Kumbe kusamehe ni kazi hivi?

Cheef Baroka

JF-Expert Member
Apr 28, 2019
491
1,000
Wakuu: Mimi ni miongoni mwa watu tunaopenda sana amani , napenda kuwa nafuraha muda mwingi, nafurahi zaidi mwingine anapofurahi au mambo yake yanapomuendea sawa.

Nimekuwa mtu nisie hifadhi chuki wala kuishi na vinyongo moyoni, nimekuwa nikipuuzia na kusamehe kila baya nalofanyiwa. Mimi ni mtu ambaye naweza kukwazika na mtu ila akija kunililia shida nikamsaidia nakusahau yote alonifanyia.

Mwaka 2010 kuna ndugu yangu (kaka) wa baba mmoja na mama mmoja matumbo mbalimbali, ye alikuwa anajishughulisha na biashara ya udongo (pemba) wanautoa kigoma kuja kuuza dsm. Binafsi sikupenda biashara ile coz nawaonaga wachafu muda wote, inatumia muda mwingi kukamilisha mzunguko (mana wananunua viroba vya udongo kutoka sehem panapoitwa Manyovu wanamwaga chini wanaponda na maji kama udongo wa tofali au kukandikia nyumba za tupe then wanafinyangisha, wanaanika , wanapakia kwenye mifuko then ndo wanasafirisha kuja dsm/ mlandizi ila sana ni DSM) , ni biashara yenye migogoro kwenye malipo, na sijaona mfano wa billionaire au hata millionaire alotokana au kupita kwenye hiyo biashara. So nikamuita tuyajenge, yeye akaniaminisha ile biashara inalipa sana kwamba pamoja na changamoto nilizoorodhesha but ina faida sana.

So siku moja nikapata vihela flani ivi kwa mbinde sana (mana me kipindi hicho sina mishe yyt bado npo school) nikaona kuliko kuhifadhi bank zikakaa tu ni bora niwekeze sehem pia nitapata na uzoefu wa biashara , ikabidi nikae chini na broo nikamkabidhi ile pesa aingize kwenye mzunguko wake azungushe ili nikuze mtaji mwisho wa siku nichukue pesa yangu ikiwa nyingi nikafanye ninachokipenda.

Brother akachukua ile pesa na kweli kazi ikaanza . Mwanzo nikashirikishwa kila hatua but soon nilipouliza faida ya mzunguko wa kwanza akanambia mdogo wangu me nina nia nikusaidie ko tufanye then nitakumegea fungu ukafanye yako. Baada ya hapo me nikawa bze na chuo nilipomaliza ikabidi nikaombe fungu sasa ili nianze harakati zangu duh! apo ndo picha likaanza broo akanambia Dogo mambo hayajakaa sawa ila suala lako linaniwazisha sana mana umekuwa unatakiwa kujitegemea ko nipe muda ,

Ikabidi nimuulizetu share yangu imefika sh ngap akasema nitakumegea kama m 4 nikamwambia broo 4 chache biashara imefanyika muda basi fanya 5 akasema powa ko ikabaki muda wa kukabidhiwa mtonyo. Basi ndugu yenu kichwa zaidi ya michoro ya KIPANYA nikajua matusua nikaweka plan kama zote ila wazo likanijia kuwa nikisema nimepata hiyo pesa nikafanye biashara ambayo sijawahi kufanya nitafeli so nikatufte mishe hata kwa kuajiliwa sehem ili hata pesa ikija inikute nina experience ya biashara apo ndipo nilipoanza kujichanganya kwenye mishe tofauti tofauti ikiwemo M-pesa, nafaka, viatu, nk huku nikijua pesa inakuja. Wakuu kiufupi ile pesa nikawa napigwa tarehe tu, ikaisha miaka miwili bado napigwa tarehe tu ,hadi naingia kwenye system bado pesa haijaja mwisho wa siku simu zikawa hazipokelewi wala sms hazijibiwi .

