Kumbe hatuna wataalamu wa hili pia?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,927
Imeripotiwa Bungeni kuwa hatuna wataalam wa abirtration serikalini ndio maana serikali inabidi kukodi wataalamu binafsi kutuwakilisha katika kesi nyingi za abirtration na kuwalipa watu mamilioni. Katika Bunge zima ati ni Mhe. Phillip Marmo pekee ndiyo ana cheti kinachomtambua kimataifa..!

Sasa kwanini tusiamue kuomba wataalamu toka Ulaya tu?
 
Imeripotiwa Bungeni kuwa hatuna wataalam wa abirtration serikalini ndio maana serikali inabidi kukodi wataalamu binafsi kutuwakilisha katika kesi nyingi za abirtration na kuwalipa watu mamilioni. Katika Bunge zima ati ni Mhe. Phillip Marmo pekee ndiyo ana cheti kinachomtambua kimataifa..!

Sasa kwanini tusiamue kuomba wataalamu toka Ulaya tu?

Abirtration? ndo nini? nimeikosa hata kwenye dictionary saidia tafadhali kama hutojali sana.
 
Sasa kama hali ndo hii kwanini serikali isifanye mpango wa makusudi wa kupeleka timu ya vijana wakapate utaalamu nje kama hauwezi patikana nchini ili warejee kulitumikia Taifa?

Viko wapi vipa umbele vya Taifa letu?
 
Sasa kama hali ndo hii kwanini serikali isifanye mpango wa makusudi wa kupeleka timu ya vijana wakapate utaalamu nje kama hauwezi patikana nchini ili warejee kulitumikia Taifa?

Viko wapi vipa umbele vya Taifa letu?


Hatuna viongozi ndugu yangu...
 
Sasa kama hali ndo hii kwanini serikali isifanye mpango wa makusudi wa kupeleka timu ya vijana wakapate utaalamu nje kama hauwezi patikana nchini ili warejee kulitumikia Taifa?

Viko wapi vipa umbele vya Taifa letu?

Naweza nikawa natoka nje ya hoja kidogo...lakini itabidi tu ni seme kwa mara nyingine, vipa umbele vya taifa havieleweki kabisa. Kwenye hizi hoja za madini ambazo ziko kwenye kurasa za mbele kila siku kwenye magazetu yetu hapa nyumbani, serikali yetu ingetakiwa kuwa imeshatangaza nafasi kama 50 na zaidi za wasomi kuwapeleka nje ya nchi kuwanoa zaidi kwa ajili ya mambo hayo ili kukidhi haja ya nyanja hiyo badala ya kutoa matamko kila leo hii kuwa hatuna wataalam wakutosha katika sekta ya madini.

Kipa umbele chao ni kuona mashangingi yanatembea kila kona za jiji la Dar bila kukosa mafuta na kununua samani kutoka nje ya nchi ili kupamba maofisi yao.

Moja la karibuni ambalo naweza kulisifia ni lile serikali ililo lifanya la kupeleka wataalam wa mambo ya moyo kule India na Israel kwa ajili ya kujiandaa na kitengo maalumu cha upasuaji kitakacho wekwa Muhimbili (natumaini).

Kwenye madini napo basi wafanye hivyo hivyo. Wasitishe uchimbaji, wapeleke wataalam kuwanoa zaidi na wasuluhishi wake, ili baada ya miaka kama mitano tu, nchi iweze kuingia mikataba yenye maana bila kugharimika kiajabu ajabu kama ilivyo sasa... Kwa kweli subira nyingine zina maana na zina baraka kama tunajiandaa nazo, badala ya kukimbilia kutia sahihi mikataba tu na punde kujiona sote mapunguwani wanaochekwa na wale tulioingia nao mikataba.

SteveD.
 
Imeripotiwa Bungeni kuwa hatuna wataalam wa abirtration serikalini ndio maana serikali inabidi kukodi wataalamu binafsi kutuwakilisha katika kesi nyingi za abirtration na kuwalipa watu mamilioni. Katika Bunge zima ati ni Mhe. Phillip Marmo pekee ndiyo ana cheti kinachomtambua kimataifa..!

Sasa kwanini tusiamue kuomba wataalamu toka Ulaya tu?
Kwanini Ulaya?An arbitrator is an impartial person chosen by the parties to solve a dispute between them, who is vested with the power to make a final determination concerning the issues in controversy.

Nafikiri kuna watu wengi wana qualify!

Arbitrators are bound only by their own discretion, exercised within the scope of the authority entrusted to them by the parties rather than rules of law, equity, procedure, or evidence.

Whereas...Arbitration is the Process of resolving a dispute or a grievance outside a court system by presenting it for decision to an impartial third party. Both sides in the dispute usually must agree in advance to the choice of arbitrator and certify that they will abide by the arbitrator's decision.

...Settlement of a dispute after a hearing of opposing arguments, by an arbitrator, rather than a court of law.
Kwa kweli hakuna watu wengine wenye uwezo huu? ma Attorney je?...Unasomea wapi hii?. Tusaidiane!
.Source:Britannica Concise Encyclopedia ,http://www.answers.com
 
Imeripotiwa Bungeni kuwa hatuna wataalam wa abirtration serikalini ndio maana serikali inabidi kukodi wataalamu binafsi kutuwakilisha katika kesi nyingi za abirtration na kuwalipa watu mamilioni. Katika Bunge zima ati ni Mhe. Phillip Marmo pekee ndiyo ana cheti kinachomtambua kimataifa..!

