Fiziolojia
JF-Expert Member
- Oct 19, 2019
- 819
- 1,079
Vifo vinavyotokana na ugonjwa wa Covid-19 nchini Brazili vinaendelea kuongezeka huku mamia ya watul wakifariki kila siku nchini humo, lakini rais Jair Bolsonaro amekuwa akitumia maneno mawili kuelezea hali hiyo: "Sasa iweje?"
Rais huyo kwa mara nyingine amewaomba raia wa Brazil warejee kazini, alipokutana na kuwasalimia kwa mikono na hata kupiga seilfie na wafuasi wake katika mkutano wa hadhara mjini Brasilia siku ya Jumapili (3).
Lakini anakabiliwa na ukosowaji mkubwa kwa kupuuza ugonjwa huo mara kwa mara.
Idadi ya wagonjwa waliothibitishwa kuambukizwa virisi vya corona vinavyosababisha ugonjwa wa Covid-19 nchini humo imepita 100,000, huku zaidi ya wa 7,000 wakifariki - idadi ambayo ni yajuu zaidi Amerika Kusini.
Lakini alipoulizwa na mwandishi wa habari kuhusu idadi ya vifo, ambayo ilikuwa imepita 5,000 siku ya Jumanne (Aprili 28), rais alisema:
"Sasa iweje? Samahani, mwataka nifanye nini? Siweezi kufanya miujiza."
Bw. Bolsonaro aliwahi kupuuza ugonjwa wa Covid-19 na kuutaja kama "homa kidogo tu" na kulaumu vyombo vya habari kwa kueneza taarifa ghushi ili kuzua taharuki katika jamii.
Huku hayo yakijiri, katika mitandao ya kijamii, kundi linalomuunga mkono rais lilichapisha picha za majeneza feki ambazo linasema ilizikwa bila kuwa na maiti ili kuongeza idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa huo.
Karibu wanahabari watatu walishambuliwa katika mukutano huo wa siku ya Jumapili ambao ulihudhuriwa na mamia ya waandamanaji waliokuwa wakishinikiza Bungea la Congress na mahakama ya juu zaidi kufungwa.
Shirika la habari la Reuterslilishuhudia mmoja wa wapiga picha wa gazeti la O Estado de S. Paulo akiburuzwa chini na kupigwa mateke mara kadhaa.
Chanzo:BBC
Rais huyo kwa mara nyingine amewaomba raia wa Brazil warejee kazini, alipokutana na kuwasalimia kwa mikono na hata kupiga seilfie na wafuasi wake katika mkutano wa hadhara mjini Brasilia siku ya Jumapili (3).
Lakini anakabiliwa na ukosowaji mkubwa kwa kupuuza ugonjwa huo mara kwa mara.
Idadi ya wagonjwa waliothibitishwa kuambukizwa virisi vya corona vinavyosababisha ugonjwa wa Covid-19 nchini humo imepita 100,000, huku zaidi ya wa 7,000 wakifariki - idadi ambayo ni yajuu zaidi Amerika Kusini.
Lakini alipoulizwa na mwandishi wa habari kuhusu idadi ya vifo, ambayo ilikuwa imepita 5,000 siku ya Jumanne (Aprili 28), rais alisema:
"Sasa iweje? Samahani, mwataka nifanye nini? Siweezi kufanya miujiza."
Bw. Bolsonaro aliwahi kupuuza ugonjwa wa Covid-19 na kuutaja kama "homa kidogo tu" na kulaumu vyombo vya habari kwa kueneza taarifa ghushi ili kuzua taharuki katika jamii.
Huku hayo yakijiri, katika mitandao ya kijamii, kundi linalomuunga mkono rais lilichapisha picha za majeneza feki ambazo linasema ilizikwa bila kuwa na maiti ili kuongeza idadi ya watu waliofariki kutokana na ugonjwa huo.
Karibu wanahabari watatu walishambuliwa katika mukutano huo wa siku ya Jumapili ambao ulihudhuriwa na mamia ya waandamanaji waliokuwa wakishinikiza Bungea la Congress na mahakama ya juu zaidi kufungwa.
Shirika la habari la Reuterslilishuhudia mmoja wa wapiga picha wa gazeti la O Estado de S. Paulo akiburuzwa chini na kupigwa mateke mara kadhaa.
Chanzo:BBC