Haya: na broo mwingne tena (kaka yangu mkubwa) yeye alinipa kazi yakusimamia kazi yake ambayo walikuwa share na jamaa yake kiufupi malipo yake hata shilingi moja sijalipwa mpaka sasa na yeye simu hazipokelewi wala sms hazijibiwi. Nilipumuulza jamaa yake akanambia yeye alitoa pesa yote hadi ya usimamizi ko broo atakuwa kaila broo wangu. Wakuu inauma sana kutapeliwa na ndugu.

Nije kwenye point:

Ukweli ni kwamba kaka zangu hawa nafsi yangu imeshindwa KUWASAMEHE

najilazimisha sana lakini nashindwa. Najaribu kukumbuka zawadi walizonipa utotoni nakumbuka nikiwaomba vipesa vidogo vidogo wananipa, nguo,viatu na vitu kibao, Pia najaribu kuukumbuka msemo wa damu ni nzito kuliko maji ila pa1 na yote moyo unashindwa kusamehe hatimae unanikumbusha msoto nilopata kipindi natafuta ile pesa (kubeba, mawe, kubeba mizigo, kulima nk) nakumbuka msoto kipindi nasimamia kazi ya broo huyu mwingne (jinsi nilivyokuwa najitesa kufanya kwa ubora kama yangu, nalala masaa 3, natukanwa nk) nakumbuka muda nilopoteza nakumbuka walivyo nivurugia mipango yangu. Wakuu natamka haya kutoka Moyoni Wallahi nimeshindwa kuwasamehe.

Jamani nilikuwa nachukulia rahisi ila ndo nagundua "KUMBE KUSAMEHE NIKAZI HIVI " wakati mwanzo nilichukulia ni jambo simple sana.
Najiona nina kila sababu yakuwasamehe ila NIMESHINDWA KUSAMEHE.
 
Pole mkuu inabdi usamehe tu hakuna namnaa..!! So long bado upo hai bhasi usikatr tamaa endelea kutafutaa fanya kama Hakijatokea kitu na kupitia yaliyotokea hope umejifunza mengi
 
Pole mkuu tambua dunia hii aina mtu mwaminifu hata mke anaweza kukufanyia vitimbwi vya kutosha. Nakusihi Fanya kusahau na ujipe moyo kwamba ipo siku utapata zaidi ya hizo.

Hakuna kitu kibaya na kinachouma kama kutoelewana na ndugu zako huu utakuwa ni mwendelezo hata kwa watoto wenu mtatengeneza mazingira magumu ya kutopendana

Nakusihi acha kabisa pesa inatafutwa
 
Ukitaka uwe na marafiki Wa kudumu au ndg Wa uhakika, USIWAKOPESHE PESA. Acha kumkopesha hela ndg yako Bali unaruhusiwa kumpa tu kama msaada lakn sio kumkopesha Wa kumpa akutunzie..
Pesa sijui ina nini..yaani unaweza kumuazima jamaa yako kiasi fulani na ukawa mwisho wa ujamaa wenu
 
Nakuomba msamehe huyu mfanyabiashara. Biashara zinachangamoto sana na huwezi kuzielewa hadi uingie kwenye system.

Kukusanya 5M na mtaji usiyumbe sio kazi rahisi. Labda kama ni biashara yenye mzunguko mkubwa na mtaji wa kutosha.
 
“The higher the expectations, the greater the disappointment”

The rule is simple “don’t take everything too serious”

Haya maisha yana mambo ya ajabu kikubwa ni kutafuta amani ya nafsi na moyo wako.

Leo braza wamekufanyia hivyo kesho utakutana na mtu baki atakufanyia vivyo hivyo.

Moral of the story ni kwamba life isn’t easy as u presumed.

Once my uncle told me “Over the fence is not always ever green” I took some years to understand those words.

