu) baada ya kuua akiwa anafanya Abortion pale Dodoma Hospital
 
Unajua Mwalimu Nyerere alikuwa na kipaji kama cha nabii kuona mbali. Ebu fikiria kama Malecela angeukwaa Urais. Si tungekuwa kama Niger? Kwa uchu wa madaraka lazima katiba ingebadilishwa tu. Sasa sikia poor Lusinde alivyogeukwa! Ahadi ya 2005 kuachiana ilikuwa danganya toto. Huyu ndie bwana Tingatinga!
 
Unajua Mwalimu Nyerere alikuwa na kipaji kama cha nabii kuona mbali. Ebu fikiria kama Malecela angeukwaa Urais. Si tungekuwa kama Niger? Kwa uchu wa madaraka lazima katiba ingebadilishwa tu. Sasa sikia poor Lusinde alivyogeukwa! Ahadi ya 2005 kuachiana ilikuwa danganya toto. Huyu ndie bwana Tingatinga!

alitukosesha opportunity ya mawazo mbadala...................
 
Lusinde wa chadema ndio yupi huyo mkuu..?

Alidai kuwa yeye na Malecela walikubaliana mwaka 2005 wakati Lusinde akiwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (chadema) na kuamua kipindi hicho alipohamia CCM.

"Mimi na Malecela tulikubaliana kuachiana nigombee ubunge wa Mtera ... nashangaa mara ya kutangaza nia yangu hiyo, nashambuliwa na viongozi wa wilaya, ninamtaka Mzee Malecela apinge kama hatukukubaliana mwaka 2005," alisema Lusinde.
Mkuu MawazoMatatu Lusinde ndiye huyo walikula dili na mzee mwaka 2005 wakati akiwa Chadema.
 
Kweli kuna kazi kubwa sana katika mambo haya maaana siasa za Tanzania ni za ajabu ajabu sana
 
Back
Top Bottom