Kumbe inawezekana kupeleleza wahujumu uchumi huku wenyewe wakiwa nje?

kagoshima

JF-Expert Member
Dec 31, 2015
2,628
5,133
Mbona mheshimiwa Lugola anachunguzwa yuko huru. Hebu wajuvi wa mambo tuelezeni. Kuna watu kadhaa wapo mahabusu kwa tuhuma za kesi za uhujumu uchumi bila dhamana takwa la kisheria (moja ya sheria kandamizi kwa mtazamo wa wengi).

Cha ajabu waziri wa zamani mambo ya ndani kangi lugola mheshimiwa yuko huru nje kwa makosa yale yale wengine wanasota sello.

Je, inchini kana ubaguzi namna ya ku implement sheria?
 
Watanzania wote wanajua utawala huu unaendesha uonevu wa kiburi cha madaraka kwa mgongo kwa kunyoosha nchi.

Wale wote wasiousujudia utawala huu wanabambikiwa kesi, huku wezi halisi wakilindwa kisa wanamashahiri ya kumtukuza mungu wa Tanzania.
 
Yule mchina kapelekwa mahakamani Jana leo kahukumiwa, safari hii mahakama umepata jembe kwelikweli
 
Mbona mheshimiwa lugola anachunguzwa yuko huru. Hebu wajuvi wa mambo tuelezeni. Kuna watu kadhaa wapo mahabusu kwa tuhuma za kesi za uhujumu uchumi bila dhamana takwa la kisheria (moja ya sheria kandamizi kwa mtazamo wa wengi ). Cha ajabu waziri wa zamani mambo ya ndani kangi lugola mheshimiwa yuko huru nje kwa makosa yale yale wengine wanasota sello. Je inchini kana ubaguzi namna ya ku implement sheria?

Ila usiombe hii ikukute wewe sasa...útajutaaa...

Utakaa ndani mpaka usahulike na ndugu zako
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom