Elections 2010 Kumbe kuna wabunge kumi wa chadema hawajatoka Bungeni Rais alipokua akihutubia bunge

kutokana na mdahalo wa jana nimesikia kua kuna wabunge kumi waligoma kutoka bungeni wakati wabunge wa chadema wakitoka nje ya bunge, yalielezwa na Hamad akijibu hoja ya Mbowe kuwa CUF inaonyesha kutowaunga mkono

jamani kwa nn hili hamlitaki kuliongelea

mjadala huo unaweza kuupata MZALENDO.NET « …Ni wakati wa ukweli na uwazi


- Mkuu una-raise a very interesting point na mimi jana niliona kwenye mdahalo, nikashitushwa sana kwamba kumbe kuna wabunge wa Chadema ambao hawakutoka nje ile siku, ikiwa na maana kwamba hawakukubaliana na ule uamuzi ambao at the heart of it ni kwamba Rais wa sasa ni wa halali na hakuna tatizo lolote na matokeo ya NEC,

- Very interesting point mkuu!


William.
 
Wabunge 10 wa CHADEMA walidinda ndani lakini CHADEMA kimya. Ukisikia kufyata mkia ndio huku...
 
Thanks kwa taarifa, mbona hata vyombo vya habari havijatamka juu ya hilo. Tupatie majina yao tuwajue "MATRAITORS".

JAMANI ujinga huu haujaanzia hapo tu, lazima tufuatilie tujue tabia zao toka utotoni na hata walipokuwa shuleni walikuwa ni watu wa aina gani.

hili ni funzo tunapochagua viongozi tusisome CV zao tu, maana CV za utotoni huwa hawaziweki.

Wengine unakuta walikuwa ni kina "TOTO TUNDU" waioambilika.

Wengine "TOTO JOGA" likigomwa kidogo tu Kiliooooo hadi majirani wasikie

Wengine " TOTO DEKA" kila kitu ng'eee ng'eee mama mie nataka ileee, mmm hii sitaki mama nataka ileeee!

wengine "TOTO JIZI" mama na baba wakiondoka nyumbani kazi kupekua masanduku au kuramba sukari.

sasa tusikurupuke kuchagua viongozi kwa kuangalia CV zao za masomo tu haya ndio matokeo yake.

kumbuka hata mashuleni tulipokuwa tukisoma, ukiwekwa msimamo fulani unakuwa wengine wanasepa haoooo huwaoni, au wale wanafunzi wa kujipendekeza, yaani likimwona teacher na mkoba, utaona hilo mbio kwenda mkumpokea, "shikamoo mwalimu".

VIJITABIA ni Kadhia kubwa inayotukabili ktk viongozi wetu wengi maana hawajaviacha vijitabia hivyo hadi sasa.
 
Baadhi ya wanaJF kila mnachokisikia mnakichukilia ni kweli bila kufanyia utafiti. Nadhani MTU WA PWANI na walioweka post za kuamini kilichosemwa na HR jana basi watutajie majina ya hao wabunge 10 wa Chadema waliogoma kutoka ndani ya bunge wakati JK anaanza kuongea la sivyo mnachokisema ni sawa na Udaku. Nachofahamu wabunge wa Chadema walioingia bungeni hiyo siku wote walitoka nje wakati JK alipoanza kuzungumza na kuna baadhi ya wabunge wa Chadema awakuingia kabisa bungeni hiyo siku.
 
Huwezi kusikia chochote cha maana kutoka kwa CCM B aka Zamani CUF! Kazi yao kubwa ni kuvunja nguvu za upinzani kulingana na matakwa ya CCM A
 
Sikweli asemalo Mtu wa pwani ukweli ni kwamba wabunge 10 hawaku ingia kabisa bungeni siku hio na sio waligoma kutoka bungeni
:hungry:
 
Baadhi ya viongozi wa CCM ni wagumu kuelewa, wakati Paul Kimiti akiwaonya viongozi wenzake wang'atuke kutokana na umri walikataa, matokeo yake wakaangushwa. Tusubiri tuu tuone kama CCM wataendelea kuwa wabishi wa kukataa katiba mpya.
 