Sasa kwanini tusiamue kuomba wataalamu toka Ulaya tu?
samahani abirtration ndio nini....
 
Sasa kama hali ndo hii kwanini serikali isifanye mpango wa makusudi wa kupeleka timu ya vijana wakapate utaalamu nje kama hauwezi patikana nchini ili warejee kulitumikia Taifa?

Viko wapi vipa umbele vya Taifa letu?

Wapeleke vijana halafu hizo pesa za consultation fee ama Arbitration fee watapataje 10% na nina hakika these people don,t come cheap na hata kama wataamua kupeleka watu kupata utaalamu usije ukashangaa kina Kingunge wakawa pale juu kwenye list ya wanaonda kupata hiyo taaluma.
 
Wapeleke vijana halafu hizo pesa za consultation fee ama Arbitration fee watapataje 10% na nina hakika these people don,t come cheap na hata kama wataamua kupeleka watu kupata utaalamu usije ukashangaa kina Kingunge wakawa pale juu kwenye list ya wanaonda kupata hiyo taaluma.

Kwikwikwi Kingunge tena?? yaani you have made my day! Japo inakera sana kuona na kusikia.
 
Imeripotiwa Bungeni kuwa hatuna wataalam wa abirtration serikalini ndio maana serikali inabidi kukodi wataalamu binafsi kutuwakilisha katika kesi nyingi za abirtration na kuwalipa watu mamilioni. Katika Bunge zima ati ni Mhe. Phillip Marmo pekee ndiyo ana cheti kinachomtambua kimataifa..!

Sasa kwanini tusiamue kuomba wataalamu toka Ulaya tu?

Kuna mengi sana yamefihika sirikalini, huu mwaka tutapata vioja vingi sana. Lakini chanzo cha yote haya ni nini?
 
Tutafika taratibu tu ndugu zangu. Si mnaona mabingwa wetu wanajaribu kuonyesha manjonjo yao kwa kumpasua mtu kibwa badala ya goti. Hizo ni moja ya mbwembwe za kitaalam kuwa mabingwa wa nyanja mbali mbali wanaendelea kunolewa katika kila sekta.
 
kazi kweli kweli........kila kitu serikali inasema hakuna pesa.

nafikiri kinachokosekana ndani ya serikali yetu ni mipango ya muda mrefu. serikali haipo tayari ku invest on people kwa ajili ya faida ya serikali ya awamu itakayokuja....na hapo ndio penye matatizo.

tunahitaji kuwa na mipango ya makusudi ya miaka 10 mbele na hata kuendelea. sio mitazamo ya mbele ya pua tu
 
Ndiyo yaleyale ya uongozi; tunawakabidhi walimu udaktari na madaktari ualimu, wapi na wapi. Sisi tunaloliweza pekee mpaka sasa hivi ni maombi kanisani na misikitini!
 
Jamani mi kumbukumbu zangu zinaniambia na Spika Sitta ni Mtaaluma kwenye hili jambo. Si ule mgogoro wa Mengi na Malima alisema ametumia busara za Spika kuwaita hawo mabwana kwenye arbitration table.
 
Imeripotiwa Bungeni kuwa hatuna wataalam wa abirtration serikalini ndio maana serikali inabidi kukodi wataalamu binafsi kutuwakilisha katika kesi nyingi za abirtration na kuwalipa watu mamilioni. Katika Bunge zima ati ni Mhe. Phillip Marmo pekee ndiyo ana cheti kinachomtambua kimataifa..!

Sasa kwanini tusiamue kuomba wataalamu toka Ulaya tu?

Bandugu, tatizo sio ukosefu wa wataalamu wa arbitration tanzania. Tatizo ni kuwa serikali imeshindwa kuwaajiri hao wataalamu kwa sababu gharama zao ni kubwa.

Kuna maswali ya kujiuliza hapa. Moja, hivi ni kweli katika vyuo vyetu vya elimu ya juu hapa tanzania hatuna uwezo wa kufundisha kozi kama hizo??? Kama kuna wahadhiri wa sheria wanaopita hapa JF, tungeomba kupata maoni yao. Mbili, kwa kuwa serikali inatambua kuwa tunao wataalamu wachache wa masuala ya arbitration kwenye sekta binasfi, ni hatua zipi ilizochukua mpaka sasa kuhakikisha ujuzi wa hao wataalamu wachache unasambazwa katika vyuo vyetu. Tatu,Kwa nini serikali kwa kushirikiana na chuo kikuu cha dar or mzumbe, isifanye utaratibu wa kumtumia mheshimiwa marmo kama muhadhiri wa arbitration katika hivyo vyuo???

Angalizo: Tuwe makini wana JF. Hii issue ya arbitration ni smokescreen. What the government is trying to do now is to provide yet another justifcation kwa nini serikali imeingia kwenye mikataba mibovu.

 
Ushauri wangu: In the short run, Marmo apangiwe kazi ya kufundisha wataalamu wa arbitration ili kulinusuru taifa katika gharama za kupeleka wataalamu wetu nje.In the long run, tufikirie kupeleka wanafunzi katika vyuo vya nje.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom