wa stendi
JF-Expert Member
- Jul 7, 2016
- 24,688
- 26,795
Nimemsikia bwana Gardner Habash mtangazaji mwenza wa marehemu Ephrahim Kibonde akisema kuwa usiku kule Mwanza kuna dawa pale hospital walikosa na akampigia simu Dr. Isaack maro akawaelekeza wakatafute maduka ya mtaani naa usiku ule wakakuta maduka yamefungwa.
Na baada ya kukosa hizo dawa walimjulisha bwana Maro kuwa imeshindikana usiku ule,na bwana Maro akawaambia kama mmekosa hizo dawa kesho mgonjwa ataamka akiwa hoi zaidi na kweli kesho yake ile alfajiri mgonjwa akaamka akiwa hoi hadi kumpelekea kushindwa kutembea kwa miguu hadi kupandishwa kwenye kile kiti cha matyre (whelchair).
Hivyo kwa namna moja au nyingine huenda wangefanikiwa kupata hizo dawa usiku ule marehem asingefariki dunia,kuwa ni uzembe wa hospital zetu kukosa dawa au kifo chake ilikuwa ni mipango ya Mungu.
R.i.p Kibonde, Mungu akuweke pahala pema
Na baada ya kukosa hizo dawa walimjulisha bwana Maro kuwa imeshindikana usiku ule,na bwana Maro akawaambia kama mmekosa hizo dawa kesho mgonjwa ataamka akiwa hoi zaidi na kweli kesho yake ile alfajiri mgonjwa akaamka akiwa hoi hadi kumpelekea kushindwa kutembea kwa miguu hadi kupandishwa kwenye kile kiti cha matyre (whelchair).
Hivyo kwa namna moja au nyingine huenda wangefanikiwa kupata hizo dawa usiku ule marehem asingefariki dunia,kuwa ni uzembe wa hospital zetu kukosa dawa au kifo chake ilikuwa ni mipango ya Mungu.
R.i.p Kibonde, Mungu akuweke pahala pema