- Mkuu una-raise a very interesting point na mimi jana niliona kwenye mdahalo, nikashitushwa sana kwamba kumbe kuna wabunge wa Chadema ambao hawakutoka nje ile siku, ikiwa na maana kwamba hawakukubaliana na ule uamuzi ambao at the heart of it ni kwamba Rais wa sasa ni wa halali na hakuna tatizo lolote na matokeo ya NEC,

- Very interesting point mkuu!


William.


Hamad katika hilo aliamua kwa makusudi kupotosha umma. Hao wabunge kumi ni wale waliopiga kura ya hapana kwa hoja ya kususia hotuba ya rais. Wabunge wote wa CHADEMA waliokuweko bungeni wakati JK akihutubia walitoka. wako wengine ambao hawakuingia kabisa akiwemo Zitto na Ndesa(correct me if wrong). Wote waliokuwepo ukumbini na wale waliokuwa wakifatilia matangazo ya TV waliona hili.

Anayebisha hili akatafute zile clip za tukio, isitoshe jambo hili lingeripotiwa na vyombo vya habari, mbona halikuandikwa??
 
Huyo Hamad si kama mwenzake Seif anachotaka nini zaidi ya kuwa kiongozi wa upinzani bungeni, huku chama chake kimeshinda Zanzibar tuu kwa kura chache kuliko jimbo la Ubungo.
 
Lakini kama unasema kuna Wabunge kumi hawakutoka mjengoni ni bora uwataje na sijui ni wewe tu ndio uliona hilo kweli kazi ipo......cha muhimu hapa ni kuelewa hao kumi hawakuingia Bungeni sababu kila mtu atakuwa na zake.

Sidhani kama hao wabunge 10 wangebaki mjengoni hili lisingeongelewa hadi leo hii.....na lazima tungelee mambo yaliyo ya kweli kama lingetokea ni wazi kuwa lingesha letwa hapa jamvini tusipotoshane kwa hili.
 
Hamad kasema yuko makini sana katika matamshi yake, aliposema "hawakutoka" alimaanisha wabunge waliamua kubaki bungeni siyo?

Na siyo wale ambao hawakuingia kabisa bungeni siyo?

Kwa sababu ukisema hawakutoka unatupa impression kwamba walibaki ndani ya bunge.

Umakini upo hapa au "mwanasiasa mkongwe" Hamad anajipigia debe tu, na tukija kwenye attention to details hayumo. Tena Hamad hawezi hata kusema Kiswahili ni lugha ya pili.
 
Hamad katika hilo aliamua kwa makusudi kupotosha umma. Hao wabunge kumi ni wale waliopiga kura ya hapana kwa hoja ya kususia hotuba ya rais. Wabunge wote wa CHADEMA waliokuweko bungeni wakati JK akihutubia walitoka. wako wengine ambao hawakuingia kabisa akiwemo Zitto na Ndesa(correct me if wrong). Wote waliokuwepo ukumbini na wale waliokuwa wakifatilia matangazo ya TV waliona hili.

Anayebisha hili akatafute zile clip za tukio, isitoshe jambo hili lingeripotiwa na vyombo vya habari, mbona halikuandikwa??


- Mkuu mimi huwa ninaongea facts, sijadili hadithi nenda kwenye clip za mdahalo utaona Mh. Hamad akisema haya maneno na hutaona Mh. Mbowe akikanusha kwamba sio kweli, mimi ninaongelea nilichokiona kwenye mdahalo tu!


William.
 
- Mkuu mimi huwa ninaongea facts, sijadili hadithi nenda kwenye clip za mdahalo utaona Mh. Hamad akisema haya maneno na hutaona Mh. Mbowe akikanusha kwamba sio kweli, mimi ninaongelea nilichokiona kwenye mdahalo tu!


William.
"selective memory"
 
Back
Top Bottom