Kibirizi
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 604
- 146
Kumbe hapo mwanzo watu wote tulikuwa weusi, ila katika ujio wa Mwenyezi mungu alipendezwa watu wote tuwe weupe sasa akaanza mchakato wakutubadilisha watu wa mataifa mbalimbali wakiwemo wazungu, waarabu wahindi, wajerumani n.k lakini wote tukiwa weusi. Basi Mungu alitengeneza bwawa moja kubwa sana, akwaita watu wa matifa yote na kuwaeleza kwamba ukiongelea kwenye bwawa lile utabadilika na kuwa mweupe, zoezi likaanza akatangulia mzungu kuogelea na akawa mweupe, akafuata mwarabu naye akawa mweupe na wakafuata wengine. Mwafrika akawa mbishi ana kiburi kwende kila inapofika zamu yake basi wakawa wanaenda watu wa mataifa mengine kumbe yale maji ya kwenye bwawa lile yalikuwa yanakauka kadri muda unavyozidi kwenda, basi mwafrika kuja kuzinduka na kuacha kiburi maji yapo kidogo sana, basi ikabidi aenda kuweka nyayo za miguu pamoja na viganja vya mkono ndio maana mpaka leo maeneo hayo ni meupe. tehe tehe kwikwi!