All in all life goes on. Heads up and move on bro and you’ll never walk alone.

#YNWA
 
Matifu ya undugu yamekuwa mengi mno, hapa jamii forum.

Samehe uwezi jua bila vikwazo vyao usingekuwa Apo, naamini mtu akikufanyia ubaya anakufungulia njia ingine ya balaka
 
Anza na kuwapenda utawasamehe tu, una mikono, miguu, macho yan ni mzima wa afya shukuru Mungu
 
Kusamehe ni rahisi kazi ni kusahau na Mungu anataka USAMEHE na USAHAU ndio msamaha wako utahesabika mbele za Mungu sababu kwa kusahau kwako manake huna kinyongo.

Tatizo wengi ni wagumu kusamehe na wakisamehe hawa sahau.
 
Kusamehe ni rahisi kazi ni kusahau na Mungu anataka USAMEHE na USAHAU ndio msamaha wako utahesabika mbele za Mungu sababu kwa kusahau kwako manake huna kinyongo.

Tatizo wengi ni wagumu kusamehe na wakisamehe hawa sahau.


Kwani swala la kusahau ni la kuamua kwamba "kuanzia sasa nasahau tukio fulani" au linatokea automatically?

Kusamehe ni tendo la hiari(kuridhia) ila kusahau ni mchakato unaofanywa na ubongo kulingana na uzito wa tukio kwa mhusika.
 
Kwani swala la kusahau ni la kuamua kwamba "kuanzia sasa nasahau tukio fulani" au linatokea automatically?

Kusamehe ni tendo la hiari(kuridhia) ila kusahau ni mchakato unaofanywa na ubongo kulingana na uzito wa tukio kwa mhusika.
Unaweza ukaamua vitu vingi ila kwenye kusamehe na ukasahau ukashindwa na ndio maana Mungu alishasema "........tusamehe dhambi zetu kama sisi tunavyo wasamehe walio tukosea.......,tusamehe na kusahau na tuwapende adui zetu...."

Kusamehe kunaanzia Moyoni alafu baada ya hapo ndio unakuja kufuta memory kwenye ubongo.So kama huna moyo wa kusamehe basi huwezi kulitoa hilo tukio kwenye ubongo wako.
 
Pole mkuu inabdi usamehe tu hakuna namnaa..!! So long bado upo hai bhasi usikatr tamaa endelea kutafutaa fanya kama Hakijatokea kitu na kupitia yaliyotokea hope umejifunza mengi
Natamani namimi ila nashindwa mkuu yani nafsi imefunga kabisa
 
Pole mkuu tambua dunia hii aina mtu mwaminifu hata mke anaweza kukufanyia vitimbwi vya kutosha. Nakusihi Fanya kusahau na ujipe moyo kwamba ipo siku utapata zaidi ya hizo.

Hakuna kitu kibaya na kinachouma kama kutoelewana na ndugu zako huu utakuwa ni mwendelezo hata kwa watoto wenu mtatengeneza mazingira magumu ya kutopendana

Nakusihi acha kabisa pesa inatafutwa
Shukran sana kaka. Nalitambua sana hilo ila ugumu ni kusamehe tu. Yani nafsi inafunga kabisa
 
“The higher the expectations, the greater the disappointment”

The rule is simple “don’t take everything too serious”

Haya maisha yana mambo ya ajabu kikubwa ni kutafuta amani ya nafsi na moyo wako.

Leo braza wamekufanyia hivyo kesho utakutana na mtu baki atakufanyia vivyo hivyo.

Moral of the story ni kwamba life isn’t easy as u presumed.

Once my uncle told me “Over the fence is not always ever green” I took some years to understand those words.

All in all life goes on. Heads up and move on bro and you’ll never walk alone.

#YNWA
Thanks alot broo but the problem ni kusamehe na kusafisha moyo kana kwamba hakuna chochote kilichotokea
 
Back
Top Bottom