Kumbe hata kabla ya vyama vingi watu waliichukia CCM ! CHEKI HAPA.

EL MAGNIFICAL

JF-Expert Member
Jan 11, 2011
938
125
Imani yangu mu wazima ndugu zangu wana jf.
Poleni na ujenzi wa Taifa japo wengine wapo kwa ajili ya kubomoa.
Lengo la kuleta uzi huu hapa ni kuudhiilisha umma kuwa kumbe hata kabla ya vyama vingi, ccm ilianza kushindwa kuliongoza Taifa hili.
Yafuatayo ni mashairi ya mwanamuziki marehemu Remmy ongala, kwale wachambuzi wa fani na maudhui nafikili watanielewa ninachokisema hapa...
nyimbo: Nyerere.
msanii : dr. Remmy ongala.
mashairi.
Nyerere
Nyerere
kitu kikubwa nyerere amefanya
kitu kikubwa nyerere amefanya tanzania hii
kutukutanisha wote watanzania tule sahani moja
Ukiwa mbena eeeh ukitaka kwenda kuoa umasaini unakwenda bila wasiwasi
unakwenda unaopoa ngoma na uludi nayo
wakati wa nyerere hakukuwa na mgao wa umeme
wakati wa nyerere ccm ilikuwa tough sana
sio siku hizi ccm imemalizika, imemalizika, imekwisha, imekwisha kabisa
ccm imekwisa, imepitwa na wakati
Nyerere kitu kimoja umefanya eeeh wakati unang'atuka eeeh kwanini hukutuambia sisi wanyonge tumchague mtu tunayempenda
ona sasa nchi hii imeuzwa kwa wahindi na waarabu
wakati wa Nyerere kulikuwa na kanisa moja tu kulikuwa na msikiti mmoja tu, lakini siku hizi misikiti arobaini, makanisa hamsini, usiku hatulali eti utasikia amka amka ni uhuni huo.
Mwisho.
Wakuu mbali na wimbo huo kuonesha ccm haifai pia ntaomba kwa wale wataalamu wa uchambuzi niwakaribishe kwa hoja.
Aksanteni.
Nawasilisha.
 
Back
Top Bottom