Kumbe Hayati Magufuli ilibaki kidogo kumshtaki Karamagi mahakamani?

Suzy Elias

JF-Expert Member
Nov 9, 2021
1,067
6,192
Unaambiwa vyombo vya dola vilishaenda kumchukua kumpeleka kolokoloni kwa ajili ya kujibu tuhuma za kulisababishia Taifa hasara kupitia baadhi ya mikataba ya madini aliyoingia wakati akiwa Waziri akiiwakilisha Serikali.

Inasemwa mzee Mwinyi aliombwa na mmoja wa Viongozi mkuu mstaafu aende kumbembeleza JPM asifanye hivyo kwa sababu ya kumlindia heshima kwa sababu kwa vyovyote vile Karamagi angemtaja boss wake.

Inasemwa Karamagi alishajipanga kumtaja aliyekuwa kiongozi wake kama ndiye aliyemruhusu kuingia mikataba ile na yeye kama Waziri asingekuwa na uwezo wa kukataa maelekezo ya boss wake.

Ukweli ni kwamba JPM alipingana na mzee Mwinyi kuhusu kumlenga mkuu wa zamani wa mhusika bali lengo alitaka mhusika akajibu yeye kama yeye tuhuma zile baadae Jaji mkuu wa kipindi kile alimshauri JPM asitishe nia yake hiyo kwa sababu kwa vyovyote vile ilikuwa ni lazima mamlaka za uteuzi wa Karamagi zingeguswa na hiyo kesi jambo ambalo katiba ya Nchi inazuia.

Kumbukeni gesi iliyopo Mtwara Tanzania si ya Watanzania.

Nb: Huenda ndiyo JPM alikufa kifo chema!
 
Unaambiwa vyombo vya dola vilishaenda kumchukua kumpeleka kolokoloni kwa ajili ya kujibu tuhuma za kulisababishia Taifa hasara kupitia baadhi ya mikataba ya madini aliyoingia wakati akiwa Waziri akiiwakilisha Serikali.

Inasemwa mzee Mwinyi aliombwa na mmoja ya Viongozi mkuu mstaafu aende kumbembeleza JPM asifanye hivyo kwa sababu ya kumlindia heshima kwa sababu kwa vyovyote vile Karamagi angemtaja boss wake.
Ila Kikwete alituharibia nchi sana, nashangaa sana watu wanaomshadadia
 
Magufuli kama aliamua kupambana na hao jamaa angepambana nao mwanzo mwisho, kuliko kuwa na nia, uwezo, na sababu lakini akaacha kwa lengo la kuwalinda wastaafu.

Hata kama sheria inawalinda, lakini jamaa wangeweza kwenda mahakamani kama mashahidi, coz sio wao walioshtakiwa, kitendo cha JPM kuwaacha ndio aliharibu, leo wako mitandaoni wanamsema kila siku.

Wangepandishwa kizimbani watoe ushahidi, Karamagi kwenye utetezi wake angewataja, wenye akili timamu wangejua nani alikuwa muhusika mkuu hata kama sheria inamlinda.
 
Unaambiwa vyombo vya dola vilishaenda kumchukua kumpeleka kolokoloni kwa ajili ya kujibu tuhuma za kulisababishia Taifa hasara kupitia baadhi ya mikataba ya madini aliyoingia wakati akiwa Waziri akiiwakilisha Serikali.

Inasemwa mzee Mwinyi aliombwa na mmoja ya Viongozi mkuu mstaafu aende kumbembeleza JPM asifanye hivyo kwa sababu ya kumlindia heshima kwa sababu kwa vyovyote vile Karamagi angemtaja boss wake.
Huyo gpm wenu roho mbaya imefupisha maisha yake ya kidunia,

Zee lilitaka lifunge watz wote uraiani abakie yeye tu
 
Nakumbuka dege liliungurumishwa usiku wa manane kwenda kufanya bargain na kiongozi wa juu wa china, kulikuwa na mawili kuingia mkataba wa kinyonyaji hasa huu wa gesi ama prince anyongwe hadharani.

Hii nchi ilichezewa mno wakati wa awamu ya nne.
 
Magufuli kama aliamua kupambana na hao jamaa angepambana nao mwanzo mwisho, kuliko kuwa na nia, uwezo, na sababu lakini akaacha kwa lengo la kuwalinda wastaafu...
Magufuli alikuwa ni binadamu kama binadamu wengine kitu kilichomgharimu ni kutokuchukua hatua kwa mamlaka za juu za awamu iliyopita.

Hapa kuna kitu nimejifunza ukiwa moto kuwa moto kwelikweli maana hata maandiko yamesema ukiwa vuguvugu huna nafasi katika ufalme wa mbingu.

Na baada ya huyu bwana kutaka kujaribu kuanza kugusa baadhi ya watu na kuacha wengine hapo ndipo alipokosea wale aliowaacha ndio wakamuwahi yeye.
 
Back
Top Bottom