GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,468
- 108,621
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo amefika nyumbani kwa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Dkt. John Magufuli wilayani Chato mkoani Geita kuangalia kaburi lake na kumjulia hali Mama yake Mzazi Suzana Magufuli.
Waziri Mkuu Majaliwa amefika nyumbani kwa Hayati Dkt. Magufuli akiwa safarini kuelekea mkoani Kigoma kuzindua kampeni za uchaguzi mdogo wa Wabunge katika majimbo ya Buhigwe na Mhambwe kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo katika uwanja wa ndege wa Chato alipokelewa na mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel.
Chanzo: tbc_online
Tafadhali ukitoka Kigoma katika Kampeni upitie pia na Butiama uzuru Kaburi la Hayati Mwalimu na usalimiane na Mjane Mama Maria.
Kisha ukitoka huko pita moja kwa moja hadi Kijijini Lupaso na ukazuru pia na Kaburi la Hayati Mkapa na pia utamkuta Kaka ( Mdogo ) wake utamsalimia pia.
Tanzania nzima Rais aliyefanya Makubwa na anayetakiwa Kukumbukwa na Kuenziwa vilivyo hakuwa huyu tu pekee na tujitahidi Kupunguza Unafiki.
Na Wengine tumeambiwa mlijifungia Vyumbani mwenu na Wake zenu mkifurahia 'Kutwaliwa' Kwake ghafla kwani alishawachokeni na alitaka hata Kutowarudisha tena hapo mlipo sasa sema tu 'Hirizi' zenu ziliwabeba.
Waziri Mkuu Majaliwa amefika nyumbani kwa Hayati Dkt. Magufuli akiwa safarini kuelekea mkoani Kigoma kuzindua kampeni za uchaguzi mdogo wa Wabunge katika majimbo ya Buhigwe na Mhambwe kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo katika uwanja wa ndege wa Chato alipokelewa na mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel.
Chanzo: tbc_online
Tafadhali ukitoka Kigoma katika Kampeni upitie pia na Butiama uzuru Kaburi la Hayati Mwalimu na usalimiane na Mjane Mama Maria.
Kisha ukitoka huko pita moja kwa moja hadi Kijijini Lupaso na ukazuru pia na Kaburi la Hayati Mkapa na pia utamkuta Kaka ( Mdogo ) wake utamsalimia pia.
Tanzania nzima Rais aliyefanya Makubwa na anayetakiwa Kukumbukwa na Kuenziwa vilivyo hakuwa huyu tu pekee na tujitahidi Kupunguza Unafiki.
Na Wengine tumeambiwa mlijifungia Vyumbani mwenu na Wake zenu mkifurahia 'Kutwaliwa' Kwake ghafla kwani alishawachokeni na alitaka hata Kutowarudisha tena hapo mlipo sasa sema tu 'Hirizi' zenu ziliwabeba.